Nakumbuka kipindi nasoma sekondari shule moja inaitwa mbweni iliyopo dar, shule hii iko kilometa4 kutoka barabara kuu hivyo ilibidi kutembea au kulipa 400 kutoka tegeta hadi shule, kutokana na hali duni ya kimaisha ilinibidi kutembea kilometa 8 kila siku.
Kwa wenyeji wa bunju wanajua kuna shule zaidi kama mbili zilizo karibu na barabara hivyo wanafunzi wa shule hizo walikua wanawahi kupata usafiri kuliko sisi ambao tulikua tunatembea kilometa 4, hali iliyokua inatufanya tuondoke kituoni baadhi ya siku saa 12 jioni.
Ilibidi tubuni njia ya mkato ili tutokee stendi ya bunju"B" ambako wanafunzi hawakua wengi.
Mkasa unaanza nakumbuka ilikua tunajiandaa kufanya mtihani wa taifa, siku ambayo nakumbuka niliondoka nyumbani mama akiwa anaumwa huku nikipewa 400 tu ya nauli bila hela ya ziada, kama kawaida nilienda shule kipindi cha mapumziko tukagombania uji na kuomba marafiki japo andazi siku iishe.
Ikafika muda wa kurudi nyumbani kama kawaida huku nikiwa na marafiki zangu lkn nilikua nawahi nyumbani maana nilikua sina raha nikiwaza hali ya mama, nilifika kituoni nikagombea usafiri nikafika nyumbani nikakuta mama kasharudi Hospital hali yake kidogo afadhali.
Siku ya pili masomo yaliendelea vizuri hadi mapumziko lkn hafla tukasikia kengele ya dharura tukakusanyika mstarini tukijiuliza kuna nini kimetokea?!
Mwl. Mkuu akatangaza watu wanaopita njia ile ya mkato ile ya bunju"B" wamefanya uhalifu mkubwa wameiba mahindi na kumpiga mlinzi wa shamba hilo hivyo amekuja kushtaki na kuwakamata wote waliohusika kwani anawajua,
Mwl. Mkuu akamwambia apite kila mstari awatoe wote anaowakumbuka walikuwepo kwenye tukio hilo, yule jamaa akaanza mstari mmoja mmoja kuanzia form1 hadi form4 huku akiwachomoa anaohisi walikuwepo au walihusika lkn hafla wakati anapita kwenye mstari wetu nikashangaa amenishika mkono nikataka kugoma lkn hafla nikashangaa bakira zinanimiminikia ikabidi nikubali tu.
Wote tukasimama mbele ya wanafunzi tukituhumiwa kuharibu na kuiba mahindi kwa kweli nilishangaa sana na hata wanafunzi wenzangu niliofuatana nao na hata wanaonijua walishangaa kwasababu sikua na tabia mbaya shuleni wala sikua mkorofi!
Tulisemwa sana na Mwal. Mkuu na walimu wengine huku tukipokea fimbo zisizo na idadi huku wanafunzi wakituzomea.
Baadae tukaambiwa tuandike barua kujieleza kwanini tusifukuzwe shule kwa kweli niliumia sana nikawa nalia huku nikijiuliza imekuaje nimemkosea nini Mungu, kwann wanafunzi wenzangu tuliofuatana nao hawakuja kunitetea wakati wanaujua ukweli kua nimesingiziwa?
Nilijiuliza maswali mengi sana itakuaje maisha yangu shuleni na darasani huku mtihani wa taifa ukikaribia?!
Mwalim mkuu alikataza kupita njia hiyo lkn nikasema moyoni sikubali lazma nipite nikaonane na yule jamaa huenda alipitiwa kunitaja mimi lkn ajabu nilivomuona nikamuuliza imekuaje kunitaja mimi wakati sikuwepo kwenye tukio na kama ningehusika basi nisingekuja shule,
Ajabu ya Musa na Firauni yule jamaa akanambia wengine anaweza kuwa na wasiwasi nao lakini sio mimi, aliniona na anauhakika kua nimehusika na akaishia kunitukana na kunifukuza.
Nilikosa amani lkn sikuwasimulia wazazi lilibaki moyoni mwangu hadi leo, nikikumbuka kesi hii machozi yananitoka!
SITASAHAU!