Ule upendo wa kweli bado upo?

Ule upendo wa kweli bado upo?

We unao huo upendo?
Ninao mwingi sana tena Najipenda mnoo

file_000000003304820c84e3a9c1bd16a42e.jpg
 
Umesema vile ninavyojua mimi, kwa kuongezea tu.....
Upendo wa kweli huanza na kujipenda kwa dhati wewe mwenyewe.
Mtu asiyethamini nafsi yake mara nyingi huwa anatafuta upendo wa kujaza pengo ndani yake. Lakini anayejipenda kwa afya ana uwezo wa kupenda bila kujipoteza, kuheshimu mipaka, kusamehe pale inapowezekana na kubaki mwaminifu bila kulazimisha.

mleta mada anauliza hivi kwa sababu huenda anaona kuna watu wameumizwa, wamekatishwa tamaa au anaangalia dhana ya upendo kupitia majeraha ya watu wengine. Lakini majeraha ya mtu mmoja hayaifuti uwepo wa upendo duniani.
Majeraha ya mtu mmoja hayafuti uwepo wa upendo duniani

Nyongeza kaka : watu tunapenda wapenzi wa watu period!
 
Naomba ufafanuzi kwenye nyongeza hapo. Kwamba watu wanapenda wapenzi wa watu, kivipi yaani? Maana maisha ya mahusiano ya kimapenzi yana siri nyingi sana 😅
Yaani una mpemda mtu kumbe ana mpenzi wake I mean ana mtu anae mpenda ambaye sio wewe

Kwahiyo umependa mpenzi wa mtu lazima ulie kilio cha mbwaaa
 
Yaani una mpemda mtu kumbe ana mpenzi wake I mean ana mtu anae mpenda ambaye sio wewe

Kwahiyo umependa mpenzi wa mtu lazima ulie kilio cha mbwaaa
Kwanini umpende mtu ambaye tayari ni mtu wa mwingine?
Kama ukisoma ile reply yangu niliyo ku-quote utanielewa.

Upendo wa kweli ni kujipenda mwenyewe. Haina sababu ya kulia kilio cha mbwa koko baada ya kuangukia kwenye upendo usio sahihi.
 
Back
Top Bottom