Ni kweli, ngoja na mimi nishushe kwa mara ya kwanza masihara yangu ya “mke wa mtu” ambayo haikukamilika lakini ili labda itoe funzo kwa wazee wa masihara yanayohusu wake za watu! Wiki tatu zilizopita nilipanda Happy Nation ya kwenda Bukoba kutoka Dar, huku mimi nikiwa nashukia Dodoma! Siti yangu nilikaa na pisi flani kali kiaina/sister duu na inayovutia
! Niliikuta imeshakaa hivyo tukawa siti ya wawili tumekaa nayo! Ikawa ni kama na usingizi flani hivi! Kufika Chalinze tu ikaniomba samahani “kaka samahani naweza kulalia hapo?!” Nilikuwa nimebeba kibegi kidogo mkononi, nikasema sawa
! Ikalalia serious, na nilipoona imelala kabisa na ku relax nikaanza kupitisha mikono taraatiiib kuanzia kwenye shingo, mgongoni, na kuja kwenye kiuno
! Ikawa imetulia tulii na mi naendelea flani kwa kuibia! Nikataka nije kwenye uzi pendwa ili wazee wa masihara mnipe mwongozo, mara nikapotezea kwa kujiamini kwamba ngoja leo na mm nijaribu zari
! Nilifanikiwa kuishika hadi kiuno (nyama kwa nyama siyo juu ya nguo
!). Mara nikashikwa na mshangao mkuu! Jamaa wa siti ya mbele yetu kulia (dirishani) akageuka nyuma na kukuta pisi imenilalia kwenye mapaja (juu ya kibegi
), jamaa akamshtua demu kwa ukali “wewe ebu amka, ujinga gani huo unafanya! Nitakutandika makofi mbele ya watu, halafu wewe brother naomba huyo mtu asikulalie tena! Demu akajitoa kwenye mapaja yangu! Kufika mbele baada ya kama lisaa jamaa aligeuka kucheki akakuta tumekaa kawaida tu. Mara demu akanionyesha simu yake nisome “plz kama una bando naomba uniunge sina internet” nikamjibu, sawa na kweli nikamuunga atumie WiFi yangu
! Muda huo huo tukapeana namba na kuanza kuchati
! Nikamuuliza “huyo jamaa aliyekukaripia ni nani, unamfahamu?! Demu akanijibu “ndiyo, huyo ni mme wangu! Tumepana kama mwaka sasa na nusu lakini tumekuwa na ugomvi na hatuelewani hivyo tumekubaliana tuachane, hivi hapa tunaenda Bukoba ili tukaongee kifamilia!!! La haula, nikashtuka na kuwaza kuwa hizi masihara hizi
!!! Naomba niiishie hapa kwa leo!