Ule utapeli wa kijuha umeanza tena...

Ule utapeli wa kijuha umeanza tena...

Habali ya leo.mimi MICAEL KUYUNGA.samahani kuna boc wangu yupo serengeti mbuga ya wanyama poli yupo na wageni wake ni wazungu.watalii.wanataka kununua vitu vya kitamaduni kama vinyago vya kuchonga na mti wa mpingo,mabatiki,mashuka ya kimasai na vitu vingine vingi.kaniomba nimtafutie mtu naemjuwa na mwaminifu amsaidie kwenye manunuzi ya hivyo vitu.kama uko tayali nimpatie namba zako akupe maelekezo zaid.mimi naumwa matonses na kifua nimebanwa sauti imenikauka.uwe unanitumia sms kwa mawasiliano zaidi.

Namba iliyotumika ni 0621 375081
Nishawahi kupata sms kama hiyo miezi kadhaa nyuma ikabidi nimuhoji vizuri nijue ni Nani maana ni kweli Kuna jamaa yangu ana kituo cha kitamaduni ila namba si zake.
Nilipoona kimya na mi nikapotezea kiaina ila si kujua kabisa kama ni Yale ya Tuma hela kwa namba hii hadi juzi dogo alipo tumia sms hiyo hiyo Ndio nikastuka
 
Huwa zinaanza na country code +255 lakini namba zinazofuata si kama namba za wateja wa mtandao husika. Huwa zinakuwa ni tofauti. Mfano ya Vodacom inaanza na +255(country code) halafu zinakuja namba zao ambayo inakuwa +255 901 767 676.

Sasa kibongo bongo hatuna namba inayoanza na 901 baada ya country code zinazotumiwa na wateja wa huduma wa mitandao ya simu. Ukipigiwa simu halafu ukiambiwa kutoka huduma kwa wateja halafu namba yake ipo kama namba wanazotumia wateja huyo ni tapeli.
Hapana. Namba wanayotumia ni ya kawaida, huo mfano ulionipa ni namba ya huduma ambayo huwa inapigwa kutoka kwenye system na hata ikikupigia hutaongea na mtu live ila utasikiliza tu maelezo na kufanya kile unachoelekezwa, lakini namba ambayo wahudumu wanatumia kuwapigia wateja ni ya kawaida, kwa mfano Vodacom wanatumia +255754100100
 
Ha ha ha njaa mbaya sana yule jamaa ambae anasambaza picha za nyuki wakiwa wamejaa kwa MTU au kifaa kilichoibiwa anajiita mzee wa nyuki kumbe nae tapeli tu
Ni hivi juzi kati aliibiwa dogo laptop yake sasa katika pitapita face book na wasap kakuta hizo picha akajaa kumbe mzee wa nyuki kamwambia atume salio na majina matatu dogo salio kakwama ikabidi anistue nikamwambia huyo atakuibia akagoma nikamwambia amwambie huyo mganga amfanyie kwanza akipata kifaa chake ndio tumlipe tukiingia mitini hizo nyuki atume kwetu,,
Mzee nyuki kuambiwa hivo matusi kama yote eti nyuki wangu nawatoa kwa gharama basi toeni hata hela ya kiti basi.
Dogo kapiga kimya kama siku mbili cha ajabu mzee nyuki ye ndio anapiga simu kila Mara kuulizia hela inatumwa au vp, nikamwambia dogo unaona yaan aliyeibiwa amepozi lkn mganga anakomaa kupiga simu kama mpiga debe akitafuta abiria.
 
Tulitapeliana na huyu binti km binti mpk tkt katuma nikaenda Moscow kula bata,nikajirudia zangu kimyaa mtaani nikakata line,mirska mtoto alikua mtamu balaa Skype kwa kwenda mbele.
Mi nikajua tu katumwa huyu,nikamlamba tkt piga fix kuna project ya pesa mingi nikifika Ferrari nini nafix.
Aah nikapata free safari.
Matusi badae nikayakoga potelea karibu.
Hujasomeka
 
Hapana. Namba wanayotumia ni ya kawaida, huo mfano ulionipa ni namba ya huduma ambayo huwa inapigwa kutoka kwenye system na hata ikikupigia hutaongea na mtu live ila utasikiliza tu maelezo na kufanya kile unachoelekezwa, lakini namba ambayo wahudumu wanatumia kuwapigia wateja ni ya kawaida, kwa mfano Vodacom wanatumia +255754100100
Pengine! Na si unajua haya mambo huwa yanakuja kutokana na experience mtu aliyokumbana nayo. Asante kwa kuniongezea maarifa.
 
Hio safi sana mzee fanya kama unamsokota sokota wkt huo lamborghini inaunguruma unguruma na udwanzi kwa sana bila papara huku na kule tindika linakwangaruka na unaithibitisha kwa M-pesa ili wazee waki approach madesa yanakua kwa Lumbert au popote kambi.
We umenielewa,kuna jamaa huko anatafuta dictionary.
 

Rafiki yangu aliibiwa simu akiwa anasafiri, mara nikatumiwa ujumbe kuwa simu yake imeharibika na anasafiri ila amepatwa na shida kidogo hivyo nimtumie laki moja na namba ikatumwa ya kutumia hela. Nikampigia akakata na kutuma ujumbe kuwa simu mbovu hatutoelewana.

