Pasta hujanielewa, umekazana na kufoka
sijui umeshalewa, ama kufungwa na Kaka
ubeti (#)3 waongelewa, posti sabini na tatu
sa sema uongo upi, kama si kujifanya fisi!!!!!!!
Muongo umeniita, adui asiye haya
Betizo ukazikita, muovu tena mbaya
Heshima umeipita, penye uso wa duniya
Kwa kuniita muongo kwa kosa langu ni lipi
Pombe adui wa siha, si matunda ya mwilini
Uso meumbwa na haya, sithubutu asilani
Sihiweki kwenye kaya, madhambi hao ya nini
Matendo mtu mlevi, kinyume na yangu dini
Viumbe kuwaheshimu, tulifundishwa mapema,
Wadogo na wamakamu, wote hupewa heshima,
Twakatazwa kudhulumu, hata porini wanyama,
Adabu tabia njema, pambo langu Islamu.