Ulikuwepo enzi za DUKA LA KAYA??

Ulikuwepo enzi za DUKA LA KAYA??

Hakuna kitu tangible alichofanya Nyerere zaidi ya kumaliza akiba ya Taifa lenu kwa kujijengea hishma ya kisiasa kuwa yupo mstari wa mbele katika ukombozi wa Afrika na kuuwa uchumi wenu kabisa.

Nchi alipewa ikiwa na akiba kubwa ya fedha, haikuwa na njaa hata kidogo, uchumi wake ulikuwa mzuri, hakukuwa na ulanguzi wala mwendo wa kuruka na kila kitu kilipatikana madukani. Yeye ndie muasisi wa Rushwa na Ulanguzi huko Tgk.


Humtendei haki mwal hata kidogo mkuu.
Kumwita mwal muasisi wa rushwa? Nchi ndio kwanza ilikuwa changa tena huru watu waliokengeuka hawawezi kukosekana mwal hakuwa mungu kuwadhibiti kama dawa ya mbu wakati wa usiku kwamba inaua mara moja kwa mpigo alijaribu na kukemea kila alipopata nafasi ya kufanya hivyo. Sasa ukimsema mwal kuhusu rushwa huyu kikwete utasema nini.kama rushwa ingekuwa marashi bs kikwete ananukia mwili mzima
 
Wee acha tu ndugu yangu enzi hizo!!! Ukimsimulia kijana wa dot com hawezi kuelewa mambo yalikuwaje.

Hawezi kabisa ataishia kumwaga matusi.na enzi hizo sungusungu kila kona ukikatiza tu mitaa ya watu usiku saa zisizoruhusiwa unakamatwa haya jina lako kazi yako kitambulisho.nakumbuka baba yangu na wenzake ikifika zamu yao ya kulinda mtaa alikuwa anafurahi haswa siku ambazo na mama zilikuwa zimegoma kidogo.
 
Swali lako hapa ni rahisi sana; lakini labda uliulize kivingine... unakumbuka ni Watanzania wangapi walikufa kwa baa la njaa wakati wa duka la kaya? Kule mtaani kwenu au kijijini unakumbuka kuwaona watu wanatembea mbavu nje kwa njaa; au hata kama unakumbuka watu waliokuwa wanakula mizizi yenye sumu ili kupata angalau chochote mdomoni...?? Labda kama kuna mtu mwingine anaweza kutusaidia katika haya...

Unachoita "uzembe" wengine tunakiona "the genius of Mwalimu". Hivi unajua leo hii kuna Watanzania wanatatizo la njaa na hii imekuwa ni kila mwaka licha ya kwamba hakuna tena "duka la kaya"?

Ukisoma wote "wanaokumbuka" kwenda kupanga foleni, kupewa mgao wao utaona kuwa hakuna hata mmoja ambaye anasimama na kusema kuwa kwenye familia yao kuna mtu alikufa kwa njaa...!!

Think about it.. je bila ya duka la kaya tungekuwaje?

Uko sahihi Mzee Mwanakijiji uamuzi wa Mwalimu kwa wakati huo ulikuwa sahihi, lingeruhusiwa soko huria watu wengi wangekufa kwa njaa.
 
Humtendei haki mwal hata kidogo mkuu.
Kumwita mwal muasisi wa rushwa? Nchi ndio kwanza ilikuwa changa tena huru watu waliokengeuka hawawezi kukosekana mwal hakuwa mungu kuwadhibiti kama dawa ya mbu wakati wa usiku kwamba inaua mara moja kwa mpigo alijaribu na kukemea kila alipopata nafasi ya kufanya hivyo. Sasa ukimsema mwal kuhusu rushws huyu kikwete utasema vl.kama rushwa ingekuwa marashi bs kikwete ansnukia mwili mzima

Ukifuatilia watu wenye chuki na Mwalimu utagundua kuwa hawamchukii kwasababu Uongozi wake ulikuwa mbaya, bali wanasukumwa na milengo ya Kidini na ndiyo maana wengi wao ni wa Imani moja. Tukubali tusikubali Mwalimu alifanya mengi mazuri.
 
Mimi nilijua kaya bangi,kumbe unamuelezea nyenyere na sera zake za kuiga.nyenyere alikuwa mlala hoi aliyesindwa kusomesha watoto darasani,na ndo maana alikufa kwa kifo cha aibu (mkanda wa jeshi),inasemekana alikuwa nakimada wa nje pale masaki ndie aliyempa lile goma.namchukuia nyenyere kuliko ukoma.
 
Mimi nilijua kaya bangi,kumbe unamuelezea nyenyere na sera zake za kuiga.nyenyere alikuwa mlala hoi aliyesindwa kusomesha watoto darasani,na ndo maana alikufa kwa kifo cha aibu (mkanda wa jeshi),inasemekana alikuwa nakimada wa nje pale masaki ndie aliyempa lile goma.namchukuia nyenyere kuliko ukoma.

Acha uongo, nyerere hajafa kifo cha aibu,
unajua utakufaje mkuu? Aibu unaijua?Acha kejeli zako, nyerere alikuwa jembe! kafa kishujaa kama alivyokufa mandela!
 
Aisee
Nyinyi wakulungwa wa zamani mlikuwa mmenyeshwa maji ya bendera enzi kuwa chipukizi wa ccm mashuleni
Yaani na mateso yote nyerere aliyoyaleta ya wazazi wetu kuvaa viraka na kunya chai ya sukari guru, naona wote bado mmeonyesha mapenzi ya dhati,
Kweli mlikuwa vilaza.....
 
Back
Top Bottom