MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 705
Nakumbuka, takriban miaka 4 iliyopita, mtu anayejiita Nabii na Mtume, Josephat Mwingira, ambaye aliwahi kutamka kwamba kabla ya kuokoka alikuwa jambazi sugu, aliwafanyia unyama wa kutisha wafanyabiashara, wajasiriamali waliokuwa wamejiajiri wenyewe, kwa kuweka vibanda vyao vya biashara, eneo la Mwenge, nje ya eneo lililokuwa la kiwanda cha umma, Mangula Plant Works (jina ni langu, lakini Mangula ni jina rasmi), ambacho kilibinafsishwa chini ya iliyokuwa Parastatal Sector Reform Commission (PSRC), sasa inaitwa Consolidated Holdings Corporation (CHC).
Bila taarifa, Mwingira alikodi magari makubwa mawili ambayo ni mitambo ya kutengeneza barabara, aina ya Caterpillar Grader na Caterpillar Scoop, ambayo yalifanya kazi ya kubomoa vibanda hivyo, jambo ambalo liliwasababishia wafanyabiashara hao hasara kubwa SANA. Wengi walifilisika, walipoteza mali na mitaji yao. Waliowahi kuokoa mali zao, walifanikiwa kuondoka mahali hapo salama. Wengi walibaki kutazama, Grader na Scoop, yakifanya maangamizi hayo, bila ya kuwa na nguvu ya kufanya lolote, kwani siku hiyo kulikuwa na magari mawili ya Polisi, aina ya LandRover Defender Pickup, yakiwa na zaidi ya askari Polisi kumi wenye silaha, wakitokea Kituo cha Polisi OysterBay. Askari hao waliitwa hapo baada ya Mwingira kuwasiliana na Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD), ambaye baada ya maelewano yao, askari walitinga hapo, kuhakikisha usalama unakuwapo.
Unyama huu wa Mwingira haukuishia hapo. Wamiliki wa viwanda vidogo vilivyo ndani ya eneo hilo la Mangula, wanatambua kwamba wao walimilikishwa maeneo yao kihalali na Serikali, kupitia PSRC, baada ya Mangula kuvunjwa. Ieleweke kwamba Mangula lilikuwa Shirika la Umma, na sio mtu binafsi.
Kwa sasa, Mwingira anaendesha kampeni ili kuhakikisha kwamba anamiliki (kwa njia yoyote ile, kana kwamba HAKUNA SERIKALI ya KUMWAJIBISHA) eneo lote la Mangula! Ameanza na kubomoa na kuharibu mali ya kiwanda cha uchapaji cha AfroPlus, ambacho kiko kwenye eneo hilo. Kwa mujibu wa habari zilizochapishwa kwenye gazeti la Uwazi, ninanukuu:
Sasa kibano kimegeuka. Kumbe na yeye anaweza kufikishwa Polisi, tena kule kule OysterBay, alikowatumia maafande kuwaharibia mali zao wajasiriamali waliokuwa wakijitafutia riziki zao, tena barabarani, na sio kwenye eneo lake la kanisa?
Sasa tujiulize, ni Nabii na Mtume gani ambaye:
Ieleweke kwamba, (mosi) eneo ilipojengwa Ephata Bank pale Mwenge ni eneo la hifadhi ya barabara, na ipo siku itakuja kubomolewa na TANROADS, anatapozuka Mkurugenzi Mkuu kichaa asiyeogopa mtu, bali anayeheshimu na kufuata/kutekeleza sheria!!!
Mwingira hafanani na huo utume na unabii wake, kwani matendo yake yanamhukumu. Wafuasi (sio waumini) wake hukesha wakiomba na kufunga, wakimwomba Mungu alete maafa kwa watu fulani ambo kwa mujibu wa Mwingira ni maadui wake, kwa mfano, Mchungaji Ambilikile Mwaisapila (Babu), ambaye wafuasi wa Mwingira walikesha na kufunga mwezi mzima, wakiomba mauti yamfikie. Mpaka leo, Babu anadunda. Ni Mungu gani huyo anayeombwa kuwaua watu wasio na hatia? Iweje, nabii na mchungaji atake watu wafe kwa amri yake yeye mwenyewe? Huyo sio Mungu, bali ni IBLIS!
