mbu wa dengue
JF-Expert Member
- Jun 2, 2014
- 9,909
- 13,288
Ni kweli aisee,mara nyingi wanacheza na akili za watu wenye tamaa ya kupiga pesa kwa haraka.Nafikiri ukishatapeliwa ndio unakuwa umekabidhiwa rasmi advance diploma ya ujinga.
Na ukienda polisi kushtaki automatically unakuwa umepata degree ya ujinga. ....maana kule unakuwa kituko zaidi cha karne, ... hasa wanapoanza kuuliza km huwa unasoma meseji za polisi? .....in case umepigwa kwa style ya (TUMA HELA KWA NAMBA HII.)
Huu utapeli wa meseji km aliyoletewa Mshana, ni random search ya watu wenye tamaa za kijinga (a deal is always too good to be true.)
Huwezi kutapeliwa km wewe si mjinga , na huna tamaa.
Kwa hyo mtu anaposikia kwamba hyo dili wanahusika na wazungu Basi picha inayomjia ni pesa nje nje.
Na kingine ni kwamba siku zote wajinga hawaishi,mbinu hizo hizo za kizamani Kuna watu wanapigwa.


