Ukwepaji Kodi: Barua ya TRA kwa Bakhressa

Ukwepaji Kodi: Barua ya TRA kwa Bakhressa

naomba muwe mnaweka na maandishi maana simu zetu wengne hazifungui hayo mafaili mnayo yaupload

Usijali mkuu rais wetu mpendwa JPM yuko ktk harakati za kuwapora mali mapapa ili na sisi wadogo wadogo tupate visent kidogo hivyo soon tu na we utakua na sim yenye uwezo wa kufungua mafail kama hayo.
 
Jamani ni sawa wabanwe na walipe kodi nchi yetu inatafunwa na familia chache nyingi tunakufa na njaa tu..... ila vipi kwa suala la kampuni moja bubu.....kuna hujuma wanafanyiwa vibarua....inatolewa hela kwa malipo ya kazi ya kumwaga zege msimamizi yeye anapiga nusu na anawapa nusu...ofisini washaenda na suala wala halifatiliwi jamaa mwenyewe kaushia kuwatishia kuwahachisha kazi....hili linawezapatiwa utatuzi vipi????
 
sio kwamba amekwepa kodi. hayo mkontena yamepita bandari yake bila kulipiwa kodi. maafisa wa TRA hapo kwake ndo wamecheza mchezo. yeye amesimamishwa kupokea mizigo kwa kuwa hakuisaidia serikali kukusanya kodi hapo bandari kavu kwake kama masharti yanavyoelekeza. hapo bakhresa hausiki, ila watendaji wa TRA na wale aliowaamini kuendesha ICD yake! inaonekana hayo makontena yalitoka bila ya kuwa na 'release order' kitu ambacho wangetakiwa kushtuka na kuripoti mapema ila hawakufanya hivyo na ndio maana wanaadhibiwa!

Mkuu hiyo hoja yako sikubaliani nayo, hapo kuna kamchezo kalichezwa na pande zote mbili, kwani yeye hakujua kuna kulipa kodi? Au iweje baadhi ya makontena alipie mengine asilipie? Uzuri wa ile sheria ya kodi hata ilisahaulika sasa itambidi alipie zote. Time does not run against the government
 
Hizi ni propaganda za kiccm baada ya kumuona baharesa kaengemea na kusaidia mrengo fulani ila kila kitu kinajulikana na wanaokwepa kodi pia wanajulikana.
Tena tukikuta alikue anasaidia upinzani basi atarudi kuuza kahawa Zanzibar.
 
Kiongozi kila jambo lazima lina angle za kidini ndani yake? Mi nimeona kinachozungumziwa hapa ni ukwepaji kodi na mahakama zipo kama pana shaka yoyote mahakama itatoa haki. Embu tuache haya makitu ya udini na ukanda kwenye mambo serious ya kitaifa kama haya




Mkuu hili ni tatizo kubwa sana bapa Tanzania.
Kwa muda mrefu tumekua tukiibiwa na kudhulumiwa kwa kutumia dhana za udini.
Kuna kundi la watu kazi yao ni kufanya mafyongo halafu wanapobanwa wanaleta dhana ya udini. Ooh nimefukuzwa kwa sababu ya dini yangu na blah blah nyingi utafikiri walitumwa na dini kuiba.

Magufuli awakatae hawa watu wenye mirengo ya kidini serikalini.
Futa misamaha yote ya kodi bila kujali hawa makuadi wa matajiri na wanyonyaji kwa mirengo ya kidini.
Hata misamaha ya kodi feki kwenye taasisi za dini zina makuwadi wake.Zinapoguswa wanajitokeza kwa nguvu kubwa kutetea ukwepaji wa kodi huku wananchi wengi wakiumia bila kujali dini zao.
Historia inaonyesha pia kuwa maajenti au mawakala wa ukoloni walikua ni watu wa dini. Mpaka leo kuna watu na akili zao hawatambui na hawataki kuelewa au kuelezwa kuwa Mengi ,MO ,Bakhressa ,Sas Abood na wengine hawa ni mabepari na wafanya biashara ,wanachoangalia ni kupata faida kubwa na kushika soko kwa namna yoyote na wasipodhibitiwa basi wanawashika wanasiasa na kukwepa kodi. Hawa sio mitume au manabii wa kidini. Hawa ni mitume na manabii wa kipepari. Hawa wanatambuana dunia nzima katika harakati zao za Kibepari bila kujali dini zao. Wanawatumia waumini wenzao wenye kulewa ushabiki wa kidini kufanya uhujumu wakijua mashabiki wao watapoteza malengo kwa kuibua hoja dhaifu za udini.