Eneo ambalo linasomeka kama EPHATA NURU CENTRE, ambao limejengwa kwa upande wa mbele (mabanda .) unaopakana na Barabara Mpya ya Bagamoyo, bado linahesabiwa, kisheria, ni mali ya Serikali, kwani, kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo, eneo hilo HALIJABINAFSISHWA kwa mtu, watu au taasisi yoyote ile. Halikadhalika, eneo ambalo kuna viwanda na kampuni kadhaa, kama vile Simon Engineering, Metal Works, imber Malt Tech, Auto Ran Makongo, Container Global, Simon Engineering, Safe Man, Profession Investigation, Elbe Ltd, Zana za Kilimo Mbeya na Kilimanjaro Machine Tools Ltd, ni eneo linalomilikiwa kihalali kabisa, kwa mujibu wa Sheria, na kampuni hizo tajwa. Iweje leo, Mwingira adai kwamba anamiliki eneo lote hilo tangu Juni 17, 2005, baada ya kulinunua kutoka kwa mtu mmoja aliyemtaja kwa jina la Mangula, hivyo anasubiri tamko la Mahakama ya Ardhi Tanzania ambako shitaka limepelekwa ????
Kwanza, hakuna mtu anayeitwa Mangula. Eneo lilikuwa mali ya kiwanda cha Mangula, Shirika la Umma lililobinafsishwa! Pia, Mwingira alikuwa anatumia uhusiano wake na Waziri Mkuu Mstaafu, Sumaye, kuwatishia majirani wake wanaofanya shughuli zao kwenye eneo hilo. HUU NI UHUNI MKUBWA!
Mwingira alipeleka maombi ya kununua eneo lote, lakini akakataliwa na PSRC. Akapewa sehemu ya nyuma, lilipo kanisa lake la EPHATA. Ni eneo kubwa. Amekuwa akitumia uwanja wa mbele wa eneo hilo kuwafanyia semina za brainwashing vijana wasiokuwa na ajira, ili wawe watumwa wa kumpelekea pesa, kwa mfumo wa kuwalipisha ada za semina mbali mbali za kiroho. WIZI TU! Hakuna lolote!
Mwingira akifa leo, kama hao wachungaji wenzake, na kanisa hilo linakufa pia, kwani hataki mtu mwingine yeyote ahubiri madhabahuni kwake. Hafanani kitabia na Kakobe huyu?
Ninachojiuliza, kwa nini Serikali inakaa kimya ilhali ina taarifa zote kuhusu mambo haya? Wakati ule wale wajasiriamali walipoharibiwa mali zao na tingatinga na kijiko vya Manispaa ya Kinondoni, wakati ule Mkuu wa Wilaya akiwa Kanali Mstaafu Massawe, Kanali aliahidi kushughulikia suala lile ili wale walioharibiwa mali zao wafidiwe. Sijui nini kiliendekea.
Leo hii, wafuasi wa Mwingira wanawapiga watu na kuharibu mali za kiwanda. Hapa hakuna kesi ya jinai? Kwa nini Kamanda Kenyela awaite Mwingira na Zain Sharifu na kuwapatanisha ilhali Mwingira ameharibu, makusudi, mali za Sharifu? Kuna nini hapa? Kwa nini Mwingira analindwa huku anavunja sheria kwa makusudi kabisa?
Hapa hakuna suala la Kesi iliyopo Mahakamani. Hapa kuna uharibifu wa mali. Kuna watu wamepigwa, wameumizwa. Iweje ACP Kenyela awapatanishe? Hapa hakuna suala la KUPATANA. Mwambieni Zain Sharifu afungue kesi ya msingi, JINAI, dhidi ya Mwingira, kwani huyu SIO NABII WALA MTUME! Ni MWIZI TU!
Nimemaliza!
Che Mchochezi Excellent!
Bila taarifa, Mwingira alikodi magari makubwa mawili ambayo ni mitambo ya kutengeneza barabara, aina ya Caterpillar Grader na Caterpillar Scoop, ambayo yalifanya kazi ya kubomoa vibanda hivyo, jambo ambalo liliwasababishia wafanyabiashara hao hasara kubwa SANA. Wengi walifilisika, walipoteza mali na mitaji yao. Waliowahi kuokoa mali zao, walifanikiwa kuondoka mahali hapo salama. Wengi walibaki kutazama, Grader na Scoop, yakifanya maangamizi hayo, bila ya kuwa na nguvu ya kufanya lolote, kwani siku hiyo kulikuwa na magari mawili ya Polisi, aina ya LandRover Defender Pickup, yakiwa na zaidi ya askari Polisi kumi wenye silaha, wakitokea Kituo cha Polisi OysterBay. Askari hao waliitwa hapo baada ya Mwingira kuwasiliana na Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD), ambaye baada ya maelewano yao, askari walitinga hapo, kuhakikisha usalama unakuwapo.
