Elections 2010 Ulimi wamponza Yusuf Makamba

Makamba hakika hakuteleza ulimi wala nini, ni hulka yake na wala si uzee unaomsumbua. Anawakilisha wanaccm wengi ambao hawaoni tatizo kutambia wakazi wa Kipawa na gongolamboto hatuna shida na kelele za ndege kubwa.

Hawataki mdahalo unaohudhuriwa na watu wa kariakoo kwa kuwa ni watu wa kariakoo ambao hawaoni kama sera za ccm zimekuwa na kitu kipya zaidi ya kuwaneemesha wachache na familia zao ambao kwa kila hali wanajitahidi waendelee kushika madaraka
 
Wakati mwingine huwa siamini kama January na Mwamvita ni watoto wa huyu mzee mropokaji!!

Naamini maneno anayoyatamka mara nyingi hayafai hata kutamkwa na balozi wa nyumba 10 wa CCM. Its a disgrace to his party, his Chairman na watanzania wote kwa kuwa na mzee wa jinsi hii.

Nakumbuka kusoma kwenye blog ya January maandishi yafuatayo..."wakati mwingine ni bahati mbaya sana unajikuta unarithi maadui wa baba yako....watu wanakuangalia na kukuona kama mtu wa aina ya baba yako....." Hii statement to me inamaana kwamba January anajua fika mapungufu ya baba yake lakini ndo hivyo tena huwezi kuchagua baba wa kukuzaa!!
 
Safi sana. CCM inajikaanga kwa mafuta yake yenyewe.

Tulisema mengi kuhusu Makamba kwamba ni mropokaji, hafai kuwa nafasi ya juu chama chochote.Tulisema kuwa CCM ya kina Makamba na JK imekumbatia matajiri na mafisadi na kuwasahau watu Maskini, ambao kwa upande moja imewasababishia umaskini, lakini wengine wakapinga.

Tuelewe kuwa CCM haina na muda kwa maskini. Hao wa Kariakoo ni mfano tu. Walipokuwa wanawasomba na magari ili wafike Jangwani kwenye mkutano wa ufunguzi wa kampeni msidhani wanapenda, ni kwa sababu walitaka kujaza uwanja, ionekane CCM inapendwa.

Maskini tupo wengi. Tunataka suala la njaa lisiwe mjadala ya miaka yote. CCM haina nia ya kumaliza njaa yetu. Tukirudisha madarakani tusibiri matusi zaidi.

Natumaini hadi sasa kila moja amekwishaona Chama gani kina nia thabiti ya kuwatoa wanzania kutoka lindi la umaskini, ila sio CCM.

Wanakariakoo, hakuna sababu ya kuhangaika na Makamba, eti aombe msamaha. Ni kutumia kura yako tu hapo Oktoba 31.
Kariakoo ndo inayoipa ushindi CC'EMU kila kipindi, Makada na wazee wengi wa sisisem hadi mbunge wa ILALA "ZUNGU" la Unga ambalo halijawai hata kuonge neno moja bungeni limechaguliwa na watu haohao wa Kariakoo.
 
huyo hasa ndio kiboko yenu

maana hamlali kama hamjamtaja

na komesha kwenu, maana huenda hata jimbo mspate mwaka huuu
 
CCM huwa haiwajari wateja wake ie wapiga kura.
Mramba alishawai sema tutakula ata Nyasi ndege ya raisi lazima inunuliwe.
Personally nshawazoe bse hatuwezi watia bakora kwa kutowapigia hasa baada ya kupewa kofia,khanga na fulana
 
CCM ni chama kilicho sheheni wasomi, madaktari, maprofesa na mainjinia kibao... lakini wote wamekubali kuongozwa na waropokaji, wapenda majungu na watu waliojaa kashfa zisizo kipimo!!

Ama kweli kama elimu za darasani tu ndizo zingelikuwa kigezo cha ukombozi... hakika Taifa hili lingekuwa miongoni mwa G20 tayari!!!
 
January is far better than his dad

Makamba nimefurahi yamekukuta maana wewe ni bingwa wa kubeba kauli za watu na kuzipigia filimbi, muosha huoshwa

LOL

LIKE FATHER LIKE SON..au unaposema January is far better unamaanisha "FAR BETTER IN TALKING CHEAP SHIT than his dad"?
 

Ulimi wamponza Yusuf Makamba

• wakazi Kariakoo wadai amewadhalilisha
• Washinikiza aombe radhi, ajiuzulu


Kauli iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bw Yusuf makamba kuhusu ombi la mdahalo la mgombea ubunge kupitia chama hicho Jimbo la Urambo Mashariki, Bw Samuel Sitta na mgombea urais kupitia Chadema, Dk Wilbrod Slkaa, imezua mtafaruku miongoni mwa wanachama wa chama hicho.

Mwishoni mwa wiki iliyopita, baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kuwa CCM imenawa mikono na haihusiki na mgogoro baina ya wanasiasa hao huku vikimkariri Bw Makamba akisisitiza kuwa Sitta na Dk Slaa, wana mambo yao wenyewe na wala hayakihusu chama hicho.