Hali hii imejitokeza sana kwenye biashara zote haram. Mtu akikamatwa wanaangalia dini yake na nguvu yake ndani ya dini na makuadi wao wanajitokeza na kuanza kulalamika kuwa ameonewa kwa sababu ya dini yake.
Ndio maana hata maeneo yenye wabunge wafanya biashara yanakua na huduma duni sana kwa wananchi na umaskini ni mkubwa sana.
Kampeni zikifika blah blah za udini zinawarudisha madarakani kwa kupitia makuwadi wao wa kidini kufanya ushawishi ya huyu ni muumini mwenzetu na anatusaidia kwenye misiba n.k. huku wanafunzi wa maeneo hayo wengi wakikaa chini.

Kwa kweli inefikia mahali kila mtu achukizwe na huu ujinga wa kuwatetea wezi kwa sababu tu ni muumini wa dini au dhehebu lake.
 
Wanao husisha udini hapa watakua wapumbavu, wakwepa kodi wote lazima washikishwe adabu, hakuna cha udini wala kabila.

Na kama alikua mfadhili wa Seif Sharif basi ni lazima tumfilisi ili wengine wapate adabu.
 
Mh Rais please deal na hawa wawekezaji taratibu, tunawahitaji wanatuhitaji pia. Sheria isimamiwe vzur, watumishi wazembe wawajibishwe sio yote yakufanya public mengine yatatishia uwekezaji mpya.
Sina maana wasilipe kodi, bali walipe kodi lakini pia heshima yao ilindwe.

Mugabe aliyafanya haya public, wananchi walimuita hero, lakini leo wanaisoma namba wao wenyewe. Hakuna muwekezaji anafikiria kuwekeza pamoja na sheria kulegezwa.
 
Mara kaanzisha timu,mara kaongeza speed boat ,mara....kumbe !
 
Ili kuwa ten good years ya kuneemesha wafanyabiashara "wagonga vichwa sakafuni" kwa jasho la watz masikini kabisa. Wakwepa kodi wakubwa wote ni "wagonga vichwa sakafuni"
Mwisho wao umefika warudi tuu Oman
captain Captain22
Umesahau Kanisa linavyo chota pesa za Watanzania kwa kisingizio cha MoU iliyotayarishwa na Lowassa. Kibaya zaidi hizo pesa mnajengea Makanisa makuubwa ndani yake mna ning'iniza masanamu . Pumbavu kabisa !
 
Last edited by a moderator:
I am not surprised by your comment, to say the least.
THE SS Bakhressa is still CLEAN and productive...!! Mkuu amini maneno yangu!!
Jigsaw Ahante Mkuu, ila wewe utabaki kulishwa na kuvishwa.... SS bakhressa hii siyo mara ya kwanza kutendewa !!! (hata wakifilisi a/c to zero balance... The Blessed Man atarudi zaidi mnavyotarajia) take my word !!! SS Bakhressa nchi za jirani anajulikana kuliko Bendera ya TAIFA !!!
kambagasa Umekurupuka na hao wanaochunguza nao wamekurupuka..... Wee subiri upewe ajira halafu ughushi ( "wz') makaratasi...hizo ndo fani zenu mwazijua vizuri !!
 
Last edited by a moderator:
Kwa hiyo mkuu hata yeye anahusika, maana huwezi kuvunja taratibu zilizowekwa kama huusiki

Taratibu wanavunja TRA na si Bakhresa ! movement ya kila kitu inaenda kwa mifumo na vibali ! TRA wakiacha kyasajili Makonteina katika mfumo wao, ni nani wa kuwashinikiza waingize !??
 
Huna akili wewe!!! mijizi ya escrow inatoka wapi? Lowassa ,chenge,tibaijuka,mengi ,wanaswali msikiti gani? sumaye anaswali msikiti gani? tutolee wazimu wako hapa,watawajibishwa kama wakwepa kodi wengine sio kwa sababu wanatoka dini fulani nyau wewe!! idadi kuubwa ya walisimamishwa kuanzia muhimbili mpaka TRA ni wale wanaabudu sanamu mshenzi wewe,ukileta kashfa hata sisi tunazijua zaidi yako ,ita mods wanipe ban kwa sababu nimekutukana

Shusha jazba!
 
Taratibu wanavunja TRA na si Bakhresa ! movement ya kila kitu inaenda kwa mifumo na vibali ! TRA wakiacha kyasajili Makonteina katika mfumo wao, ni nani wa kuwashinikiza waingize !??

Kweli mkuu inakuwa vigumu kuwashinikiza tra
 
Back
Top Bottom