Ulishawahi kusingiziwa kitu?

Ulishawahi kusingiziwa kitu?

Nilisingiziwa kisawasawa na spicy señorita mmoja kuwa natoka naye na tumeshibana.
She had confessed some feeling about me, before that, but i was like meeh.
Basi mi nikaona sio mbaya tu-spend tha night moja matata, af tu-call it a history.
Long story short, lets just say, THAT NIGHT WAS A MISTAKE aisee.
Kashfa hiyo ilichukua muda mrefu kuisha huku ikiambatana na drama kibao.
I couldnt reverse shit!
But I learned my lesson kwamba some women sio wa kuwachezea feelings. Hands down!
 
mimi kuna mtu alinisingizia mambo mengi tu hiyo ni baada ya kumfuma kwenye tank langu anaiba maji na hapo tulikuwa tumenuniana nikaamua kumshtak kwa mwenye nyumba wacha anishuhudie uongo ambao hata sikuwah kuuona dunia hii kubwa zaid akanisingizia natembea na mumewe jaman wakat huyo kaka hata mazoea nae sina yan nilikasirika nilimbamiza pale pale mbele ya kikao cha watu wanne!!! had leo adabu na heshima @sitakag ujinga mimi usio na maana
 
Kusingiziwa kupoo, mfano mimi navyokusingizia mleta uzi wewe ndio chanzo watu wana chat badala ya kupiga kazi
 
kuna watu wanajua kuwashuhudia uongo wenzao hata shetan hawataki! kuna dada niligombana nae tu kisa mambo ya umbea umbea nikapiga zangu kimya bas akawa ananipiga vijembe vya waz waz,

nilivumilia sana sasa siku ya siku alijua nimeenda job kumbe nipo ndan akawa anachota maj yangu kwenye tank ,mi nikamuacha tu ajaze namchungulia tu dirishani alipokuwa anamalizia ndoo ka mbil nikatoka wacha ashtuke nikamwambia tu malizia coz toka unachota nimekuwa nakuona

alinyanyua ndoo zake akaingia ndani, bas huko ndan akawa anajipigisha simu kuzuga ili nimuogope ooh et nilikuwa namtafuta siku nyingi nimekaa na hiki kitu miez mitatu nilikuwa namsubir aingie kumi na nane zangu

mi nikaona isiwe shida ye si mshari nikaenda kumsemea kwa mwenye nyumba, tukaitwa kikao cha watu watano bas nikaongea vyangu had kulichosababisha sis kununiana, ilipofika zamu yake alinisemea uongo mwingi sana had kumwimbia hotpot zake na kubwa et nimetembea na mumewe!

jaman nilichukia saaana ukizingatia mambo yote aliyonishuhudia ni uongo nilikasirika had nwisho nilinyanyuka nikamtia misumbwi.ya maana iliyoenda shule tena ile ya hasira mbele ya kikao had wanakuja kugombelezea tayar mtu sura haifai yan had leo ni adabu na heshima ananiheshimu na tunaongea, nilimsamehe
Daah hapoo kwa kumuibia mume tenaa..!! Sema usingempigaa wew ungefanya kweli sasa...
 
Daah! Aisee nilishawahi singiziwa kitu cha ajabu sema nimekisahau ningewambia.
 
Mchumba wa Rafiki yangu alikuwa ananitaka Kimapenzi nilimkatalia na ''kumtolea macho'' kwa hasira........ akaniomba yaishe na nisimueleze yeyote hatarudia tena............Ikafika wakati wanafanya Sendoff yake wakati tunatoa zawadi kwa bibi Harusi Mtarajiwa.......Nilipompa Mkono wa kumpongeza....................Eeeeeeeeeeeebwanaeeeeeeeee aliangua Kilio huku akisema Nimemfinya.........Nilitolewa Nje Mzobemzobe nilivunjiwa heshima siku ileeee sitasahau maishani.............................!!!!!!
 
Mchumba wa Rafiki yangu alikuwa ananitaka Kimapenzi nilimkatalia na ''kumtolea macho'' kwa hasira........ akaniomba yaishe na nisimueleze yeyote hatarudia tena............Ikafika wakati wanafanya Sendoff yake wakati tunatoa zawadi kwa bibi Harusi Mtarajiwa.......Nilipompa Mkono wa kumpongeza....................Eeeeeeeeeeeebwanaeeeeeeeee aliangua Kilio huku akisema Nimemfinya.........Nilitolewa Nje Mzobemzobe nilivunjiwa heshima siku ileeee sitasahau maishani.............................!!!!!!
Daah maskini... sasa umemfinya mpaka akalia!??? Duuh visa hivi
 
Pole
Hakuna kitu kinaumiza kama kusemewa uongo, ingawa wengi husema ukweli unauma, kwangu uongo huniumiza zaidi.
Mmh. Unatabia mbaya wewe. Yaani umesahau kabisa ile njia ya kuja kwangu vibaya hivyo shoga yangu.

Mzima?
 
Back
Top Bottom