Bw Makamba alikaririwa akisema CCM kimekataa midahalo kwa sababu hukusanya watu wa hovyo na hakuna mikakati maalum ya kuiendesha kwa kujieleza na kukosoana kulingana na sera za vyama husika.

Alisema chama hicho hakiogopi midahalo, bali kisingependa kuona kinashiriki kwenye midahalo kwa sababu zinaweza kuibuliwa hoja zisizo na msingi kwa makusudi ya kukichafua.

“Tunataka mdahalo uwe wa sera. Sio unakusanya watu wa Kariakoo halafu anajitokeza miongoni mwao ambaye jana alilala njaa halafu anasema jana CCM ilitulaza njaa,” alinukuliwa akisema Bw Makamba.

Kitendo cha Bw Makamba kutolea mfano wakazi wa eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam kimezua mtafaruku miongoni mwa wananchi hao na kuwafanya baadhi yao kufika katika ofisi za gazeti hili na wengine kupiga simu kwa madai wamedhalilishwa na Kariakoo kuonekana ni eneo wanaokusanyika watu wenye njaa.

Wananchi hao walionesha hisia za kukerwa na kauli hiyo huku wengine wakimtaka Bw Makamba awaombe radhi sambamba na kujiuzulu wadhiufa wake ndani ya chama hicho tawala kwani amewadhalilisha wakazi wa Kariakoo, watu wanaofanya biashara zao sehemu hiyo na eneo hilo kwa ujumla.

Walikwenda mbali zaidi na kudai kuwa mdahalo ni haki ya wapiga kura na kwamba yeyote anayeshiriki awe mwenye njaa au aliyeshiba mawazo yake yanapaswa kuheshimiwa kwani kinachotakiwa kusikilizwa ni majibu ya kutoka pande zinazohojiwa.

Walidai kuwa kauli ya Makamba imejaa kejeli na dharau kubwa dhidi ya watu masikini kwani njaa zao zimechangiwa na wanasiasa hivyo wana haki ya kuwauliza kwa nini sera zao zinawaletea njaa.

“Watu hawalali njaa kwa kupenda, kuna mambo mengi, mengi yanachangiwa na hawa wanasiasa. Sasa kama kuna mtu amelala njaa ana haki kwenda kwenye mdahalo na kuhoji chanzo cha njaa yake. Sasa kama Makamba anatuona tunaokaa Kariakoo au kufanya biashara zetu pale tukiamka na njaa zetu tunakuwa hatuna akili na hatutakiwi kwenda kwenye mdahalo kwa sababu tutauliza kwa nini hatukula, hii ni dharau kwa umma, awajibike, ametudhalilisha watu masikini! Njaa si kigezo cha kuzuiwa kwenda kuhoji watu wanaoomba uongozi………..”

Habari zaidi katika Majira ya leo.
Makamba, hajui alitendalo. Kwa maneno yake anatusaidia kuweka pembeni CCM. Makamba na asonge mbele kuropoa kwake ni mtaji katika kipindi hiki chakuelekea mabadiliko maana anazidi kuaminisha umma kwamba CCM haina mwelekeo na imekosa dira. Kukosa dira kw CCM ni zao laviongozi walio kosa dira.
 
LIKE FATHER LIKE SON..au unaposema January is far better unamaanisha "FAR BETTER IN TALKING CHEAP SHIT than his dad"?

You hit the nail on the head! Hana unafuu ila labda ameanza kutembea nje ya nchi mapema so amekuwa polished kidogo. Ila kama mshauri wa rais huko Ikulu 2005 - 2010 hajaweza kutuonyesha umahiri wake katika chochote zaidi ya kudaka projects za watu kama akina Sugu ya Malaria na wengine ambao wamekuwa waoga kwa sasa kuongea...
 
Makamba anadai apelekewe maswali, hlafu baadae yatafutiwe majibu ndo mdahalo uwepo, Haaa, huyu mzee kazeeka kweli. Nadhani CCM hawana sera
 
huyo ndiye baba january anataka waongee rostam,ahmed shabib,mo dewji,id azan,zungu,abood.kwa nini mungu asitupe idd amin wa tz tukawatimua hawa nyang"au wezi wa mali ya uma na vibaraka wao ndani ya ccm..chagua slaa ndiyo fimbo yao
 
Sidhani kuwa akienda kuzimu atapokelewa, kwani walioko huko wananafuuu kidogo, yeye sasa amemshinda hata shetani ambaye nae anashangaa maneno ya huyu mzee, ila niliskia kuwa alishamtimua ndg yake toka bumbuli aliyekuja kumsalimia hapa jijini hivyo nadhani labda kakosa radhi ya wazee kule kijijini bumbuli.

kwanza aache kutumia vitabu vitakatifu kudhalilisha binadamu wa MUNGU, HIVI kwa nini sisiemu wasipumzike kwanza jamani?

GOD bless Tanzania
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom