The Sheriff
JF-Expert Member
- Oct 10, 2019
- 617
- 1,800
Mnamo mwaka 2020 Gavana wa Machakos Dkt. Alfred Mutua alizindua makao makuu mapya ya kaunti hiyo. Jengo hilo jipya, ambalo linafananishwa na Ikulu ya Marekani - lilifunguliwa rasmi Jumatano, Mei 6, 2020 baada ya ujenzi wake kukamilika kwa gharama ya kiasi cha fedha Ksh. 350 milioni ambazo ni zaidi ya Bilioni 6 za Tanzania.
Mnamo tarehe 20 Mei, 2023 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan aliongoza uzinduzi rasmi wa Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma ambapo Rais na watumishi wengine watahamia katika Ikulu hiyo. Ujenzi wa Ikulu hiyo umegharimu zaidi kiasi cha fedha Ksh. 175 milioni ambazo ni zaidi ya Bilioni 3 za Tanzania.
Ikulu ya Serikali iliyoko Dar es Salaam ilijengwa na wakoloni, hata hivyo, Ikulu ya Chamwino inajivunia ujuzi na nguvu kazi kutoka kwa wenyeji kwa kupitia Jeshi la Kujenga Taifa la Tanzania (JKT). Ujenzi huo kutekelezwa na JKT kunaelezwa kusababisha kupungua kwa gharama za ujenzi huo.
Mnamo tarehe 20 Mei, 2023 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan aliongoza uzinduzi rasmi wa Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma ambapo Rais na watumishi wengine watahamia katika Ikulu hiyo. Ujenzi wa Ikulu hiyo umegharimu zaidi kiasi cha fedha Ksh. 175 milioni ambazo ni zaidi ya Bilioni 3 za Tanzania.
Ikulu ya Serikali iliyoko Dar es Salaam ilijengwa na wakoloni, hata hivyo, Ikulu ya Chamwino inajivunia ujuzi na nguvu kazi kutoka kwa wenyeji kwa kupitia Jeshi la Kujenga Taifa la Tanzania (JKT). Ujenzi huo kutekelezwa na JKT kunaelezwa kusababisha kupungua kwa gharama za ujenzi huo.