Ukweli lazima usemwe

soma hapa ili ujue kweli na uweze kusema ukweli:

EFATHA FOUNDATION LTD

P.O BOX 32174, MWENGE, DAR ESSALAAM

TELEPHONE:+255732993196, FAX:+255732993196

WEBSITE:www.efathafoundation.org

EMAIL: efathafoundationltd@yahoo.com /info@efathafoundation.org




OUR REF: EFL/ADMN/4/2012

DATE: 11[SUP]th[/SUP]April, 2012


TAARIFAKWA UMMA
1. UMILIKIWA KIWANJA NA. 90, ENEO LA MWENGE (NURU CENTRE)

1.1 Utangulizi

Tarehe 9 mwezi April 2012,Jumatatu ya Pasaka,baadhi ya vyombo vya habari vilitangaza habari ya umiliki namatukio yaliyotokea katika eneo hilo. Habari zilizotangazwa ni za upande mmojana hazina usahihi. Huduma ya Efatha inapenda kuelezea umma taarifa sahihi juuya upatikanaji wa kiwanja na 90, umiliki na matukio yaliyotokea katika eneohilo.

1.2 Upatikanaji na umiliki wa eneo

Serikali kupitia Tume ya Kurekebishana Kubinafsisha Mashirika ya Umma (PSRC) ilitangaza zabuni ya uuzwaji wa eneola Mang'ula Mechanical and Machine Tools Company Ltd iliyofilisika, Kiwanjanamba 90, Mwenge katika magazeti ya Uhuru na Daily News ya tarehe 4 mwezi Mei2005.

Tarehe 18 Mei 2005, huduma yaEfatha kupitia kitengo chake cha uchumi, Efatha Foundation Ltd, ilipelekamaombi ya zabuni ya kununua eneo hilo PSRC.

Efatha Foundation Ltd ilipokeabarua kutoka PSRC yenye kumbukumbu Na. PSRC/1/13/93 ya tarehe 30 Mei 2005 ikiarifu kwamba zabuni yetu ya kununua eneohilo imeshinda kwa kiasi cha shilingi za kitanzania milioni mia nne.

Masharti ya Malipo ya zabuniyalikuwa asilimia kumi ilipwe wakati wa kupeleka maombi na asilimia tisiniilipwe ndani ya miezi mitatu baada ya kushinda zabuni.Efatha Foundation Ltd ililipashilingi milioni arobaini yaani asilimia kumi ya bei siku ya kupeleka maombi yazabuni kwa hundi Na. 000261 ya benki ya Azania na kupewa risiti ya PSRC Na.6956 ya tarehe 31 Mei 2005. Na shilingi milioni mia tatu sitini ililipwakupitia hundi Na. 000319 ya benki ya Azania ambayo ni asilimia tisini tarehe 10mwezi Juni 2005 na kupewa risiti ya PSRC Namba 6984 na hivyo malipo yote yakawayamekamilishwa.

Baada ya kukamilisha malipoEfatha Foundation Ltd ilikabidhiwa hati miliki Namba 41641 ambayo ilipelekwawizara ya Ardhi ili ibadilishwe jina kutoka mmiliki wa mwanzo na kuandikishwajina la Efatha Foundation Ltd. Kwa hiyo Serikali ikahamisha umiliki kutoka Mang'ula Mechanical and Machine Tools CompanyLtd iliyofilisika kwenda Efatha Foundation ltd tarehe 15 Novemba 2005 saa sitakamili mchana kwa uhamisho Namba 98648.Kabla ya Huduma ya Efathakununua eneo hilo kulikuwa na wavamiziambao ni makampuni na watu binafsi kumi na moja ambao walikuwa wamewekwa katikaeneo hilo na Mang'ula Mechanical andMachine Tools Company Ltd iliyofilisika bila kibali cha mfilisi yaani PSRC. Kwakuwa hawakuwa wapangaji halali walikuwa wavamizi (trespassers). Wavamizi haowakapewa notisi ya kuondoka na PSRC lakini hawakuondoka. Baadae shughuli zamfilisi, PSRC, zikachukuliwa kisheria na Consolidated Holding Corporation(CHC). CHC nao wakawapa wale wavamizi notisi kuwa waondoke kwa sababu eneo hilolimeuzwa lakini hawakuondoka.

