Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Ulimi wamponza Yusuf Makamba
wakazi Kariakoo wadai amewadhalilisha
Washinikiza aombe radhi, ajiuzulu
Kauli iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bw Yusuf makamba kuhusu ombi la mdahalo la mgombea ubunge kupitia chama hicho Jimbo la Urambo Mashariki, Bw Samuel Sitta na mgombea urais kupitia Chadema, Dk Wilbrod Slkaa, imezua mtafaruku miongoni mwa wanachama wa chama hicho.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kuwa CCM imenawa mikono na haihusiki na mgogoro baina ya wanasiasa hao huku vikimkariri Bw Makamba akisisitiza kuwa Sitta na Dk Slaa, wana mambo yao wenyewe na wala hayakihusu chama hicho.
Bw Makamba alikaririwa akisema CCM kimekataa midahalo kwa sababu hukusanya watu wa hovyo na hakuna mikakati maalum ya kuiendesha kwa kujieleza na kukosoana kulingana na sera za vyama husika.
Alisema chama hicho hakiogopi midahalo, bali kisingependa kuona kinashiriki kwenye midahalo kwa sababu zinaweza kuibuliwa hoja zisizo na msingi kwa makusudi ya kukichafua.
Tunataka mdahalo uwe wa sera. Sio unakusanya watu wa Kariakoo halafu anajitokeza miongoni mwao ambaye jana alilala njaa halafu anasema jana CCM ilitulaza njaa, alinukuliwa akisema Bw Makamba.
Kitendo cha Bw Makamba kutolea mfano wakazi wa eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam kimezua mtafaruku miongoni mwa wananchi hao na kuwafanya baadhi yao kufika katika ofisi za gazeti hili na wengine kupiga simu kwa madai wamedhalilishwa na Kariakoo kuonekana ni eneo wanaokusanyika watu wenye njaa.
Wananchi hao walionesha hisia za kukerwa na kauli hiyo huku wengine wakimtaka Bw Makamba awaombe radhi sambamba na kujiuzulu wadhiufa wake ndani ya chama hicho tawala kwani amewadhalilisha wakazi wa Kariakoo, watu wanaofanya biashara zao sehemu hiyo na eneo hilo kwa ujumla.
Walikwenda mbali zaidi na kudai kuwa mdahalo ni haki ya wapiga kura na kwamba yeyote anayeshiriki awe mwenye njaa au aliyeshiba mawazo yake yanapaswa kuheshimiwa kwani kinachotakiwa kusikilizwa ni majibu ya kutoka pande zinazohojiwa.
Walidai kuwa kauli ya Makamba imejaa kejeli na dharau kubwa dhidi ya watu masikini kwani njaa zao zimechangiwa na wanasiasa hivyo wana haki ya kuwauliza kwa nini sera zao zinawaletea njaa.
Watu hawalali njaa kwa kupenda, kuna mambo mengi, mengi yanachangiwa na hawa wanasiasa. Sasa kama kuna mtu amelala njaa ana haki kwenda kwenye mdahalo na kuhoji chanzo cha njaa yake. Sasa kama Makamba anatuona tunaokaa Kariakoo au kufanya biashara zetu pale tukiamka na njaa zetu tunakuwa hatuna akili na hatutakiwi kwenda kwenye mdahalo kwa sababu tutauliza kwa nini hatukula, hii ni dharau kwa umma, awajibike, ametudhalilisha watu masikini! Njaa si kigezo cha kuzuiwa kwenda kuhoji watu wanaoomba uongozi ..
Habari zaidi katika Majira ya leo.