Ulianzaje kukaa gheto?

Mimi kwenda kukaa gheto haki nilifosi,yaani wazazi walikua wabishi kukubali woiii ikabidi niingie gharama ya kutafuta chuo niongezee elimu,nikaondoka home kwa kigezo cha kwenda kujisomea nikaenda kupanga ilala mchikichin karibu na kiwanda cha bia lol.Aisee kile kiwanda cha bia kilinifanya niwe nalewa kila mara maana ule upepo wa pombe ukivuma nahisi mawenge.Tokea hapo ndo ukawa mwanzo wa kujitegemea.
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
 
Aisee hatari,soon baada ya kumaliza chuo way back 2014 nikarudi home nikajaribu mishe za maskani ikawa chenga na maneno mengi ya maudhi,nikauza pc nikazama Dar kuna mwana akanipokea

baada ya mwezi wa kutafuta ramani mshikaji kaniunganisha kazi alipokuwa anafanyia salary 270,000 per month nikapiga kaz by septemba 2015 kibarua kikaota nyasi kampuni ilifilisika mfukoni nina 1,200,000 jamaa akasema saiz kila mtu aangalie namna ya kujisaidia

Nikapiga akili mambo magumu had pesa ikakata hiyo ni may mwaka uliofuata,nikarudisha mpira kwa kipa tena kwa nauli ya kusaidiwa na mdau tuliyefahamiana tuu.Maskani michosho mingi kuna siku nikagoma kufanya ishu fulani fulani wakanitimua nikapanda gari hadi swax,alikuwepo mwana fulani home nilitoka na 60,000 baada ya kulipa nauli nikabakiwa na 40,000 hapo hakuna anayejua nikikokwenda.
Nikamkuta mwana akanipokea nikamwambia nimekuja kusaka life kazi yoyote ntafanya.jamaa akasema utakula ila pia kulala tafuta geto,ndo ikawa mara ya kwanza nimeanza kupanga hiyo ni june 2016 hapo godoro ni mabox mimi na ndoo moja tu ndo kiti hicho.

Asubuhi nawahi kwenda kwenye vibarua jioni nakula kwa mshikaji nachagua nikipata.Baridi yote iliniishia maana nilikuwa na shuka tu na sakafu ya baridi,mwezi wa kumi baada ya kudunduliza nikanunua godoro na vyombo vichache vya kuanzia maisha.Ilifika kipindi hali ikawa ngumu sana sometime hakuna kazi unashindia miwa na bumunda tuu huku unawaza kodi na bili za maji na umeme,kodi ilikuwa 12,000 umeme 1000 na maji 2000 jumla 15,000 lakini inasumbua.

Piga sana kazi za zege na saidia fundi kutwa 5000 ila ndo hivyo lazima maisha yaende

By Novemba 2016 Mungu saidia kuna mwana akanifanyia connection ya kazi za ukandarasi ambazo ndio fani yangu from there hadi leo hii ndio nilipata nafuu ya maisha japo ni kazi za muda zinaishia zinakuja tena so wanaofanya kazi kwa wakandarasi wanaelewa.

Pamoja na kwamba sijatoboa niko kwenye nafuu maana nina familia na nina boma siku yoyote ntahamia kwangu

Ila kitu sitosahau nilipata tabu sana na ishu iliyonisikitisha nilipata demu nikamketa geto baada ya kuona jinsi lilivyochoka hakutaka kukaa na kuanzia hapo akaniblock.Wakati fulani pia nikiwa kwenye ukidampa kuna demu alinielewa but wenzie walimponda eti ntampa pesa gani wakati nashindia ukidampa nae akasepa nikaacha kabisa kutokea mademu
 
Wakuu mambo vipi,,Leo naomba tufanye kushare kila mtu jinsi alivyo chomoka Nyumbani kwao..Hii itatoa hamasa kwa wale waliokua nyumbani na kuogopa kuhama na kuanza kujitegemea.