EfathaFoundation Ltd ilipomiliki eneo hili kihalali na kisheria wakawapa wavamizinotisi ya kuondoka mwaka 2005, wavamizi nane wakatii amri wakaondoka na wavamizi watatu walikaidi kuondoka ambaoni pamoja na Afro Plus Industries Ltd.
Baada ya hapo wavamizi watatu waliokataa kuhama wakafungua kesimahakamani dhidi ya Efatha Foundation Ltd wakipinga kuhamishwa. Ni vyema ieleweke kuwa Efatha Foundation Ltd iliponunua eneo hilithamani yake ilijumuisha majengo yaliyokuwa yamejengwa humo na Mang'ula Mechanical and Machine Tools CompanyLtd iliyofilisika. Hii ni pamoja na jengo alilokuwa anatumia Afro PlusIndustries Ltd ambalo linalalamikiwa kubomolewa na kwamba tumeharibu mali.Jengo lililobomolewa ni mali ya Efatha Foundation Ltd na siyo mali ya Afro PlusIndustries Ltd kama ilivyodaiwa.

2. UVAMIZIWA POLISI NDANI YA KANISA LA EFATHA MWENGE

Tarehe 9 Aprili 2012, jumatatuya pasaka, majira ya saa kumi na mbili asubuhi waumini wa Efatha walikuwakatika ibada ya morning glory katika kanisa la Efatha Mwenge wakiongozwa katikaibada hiyo na Mchungaji David Mwakisole ndani ya kanisa. Kanisa limezungushiwaukuta pande zote nne na lina mageti ya kuingilia kanisani ambayo yanafungwa.Polisi walipanda ukuta wakachungulia wakasikika wakisema hawa huku ndani. Baadae polisi wakarukia ndani kupitiaukutani. Wakati ibada inaendelea ghafla waumini walivamiwa kutoka nje na watuambao baadae walitambuliwa kuwa ni polisi. Walipoingia kwa nguvu wakatupamabomu ya machozi ndani ya kanisa huku wakifyatua risasi za moto wakati ibadaikiendelea. Kwa kitendo hicho ibada ilivurugika na kusimama na waumini wakaanzakukimbia ovyo ndani ya kanisa. Risasi namabomu ya machozi yalitupwa kuelekea madhabahuni na kuelekea kwa wauminiwaliokuwa katika ibada. Waumini wengine waliokuwa wakija kwenye ibadawalizuiliwa nje na kukamatwa. Kilichofuata ni vurugu huku waumini wakikimbia napolisi wakiwapiga kwa virungu, vitako vya bunduki na mateke. Baadhi ya waumini walijeruhiwa vibaya sehemumbalimbali za mwili na ukumbi wa kanisa ulitapakaa damu. Pia polisi walivunjamadirisha, viti, milango na spika kama ilivyoonyeshwa katika baadhi ya vyombovya habari hasa ITV. Kabla hawajavamia, mmoja wa askari aliwatahadharishawenzake kuwa wasipige mabomu na risasi kwa kuwa hapo ni kanisani lakini wenzakewalipinga wakisema kuwa huyu mtu ana kiburi na watu hawa ni wakorofi. Wakatirisasi na mabomu yakipigwa baadhi ya askari walikuwa wakiokota maganda yarisasi na mabaki ya mabomu ya machozi ili kuondoa ushahidi. Hata hivyo baadhiya risasi za moto, maganda ya risasi zamoto na mabaki ya mabomu yalibaki kanisani na yamehifadhiwa mahali maalum kwahatua zaidi.Kanisani kulikuwa na idadi yawaumini kati ya sitini na sabini waliokuwa wanaabudu. Polisi waliwakamata jumlaya waumini 53 pamoja na wachungaji waliokuwa wakiongoza ibada wakiwapiga nakuwasweka katika magari ya polisi kuwapeleka kituoni pamoja na kuvuta garizilizokuwa zimeegeshwa nje ya kanisa kwa breakdown. Tumepata habari kuwawalikuja na baadhi ya waandishi wa habari walioandaliwa kabla ili kurekoditukio hilo na ushahidi tunao. Kwetu sisi inaonyesha kuwa tukio hiloliliandaliwa kwa makusudi ili likatekelezwe katika kanisa la Efatha. Tukio hililinatupa hisia kuwa kuna chuki kubwa kwa Huduma ya Efatha.