Unyama huu wa Mwingira haukuishia hapo. Wamiliki wa viwanda vidogo vilivyo ndani ya eneo hilo la Mangula, wanatambua kwamba wao walimilikishwa maeneo yao kihalali na Serikali, kupitia PSRC, baada ya Mangula kuvunjwa. Ieleweke kwamba Mangula lilikuwa Shirika la Umma, na sio mtu binafsi.
Kwa sasa, Mwingira anaendesha kampeni ili kuhakikisha kwamba anamiliki (kwa njia yoyote ile, kana kwamba HAKUNA SERIKALI ya KUMWAJIBISHA) eneo lote la Mangula! Ameanza na kubomoa na kuharibu mali ya kiwanda cha uchapaji cha AfroPlus, ambacho kiko kwenye eneo hilo. Kwa mujibu wa habari zilizochapishwa kwenye gazeti la Uwazi, ninanukuu:
KIONGOZI wa Kanisa la Efatha, Nabii na Mtume Josephat Mwingira amekamatwa na polisi na kupewa kibano katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Dar es Salaam, akituhumiwa kuharibu mali za mfanyabiashara, Zain Sharifu.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, ACP Charles Kenyela, Mwingira alikamatwa wiki iliyopita na kushikiliwa kituoni hapo.
Hata hivyo, Kenyela alisema, Mwingira alidhamiwa baada ya kuhojiwa kuhusiana na tuhuma za kuvunja na kuharibu mali ndani ya Kiwanda cha Uchapaji cha Afroplus kinachomilikiwa na mlalamikaji.
Tumemkamata kiongozi huyo ili atoe ufafanuzi wa kina baada ya kupokea malalamiko hayo, alisema Kenyela alipozungumza na mwandishi wetu wiki iliyopita ofisini kwake.
Kenyela alisema, mashtaka hayo yalifikishwa polisi na Zain, Januari 8, mwaka huu, akidai kwamba walinzi binafsi wa kiongozi huyo wa kanisa, walivamia kiwandani kwake na kuharibu mali baada ya kufanya fujo.
Aliongeza kuwa polisi baada ya kupata taarifa hizo, walikwenda eneo la tukio kushuhudia na kukuta mali zilizoharibiwa, hivyo walimtaka Mwingira kufika polisi ili atoe ufafanuzi lakini alikaidi ndipo polisi ikatumia nguvu kumkamata.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, ACP Charles Kenyela, Mwingira alikamatwa wiki iliyopita na kushikiliwa kituoni hapo.
Hata hivyo, Kenyela alisema, Mwingira alidhamiwa baada ya kuhojiwa kuhusiana na tuhuma za kuvunja na kuharibu mali ndani ya Kiwanda cha Uchapaji cha Afroplus kinachomilikiwa na mlalamikaji.
Tumemkamata kiongozi huyo ili atoe ufafanuzi wa kina baada ya kupokea malalamiko hayo, alisema Kenyela alipozungumza na mwandishi wetu wiki iliyopita ofisini kwake.
Kenyela alisema, mashtaka hayo yalifikishwa polisi na Zain, Januari 8, mwaka huu, akidai kwamba walinzi binafsi wa kiongozi huyo wa kanisa, walivamia kiwandani kwake na kuharibu mali baada ya kufanya fujo.
Aliongeza kuwa polisi baada ya kupata taarifa hizo, walikwenda eneo la tukio kushuhudia na kukuta mali zilizoharibiwa, hivyo walimtaka Mwingira kufika polisi ili atoe ufafanuzi lakini alikaidi ndipo polisi ikatumia nguvu kumkamata.
Sasa kibano kimegeuka. Kumbe na yeye anaweza kufikishwa Polisi, tena kule kule OysterBay, alikowatumia maafande kuwaharibia mali zao wajasiriamali waliokuwa wakijitafutia riziki zao, tena barabarani, na sio kwenye eneo lake la kanisa?
Sasa tujiulize, ni Nabii na Mtume gani ambaye:
- Anataka kuwaondoa watu wanaomiliki maeneo yao ya kibiashara, kihalali, tena kwa nguvu, kwa kuwaharibia mali zao ili watishike, kwambe yeye ana NGUVU?
- Amekwishawaharibia watu, watafutaji, maskini, mali zao, na wengine kuwafilisi kabisa, chini ya mtutu wa bunduki, eti kwa kuwa alikuwa anasafisha barabara ya kuelekea kwenye kanisa lake?
- Anataka kujilimbikizia mali (Ardhi) bila kufuata sheria?
Ieleweke kwamba, (mosi) eneo ilipojengwa Ephata Bank pale Mwenge ni eneo la hifadhi ya barabara, na ipo siku itakuja kubomolewa na TANROADS, anatapozuka Mkurugenzi Mkuu kichaa asiyeogopa mtu, bali anayeheshimu na kufuata/kutekeleza sheria!!!