Nikiwa njiani kuelekea kwa wakala nafsi ikasita, nikampigia mama yake bahati nzuri nae(rafiki) ndio alikuwa amefika, kumueleza akastuka kweli, ikabidi aanze mchakato wa kuwajulisha alioweza kuwa ameibiwa simu. Ila kuna mjomba wake alikwishatuma pesa.
Mie dogo alisafiri kwenda Dodoma akaibiwa simu.Waliomuibia Simu wakaanza kuitumia simu yake kusambaza meseji kama hizo.Nikajifanya nimeingia king,nikasema nauliza maswali ya kuconfirm wewe Nani akataja jina la Dogo,upo wapi akataja Dodoma.We unatokea Kijiji Gani,na last born kwenu anaitwa Nani,na maswali kama hayo jamaaa akapotea
 
Mimi aliniambia anatoka kampuni ya voda! Kuna pesa imetumwa kimakosa hivyo niirudishe. Halafu walivyokuwa hawatumii akili, code namba zao si za huduma za wateja bali ni za wateja. Alivyoona nimemshutukia ananiambia subiri sasa tukufungie line yako halafu akakata simu.
Wajinga Sana,ila kuna watu wanawakamata.
 
Mazungumzo ya Tapeli Na Mwalimu aliyetaka kuhama kituo Cha kazi.

Tapeli:Hallo,wewe ni Mwalimu Fulani bin Fulani Na unataka kuhama

Mwalimu:Ndiyo nina uhitaji sana wa kuhama huku niliko.

Tapeli:Mimi nipo Tamisemi kuna mtu hapa nipo naye Ana uwezo wa kukusaidia tatizo lako ndani ya muda mfupi

Mwalimu:Nitashukuru sana kama nitafanikiwa.

Tapeli:Ila huyu mheshimiwa anahitaji ya maji kidogo ili aweze kufanya zoezi lako la kukuhamisha.

Mwalimu:Anataka kiasi Gani Na lini?

Tapeli:Anataka kiasi Fulani (Ziatajwa laki kadhaa) Fanya haraka Sasa hivi maana nafasi ni chache Na wahitaji ni wengi.

Mwalimu:Kwa Sasa hivi kupata hela ni ngumu maana hela ipo benki Na muda huu hakuna magari Na kwa bodaboda nauli haitoshi.

Tapeli:Mchukue bodaboda uende naye mjini utamlipa ukifika benki.Ufanye hima Mwalimu

Mwalimu: Oooh umenipa wazo zuri nachukua bodaboda nitamlipa nikifika mjini.(Mwalimu anampanga bodaboda kuwa aseme hawezi mpeleke town Bila kuweka advance ya shilingi elfu kumi,nyingine atamalizia akifika town)

Tapeli:Fanya haraka ukichelewa ofisi zitafungwa Na utakuwa umekosa nafasi

Mwalimu:Nimeongea Na bodaboda amekataa kunipeleka Bila kuweka advance hela ya mafuta labda uongee naye wewe umshawishi anipeleke.

Tapeli anaongea Na bodaboda,bodaboda anagoma kumpeleka mwalimu,Bodaboda anamshauri Tapeli amkopeshe mwalimu hela halafu ye ndo atalipwa Na Mwalimu.Tapeli anaingia kingi anatuma elfu kumi kwa bodaboda.Bodaboda Na Mwalimu wanatoa fasta ile elfu kumi halafu Mwalimu anapiga simu kwa Tapeli.

Mwalimu:Ndugu yangu umeniokoa,nimeshaanza safari ya mjini.

Masaa kadhaa yanapita.

Tapeli:Vipi mmeshafika mbona kimya.

Mwalimu:Mkuu sio kila siku unatapeli tu watu nawe siku moja Moja ukitapeliwa siyo vibaya.

Tapeli🙁Anatukana matusi yote Na anagundua kuwa naye kaliwa)
 
Habali ya leo.mimi MICAEL KUYUNGA.samahani kuna boc wangu yupo serengeti mbuga ya wanyama poli yupo na wageni wake ni wazungu.watalii.wanataka kununua vitu vya kitamaduni kama vinyago vya kuchonga na mti wa mpingo,mabatiki,mashuka ya kimasai na vitu vingine vingi.kaniomba nimtafutie mtu naemjuwa na mwaminifu amsaidie kwenye manunuzi ya hivyo vitu.kama uko tayali nimpatie namba zako akupe maelekezo zaid.mimi naumwa matonses na kifua nimebanwa sauti imenikauka.uwe unanitumia sms kwa mawasiliano zaidi.

Namba iliyotumika ni 0621 375081
Huu ni utapeli wa msimu si zamani .Biashara ya utalii imeshika huu msimu
 
Zamani sana.nilisha wai kupigiwa cm na watu wa dizaini hiyo..but mwisho wa picha nikawataperi wao.baada ya kujua nimewaingiza king walinituka sana hahaha.
 
Habali ya leo.mimi MICAEL KUYUNGA.samahani kuna boc wangu yupo serengeti mbuga ya wanyama poli yupo na wageni wake ni wazungu.watalii.wanataka kununua vitu vya kitamaduni kama vinyago vya kuchonga na mti wa mpingo,mabatiki,mashuka ya kimasai na vitu vingine vingi.kaniomba nimtafutie mtu naemjuwa na mwaminifu amsaidie kwenye manunuzi ya hivyo vitu.kama uko tayali nimpatie namba zako akupe maelekezo zaid.mimi naumwa matonses na kifua nimebanwa sauti imenikauka.uwe unanitumia sms kwa mawasiliano zaidi.

Namba iliyotumika ni 0621 375081
Wakikupigia simu kuwa mpole wachore tu 😁😁😁😂😂😂🤣🤣🤣🏃‍♂🏃‍♂🏃‍♂🚬🚬🚬
 

Attachments

Back
Top Bottom