toplemon
JF-Expert Member
- Mar 26, 2017
- 4,581
- 4,628
Hongera sana mkuuSiku ya kwanza kuhamia kwangu, nakumbuka nililala chini kwenye tiles, nilikuwa nimeshafanya usafi nikasogea kula bata maeneo ya sinza mpaka saa 8 usiku, nikiwa nnarudi home kwa wazee nikajisemea ngoja nikakague tena kwangu, hapo hamna kitu nikafika nikaangusha sitting room, kuanzia hiyo siku sikuwahi kulala tena home
Kesho yake asubuhi nikazama game nikanunua sofa bed kwa 395,000/= nakumbuka nilikuwa nnalitamani sana afu likawa kwenye ofa nikajilipua, sahani, frying pan, sufuria na glass, nikarudi huome nikang’oa TV yangu, music system + king’amuzi na ki fridge kidogo nilikuwa nnatumia chuo nikabeba na kimeza cha kishkaji cha kuwekea Tv nikamuaga mzee mimi ninasepa nahamia sinza, akasema poa nikapita mwenge nikachukua jiko la gas + mtungi
Hii siku ya pili nikaanza na asset zangu zilikuwa ni sofa bed, kimeza cha kuzushi cha tv, tv, music, jiko la gas, mtungi na vyombo vya jikoni...
Kwa miezi miwili mfululizo nilikuwa nnalala sitting room