Janga hili linawakumba wana vyuo wengi,unakuta mtu anamalza chuo akiwa labda ana 25 then anarud nyumbani ,mbaya zaid anasubir kazi..alaf kazi zenyew haijulkani utapata lini.

Hii inapelekea wana wengi kua na fear ya kuchomoka home...Kiukwel hali ya kukaa hom inakata sana..Mzee unakuta anachomoka anakuachia mikazi flani hivi howcome.

Ukija upande wa MMU ndio mambo yanakua sio mambo...mtoto anataka aje kukusalmia unaona soo kwasababu upo nyumbani..inakata sana hii

Tukija kwenye maisha ya kujituma tu..sometime unakosa hamasa ya kupambana kwasababu ugali wa bure,unalala bure,kila kitu bure..hii inakua ngumu kuwaza kwa mapana ili kuanza kukamilisha dream zako..

Pia inakata sana..pale wanao unakuta wapo na mageto yao..lakin wewe kwako ni tofauti.

Sasa naomba kila mmoja aseme alichomokaje home na kuanza kukomaa na maisha..Achilia changamoto zake kikubwa hapa ni kusepa kwa maza..

##Mimi binafsi geto nilianza kukaa soon nilivyoingia chuo,,,nakumbuka nilipata room ya elf 50 nikaanza nayo kibish,nikanunua bed ya 150, 5 kwa 6,nikatafuta feni tu ya elf 35..si unajua joto la dar..nikaingia k.koo nikavuta subwoofer ya elf 75 tu...geto bila mziki sio geto ni choo,kujichek mfukoni boom likawa lishakata...basi nikaendelea kuishi geto hadi namalza chuo geto likawa limesheheni tu...
sasa baada ya kumalza chuo. Ndio nikarudi hom..ujinga niliofanya ni kurud hom na baadhi ya vitu niliviuza...Kasheshe ndio ipo saiz..wakuu hom akili inalala,,vibe yote hakuna ,hapa ndio najichanga nichomoke tena nirud geto nianze kupambana..hop ndan ya huu mwaka nitakua nishasepa hom kwa mara nyingine.

Sasa share kitu basi nawewe..

#Nini lilikusukuma usepe home?
#Kitu gani kilikupa mzuka wa kuanza kukaa geto?
#Vipi ulianza kukaa geto ukiwa na kazi au kibishi tu?
#Maisha yalkuaje since day one?
#Je ulienjoy uamuzi wako wa kusepa home?
#ulianza kununa vitu gani vya msingi na kuanza kuishi geto
#Una lipi la kuwaambia wana walioko home hadi leo wakiogopa kukaa geto kisa hawana ajira bado?

Karibuni wakuu..

