Nakumbuka kipindi fulani niko shuleni kuna demu mmoja nilikuwa na kabifu nae ka chini chini kabisa yule alikuwa rafiki angu sana,akasema mimi mjamzito na ni muathirika nina ukimwi. Nilikuwa nalia kila siku Dom watu wananicheka balaa,tena shule ya girls umbea unasambaa kama moto wa petrol kila kona unanyooshewa vidole. Nakumbuka nilimfata nikamuuliza kwanini unanizushia tuhuma hizi,mbele za watu huku akipaza sauti akasema ndio wewe una mimba na ukimwi kwani uongo? Watu walinicheka,walinizomea na kunisema vibaya juu ,Niliishiwa pozii hata ya kunyanyua mguu kutoka sikuwa na nguvu hivo, kuna dada alikuwa anatuzidi darasa ndio akaja kunitoa. She please me mpaka nikaacha kulia lakini moyoni nilikuwa na hasira kali na yule demu,nikaenda kwa matron nikamwambia nataka kupima ukimwi,matron alishangaa balaa akamuita mwalimu wa malezi still nika insist nataka kupimwa,wakanipeleka kufanyiwa counselling na mshauri wa wanafunzk nikagoma na kusimamia msimamo wangu ikabidi siku ile ile wanipeleke hospital wanipime,nikakutwa sina maambukizi wala mimba hapo nikaliamsha dude maana sikusema lolote kwao nilisubiri mpaka nipimwe wawe na uhakika,ilikuwa bonge la kesi akaambiwa aniombe msamaha assemble maana alitangaza taarifa za uongo karibia shule nzima ilijua, watu wakaanza kumzomea alivyokuwa anajielezea kwamba kanizushia sababu ya kibifu chetu kisicho na kichwa wala miguu.
Sitasahau ile ishu aseeee.