Ni kumbukumbu ipi unaikumbuka siku ulivyoondoka kwenu na kilichokufanya uondoke kwenda kuanza maisha ya kujitegemea?

NetMaster

JF-Expert Member
Sep 12, 2022
1,454
4,853
Hakika ilikuwa ni siku ambayo binafsi niliumia, ni baada ya kushindwa kuendelea na elimu yangu nilipomaliza form 4 mwaka 2012..

pale home nilionekana nipo nipo tu, ikabidi nitafte mishe ya kujifunza useremala lengo likiwa nikianza kupata pesa nihame, haikuwa kama nilivyotegemea maana hata nilipopata sehemu ya kujifunzia mtaani na kumsaidia fundi nilikuwa sipati chochote zaidi ya chakula tu kwa fundi, hata nauli nilikuwa sina nakanyaga kwenda na kurudi, yani nikifika nyumbani nlikuwa sina amani maana sirudi na chochote.

Hii ilinifanya niongeze juhudi zaidi kujifunza kwa spidi, ndipo baada ya miezi kama 10 hivi nikaanza kupata vihela.

Sikulaza damu nikaondoka pale nyumbani fasta sana kwenda kupanga geto la elf 10 hapo nikiwa miaka 18 ukingoni.

Nakumbuka ndio siku ambayo nilimuona mama yangu analia iliniuma sana kwakweli, mzee nae akawa ananibembeleza nikae kae hapo home ila nilishakata shauri nikasepa.

Maisha ya mtaani yalikuwa tofauti sana, ila yalinifanya nipige kazi zaidi angalau nikaanza kupanga nje ya uswahilini

Anyway nilichojifunza hadi sasa hata upangishe nyumba hakuna uhuru, ilinibidi ninunue kiwanja na kwa sasa mdogo mdogo na mimi najenga kwangu japo ni kanyumba ka kawaida nitapata amani kuwa na kanyumba kangu.
 
ilikua mwaka mmoja baada ya kumaliza kidato cha nne. Nakumbuka siku hiyo nimeingia chooni kuoga sasa kabla ya mimi kuingia choon kuna mwana alitoka kunyoa mavyuzi

basi m nikamaliza haja zangu nikatoka time natoka nakutana na sista angu kanizid kama miaka miwil au mitatu hiv

basi sista kutoka choon akaaja na mada "MKINYOA MSAFISHE NYWELE ZENU" aloo siku nzima sikua na aman kuna mwanangu mmoja alikua anapiga mishe town basi nikamuomba niwe naenda nae kushinda town

jama akakubali baada ya miez miwili nikamuaga bimkubwa nasepa home akawa anacheka tu akasema we nenda nakupa mwezi utarud adi leo hii naandika huu Uzi sjarudi nyumbani

SHUKRANI kwa sista bira yeye adi muda huu ningekua home nazani
 
ilikua mwaka mmoja baada ya kumaliza kidato cha nne. Nakumbuka siku hiyo nimeingia chooni kuoga sasa kabla ya mimi kuingia choon kuna mwana alitoka kunyoa mavyuzi...
kilaa mtu anamnaa yake yakuondoka hom,na kuna wengine mpk leo hawajaondokaa makwao na hawana mpngo huooo...nyumba alijenga Babu mpk wajukuu wataitumiaa...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi bado nipo wadau Ila nasoma chuo Nina 20 years mnanishauri nn asee namalizia nikiwa na 22 years
Tafuta skill au biashara mapema ambayo unaweza kuanza kuifanya ukimaliza tu chuo.. unaifanya hio mishe hata ukondoka home unaweza kujitafutia pesa kusurvive huku unaendelea kutafuta ajira ya taaluma uliyosomea,

Mishe za fasta fasta hizi hapa

Unaweza kujifunza kunyoa hukosi pesa ya kujitunza

unaweza kufanya biashara ya kukaanga chipsi na kyepe yai, wateja kibao ila upige mzigo aisee.
 
Nilipomaliza chuo sikurudi home, nilichofanya nilihama nilipokua mwanzo na kuhamia eneo lingine penye nafasi, sikupenda kukaa home kubanwa banwa na masharti kibao.

Nilipowaambia sirudi, wazazi walisononeka ila wakanipa baraka zao na kunambia life likibana pale ndio home na room yangu ipo wameifunga tu.

Mwaka wa sita huu nakomaa na soon nahamia kwenye nyumba yangu niepukane na kodi na niwe huru zaidi.
 
Back
Top Bottom