Mwingira hafanani na huo utume na unabii wake, kwani matendo yake yanamhukumu. Wafuasi (sio waumini) wake hukesha wakiomba na kufunga, wakimwomba Mungu alete maafa kwa watu fulani ambo kwa mujibu wa Mwingira ni maadui wake, kwa mfano, Mchungaji Ambilikile Mwaisapila (Babu), ambaye wafuasi wa Mwingira walikesha na kufunga mwezi mzima, wakiomba mauti yamfikie. Mpaka leo, Babu anadunda. Ni Mungu gani huyo anayeombwa kuwaua watu wasio na hatia? Iweje, nabii na mchungaji atake watu wafe kwa amri yake yeye mwenyewe? Huyo sio Mungu, bali ni IBLIS!
Eneo ambalo linasomeka kama EPHATA NURU CENTRE, ambao limejengwa kwa upande wa mbele (mabanda .) unaopakana na Barabara Mpya ya Bagamoyo, bado linahesabiwa, kisheria, ni mali ya Serikali, kwani, kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo, eneo hilo HALIJABINAFSISHWA kwa mtu, watu au taasisi yoyote ile. Halikadhalika, eneo ambalo kuna viwanda na kampuni kadhaa, kama vile Simon Engineering, Metal Works, imber Malt Tech, Auto Ran Makongo, Container Global, Simon Engineering, Safe Man, Profession Investigation, Elbe Ltd, Zana za Kilimo Mbeya na Kilimanjaro Machine Tools Ltd, ni eneo linalomilikiwa kihalali kabisa, kwa mujibu wa Sheria, na kampuni hizo tajwa. Iweje leo, Mwingira adai kwamba anamiliki eneo lote hilo tangu Juni 17, 2005, baada ya kulinunua kutoka kwa mtu mmoja aliyemtaja kwa jina la Mangula, hivyo anasubiri tamko la Mahakama ya Ardhi Tanzania ambako shitaka limepelekwa ????
Kwanza, hakuna mtu anayeitwa Mangula. Eneo lilikuwa mali ya kiwanda cha Mangula, Shirika la Umma lililobinafsishwa! Pia, Mwingira alikuwa anatumia uhusiano wake na Waziri Mkuu Mstaafu, Sumaye, kuwatishia majirani wake wanaofanya shughuli zao kwenye eneo hilo. HUU NI UHUNI MKUBWA!
Mwingira alipeleka maombi ya kununua eneo lote, lakini akakataliwa na PSRC. Akapewa sehemu ya nyuma, lilipo kanisa lake la EPHATA. Ni eneo kubwa. Amekuwa akitumia uwanja wa mbele wa eneo hilo kuwafanyia semina za brainwashing vijana wasiokuwa na ajira, ili wawe watumwa wa kumpelekea pesa, kwa mfumo wa kuwalipisha ada za semina mbali mbali za kiroho. WIZI TU! Hakuna lolote!
Mwingira akifa leo, kama hao wachungaji wenzake, na kanisa hilo linakufa pia, kwani hataki mtu mwingine yeyote ahubiri madhabahuni kwake. Hafanani kitabia na Kakobe huyu?
Ninachojiuliza, kwa nini Serikali inakaa kimya ilhali ina taarifa zote kuhusu mambo haya? Wakati ule wale wajasiriamali walipoharibiwa mali zao na tingatinga na kijiko vya Manispaa ya Kinondoni, wakati ule Mkuu wa Wilaya akiwa Kanali Mstaafu Massawe, Kanali aliahidi kushughulikia suala lile ili wale walioharibiwa mali zao wafidiwe. Sijui nini kiliendekea.
Leo hii, wafuasi wa Mwingira wanawapiga watu na kuharibu mali za kiwanda. Hapa hakuna kesi ya jinai? Kwa nini Kamanda Kenyela awaite Mwingira na Zain Sharifu na kuwapatanisha ilhali Mwingira ameharibu, makusudi, mali za Sharifu? Kuna nini hapa? Kwa nini Mwingira analindwa huku anavunja sheria kwa makusudi kabisa?
Hapa hakuna suala la Kesi iliyopo Mahakamani. Hapa kuna uharibifu wa mali. Kuna watu wamepigwa, wameumizwa. Iweje ACP Kenyela awapatanishe? Hapa hakuna suala la KUPATANA. Mwambieni Zain Sharifu afungue kesi ya msingi, JINAI, dhidi ya Mwingira, kwani huyu SIO NABII WALA MTUME! Ni MWIZI TU!
Nimemaliza!
Che Mchochezi Excellent!