Ule upendo wa kweli bado upo?

Ule upendo wa kweli bado upo?

Naulizia ule upendo unaopenda toka moyoni Kwa Nia ya dhati.
Ule upendo ambao hauangalii una Nini au we ni nani au ukoje,unaakuangalia moyo wako.

Unaowaunganisha watu Kwa mioyo Yao na sio walivyo navyo.
Ule upendo ambao hata ukiporomoka Hadi 0 mwenzio bado anakwambia nipo nawe.tutatafuta tutapata na Maisha yataendelea.

Ule upendo hata ukiwa hoi unaumwa mfano umepata ajali bado mwenzio yupo pembeni yako,anakwambia utakuwa sawa na Maisha yataendelea.

Ule upendo unaojali bila ubinafsi.
Ukipatwa na aibu yuko mstari wa mbele kukusitiri
Unapojikwaa ndie wa kwanza kukuinua

Unaoheshimu viapo na ahadi.
Bado upo?
Maana siku hizi ndoa zinavunjika kirahisi sana.

Ukikosa kazi tu mwenzio huyo anaondoka. Akiona unachelewa kuzaa kashatafuta mimba nje
Ukipata ajali au ugonjwa ukakuacha mlemavu msahau!
Wanandoa wanakimbiana.watoto wanatelekezwa.

Mtu anaamua kuwa nawe sababu unaweza kumpa hiki ama kile lakini sio Kwamba anakupenda wewe kama wewe.

Wengine huenda Hadi madhabahuni kula kiapo ila after few months anaondoka.
Ama mwingine anaingia sababu unaweza mpa ndoa lakini hakupendi,unaletewa mimba sio zako,anafanyana na anaowapenda na kukuletea wewe damu sio zako.

Anazaa watoto nje Kwa anaowapenda lakini hawana vigezo vya kuwa wake,yuko nawe sababu unafit na uko tayari kuwa mke.

Upendo genuine kabisa ule upo?
Sr. Abigail; Sahau hiko kitu kabisa. Upendo ule almaarufu kama Upendo wa Agape haupo tena kabisa-sio kwa wanandoa tu bali hata kwa watu wa kawaida ambao hata hawajafungwa kwa viapo; pia hata kwa viongozi walioapa madhabahuni e.g. mapadre /watawa/wachungaji n.k. au mbele ya kadamnasi e.g. viongozi wa Kiserikali e.g. Wanajeshi n.k. au Siasa -Wabunge n.k. Woote hao kwa Ukweli halisi huwa wanaangalia maslahi binafsi zaidi. Mambo yakibuma au kuwa tofauti na matarajio yao huondoka au Hukengeuka.
 
Sio adimu kiukweli upendo una gharama zake!!! je uko tayari???
1 kuvumilia
2 kuheshimu
3 ukweli tupu
4 tutokusalitiana
5 kuwa muelewa kwa chochote kile
6 kuheshimu maamuzi na faragha ya mwenza wako.
7 daima kusimama na mwenzi wako hata kama dunia ikishindwa kumuelewa.
8 kumjali na kuhudumia kifedha , kiakili na kimwili.
na mengine mengi.

Upendo upo na bado upo endapo tu mtu akiwa tayari kuupata.
Namba 5 hapo kwangu ndio huwa naona kipengele. 😅😅😅

Mimi ni muelewa sana lakini nina standards zangu ambazo huwa sipendi kuingiliwa au kupuuzwa
 
Sr. Abigail; Sahau hiko kitu kabisa. Upendo ule almaarufu kama Upendo wa Agape haupo tena kabisa-sio kwa wanandoa tu bali hata kwa watu wa kawaida ambao hata hawajafungwa kwa viapo; pia hata kwa viongozi walioapa madhabahuni e.g. mapadre /watawa/wachungaji n.k. au mbele ya kadamnasi e.g. viongozi wa Kiserikali e.g. Wanajeshi n.k. au Siasa -Wabunge n.k. Woote hao kwa Ukweli halisi huwa wanaangalia maslahi binafsi zaidi. Mambo yakibuma au kuwa tofauti na matarajio yao huondoka au Hukengeuka.
Sawa mkuu
Ndio mambo yalipofikia Kwa Sasa😊
 
No No,kwani unazungumzia upendo wa agape???

Kwakweli nina muda sana kuona,ata mm nautafuta sana,kuna wimbo ameimba jamaa mmoja anaitwa ambwene mwasongwe unaitwa upendo wa kweli nadhani ndicho unazungumzia.
 
Back
Top Bottom