Mazungumzo ya Tapeli Na Mwalimu aliyetaka kuhama kituo Cha kazi.
Tapeli:Hallo,wewe ni Mwalimu Fulani bin Fulani Na unataka kuhama
Mwalimu:Ndiyo nina uhitaji sana wa kuhama huku niliko.
Tapeli:Mimi nipo Tamisemi kuna mtu hapa nipo naye Ana uwezo wa kukusaidia tatizo lako ndani ya muda mfupi
Mwalimu:Nitashukuru sana kama nitafanikiwa.
Tapeli:Ila huyu mheshimiwa anahitaji ya maji kidogo ili aweze kufanya zoezi lako la kukuhamisha.
Mwalimu:Anataka kiasi Gani Na lini?
Tapeli:Anataka kiasi Fulani (Ziatajwa laki kadhaa) Fanya haraka Sasa hivi maana nafasi ni chache Na wahitaji ni wengi.
Mwalimu:Kwa Sasa hivi kupata hela ni ngumu maana hela ipo benki Na muda huu hakuna magari Na kwa bodaboda nauli haitoshi.
Tapeli:Mchukue bodaboda uende naye mjini utamlipa ukifika benki.Ufanye hima Mwalimu
Mwalimu: Oooh umenipa wazo zuri nachukua bodaboda nitamlipa nikifika mjini.(Mwalimu anampanga bodaboda kuwa aseme hawezi mpeleke town Bila kuweka advance ya shilingi elfu kumi,nyingine atamalizia akifika town)
Tapeli:Fanya haraka ukichelewa ofisi zitafungwa Na utakuwa umekosa nafasi
Mwalimu:Nimeongea Na bodaboda amekataa kunipeleka Bila kuweka advance hela ya mafuta labda uongee naye wewe umshawishi anipeleke.
Tapeli anaongea Na bodaboda,bodaboda anagoma kumpeleka mwalimu,Bodaboda anamshauri Tapeli amkopeshe mwalimu hela halafu ye ndo atalipwa Na Mwalimu.Tapeli anaingia kingi anatuma elfu kumi kwa bodaboda.Bodaboda Na Mwalimu wanatoa fasta ile elfu kumi halafu Mwalimu anapiga simu kwa Tapeli.
Mwalimu:Ndugu yangu umeniokoa,nimeshaanza safari ya mjini.
Masaa kadhaa yanapita.
Tapeli:Vipi mmeshafika mbona kimya.
Mwalimu:Mkuu sio kila siku unatapeli tu watu nawe siku moja Moja ukitapeliwa siyo vibaya.
Tapeli🙁Anatukana matusi yote Na anagundua kuwa naye kaliwa)