View attachment 878774
mi Niko mbioni...kukaaa ghetooo kikubwa uzima
 
Aisee hatari,soon baada ya kumaliza chuo way back 2014 nikarudi home nikajaribu mishe za maskani ikawa chenga na maneno mengi ya maudhi,nikauza pc nikazama Dar kuna mwana akanipokea ,baada ya mwezi wa kutafuta ramani mshikaji kaniunganisha kazi alipokuwa anafanyia salary 270,000 per month nikapiga kaz by septemba 2015 kibarua kikaota nyasi kampuni ilifilisika mfukoni nina 1,200,000 jamaa akasema saiz kila mtu aangalie namna ya kujisaidia
Nikapiga akili mambo magumu had pesa ikakata hiyo ni may mwaka uliofuata,nikarudisha mpira kwa kipa tena kwa nauli ya kusaidiwa na mdau tuliyefahamiana tuu.Maskani michosho mingi kuna siku nikagoma kufanya ishu fulani fulani wakanitimua nikapanda gari hadi swax,alikuwepo mwana fulani home nilitoka na 60,000 baada ya kulipa nauli nikabakiwa na 40,000 hapo hakuna anayejua nikikokwenda.
Nikamkuta mwana akanipokea nikamwambia nimekuja kusaka life kazi yoyote ntafanya.jamaa akasema utakula ila pia kulala tafuta geto,ndo ikawa mara ya kwanza nimeanza kupanga hiyo ni june 2016 hapo godoro ni mabox mimi na ndoo moja tu ndo kiti hicho.Asubuhi nawahi kwenda kwenye vibarua jioni nakula kwa mshikaji nachagua nikipata.Baridi yote iliniishia maana nilikuwa na shuka tu na sakafu ya baridi,mwezi wa kumi baada ya kudunduliza nikanunua godoro na vyombo vichache vya kuanzia maisha.Ilifika kipindi hali ikawa ngumu sana sometime hakuna kazi unashindia miwa na bumunda tuu huku unawaza kodi na bili za maji na umeme,kodi ilikuwa 12,000 umeme 1000 na maji 2000 jumla 15,000 lakini inasumbua.Piga sana kazi za zege na saidia fundi kutwa 5000 ila ndo hivyo lazima maisha yaende
By Novemba 2016 Mungu saidia kuna mwana akanifanyia connection ya kazi za ukandarasi ambazo ndio fani yangu from there hadi leo hii ndio nilipata nafuu ya maisha japo ni kazi za muda zinaishia zinakuja tena so wanaofanya kazi kwa wakandarasi wanaelewa.Pamoja na kwamba sijatoboa niko kwenye nafuu maana nina familia na nina boma siku yoyote ntahamia kwangu
Ila kitu sitosahau nilipata tabu sana na ishu iliyonisikitisha nilipata demu nikamketa geto baada ya kuona jinsi lilivyochoka hakutaka kukaa na kuanzia hapo akaniblock.Wakati fulani pia nikiwa kwenye ukidampa kuna demu alinielewa but wenzie walimponda eti ntampa pesa gani wakati nashindia ukidampa nae akasepa nikaacha kabisa kutokea mademu,,
Hahah dah hawa viumbe hawataki Shida..pole sana mkuu na hongera sana kwa struggle..kutoka hom inatakiwa uwe mbish kwel ,ila ndio njia ya kujitegemea
 
WANAGETTO NISAIDIENI NIPATE CHUMBA MAENEO HAYA MAANA MADALALI WANATUKAMUA SANA
-Anayejua chumba maeneo ya Mabibo hostel,sinza,changanyikeni,survey,makongo juu,ubungo external,mwenge na riverside....
Budget yangu ni cha 40k au 50k kwa mwezi...
Tusaidiana na wanaotafuta vyumba maeneo hayo pia...

Nipm nipigie au nitext kwa namba 0759432654
 
Siku ya kwanza kuhamia kwangu, nakumbuka nililala chini kwenye tiles, nilikuwa nimeshafanya usafi nikasogea kula bata maeneo ya sinza mpaka saa 8 usiku, nikiwa nnarudi home kwa wazee nikajisemea ngoja nikakague tena kwangu, hapo hamna kitu nikafika nikaangusha sitting room, kuanzia hiyo siku sikuwahi kulala tena home

Kesho yake asubuhi nikazama game nikanunua sofa bed kwa 395,000/= nakumbuka nilikuwa nnalitamani sana afu likawa kwenye ofa nikajilipua, sahani, frying pan, sufuria na glass, nikarudi huome nikang’oa TV yangu, music system + king’amuzi na ki fridge kidogo nilikuwa nnatumia chuo nikabeba na kimeza cha kishkaji cha kuwekea Tv nikamuaga mzee mimi ninasepa nahamia sinza, akasema poa nikapita mwenge nikachukua jiko la gas + mtungi

Hii siku ya pili nikaanza na asset zangu zilikuwa ni sofa bed, kimeza cha kuzushi cha tv, tv, music, jiko la gas, mtungi na vyombo vya jikoni...

Kwa miezi miwili mfululizo nilikuwa nnalala sitting room
 
Back
Top Bottom