Kitendo cha polisi kuvamia nakuvuruga ibada ni kinyume na sheria na katiba ya jamhuri ya Muungano waTanzania iliyoweka uhuru wa kuabudu na sheria za nchi zinazoeleza kwamba ibadaziheshimiwe na zisiingiliwe. Tunajiuliza kulikuwa na tatizo gani polisiwasisubiri nje ibada iishe na wawachukue watu wanaotaka kuwachukua. Ndani yakanisa hakukuwa na vita, wala mtu mwenye silaha, wala mtu anayeuawa ambayepolisi walilazimika kwenda kumwokoa. Sisi tunaliona hili kuwa ni kumdharauMungu, kuvuruga ibada na kuwadhalilisha waumini wa Efatha waliokuwa wakitumiauhuru wao wa kuabudu. Leo wamefanya hivyo kwa dharau ndani ya kanisa la Efatha, kesho tutegemee watakwenda kufanya nini kwa dhehebu jingine, Msikiti, Dininyingine au watu waliokusanyika kihalali na kwa sababu halali?

3. MAJUMUISHO

Vielelezo vyote kuhusuumiliki wetu halali wa eneo hilivilishawasilishwa polisi mkoani na wilayani. Kutokana na maelezo haya EfathaFoundation Ltd inapenda kuuthibitishia umma kuwa EFATHA FOUNDATION LTD ndiyommiliki halali wa KIWANJA NA. 90, ENEO LA MWENGE (NURU CENTRE) na sivinginevyo.


KATIBU

EFATHA FOUNDATION LTD
 
Hii Efatha Limited na Waumini ni ma shareholders au vipi? Yaani Kazi ya Mungu inafanywa na watu wanaojitambulisha kama Ltd, Njoja nikasali aisee, Naona the end has come.
 

3. MAJUMUISHO

Vielelezo vyote kuhusu umiliki wetu halali wa eneo hili vilishawasilishwa polisi mkoani
na wilayani. Kutokana na maelezo haya Efatha Foundation Ltd inapenda kuuthibitishia
umma kuwa EFATHA FOUNDATION LTD ndiyo mmiliki halali wa KIWANJA NA. 90, ENEO
LA MWENGE (NURU CENTRE) na si vinginevyo.

KATIBU
EFATHA FOUNDATION LTD


JF mbona tunaanza kukurupuka, We must be great thinkers.
 
Katika masuala ya imani za kiroho, kanuni kuu inayofanya kazi ni moja tu; ni UHURU WA MTU KUAMINI NA KUFUATA KILE ANACHOAMINI. Sidhani kama kuna MFUASI yoyote wa dini au wa kiongozi wa kidini hapa Tanzania atakayedai kuwa amelazimishwa, ameburuzwa au ametishiwa ili afuate dini au amfuate kiongozi yeyote wa kidini. Aidha, wafuasi wote ni watu wazima wenye akili zao timamu. Tena si kwamba ni watu ambao hawajaenda shule. Sasa, wanaoamua kuwafuata Mwingira, Kakobe, Rwakatare, n.k. na kuwakabidhi nafsi na rasilimali zao naamini hao wanajua manufaa wanayoyapata huko.

Hivyo, kama kuna hoja ya kujadili hapa ni kuhusiana na vitendo vya kijinai (vinavyohusisha viongozi wa kidini) ambavyo tunaona havishughulikiwi ipasavyo na si kuhangaika na imani za watu wazima wenye fahamu zao. Kama ni utapeli, basi ndio sehemu ya maisha yetu katika kila fani: siasa, biashara, mapenzi, you name it. Hapo ndipo ile busara ya "mnunuzi kuwa makini" (buyer beware!) inapotakiwa kutumika ni kila mtu. Halafu hii mada haiko kwake hapa.
 
Nashukuru kwa uchambuzi wako mzuri. Ili watu wengi wasome ujumbe huu weka maneno yako ya mwisho kuhusu Mwingira, yaani rusha upya mada hii - wengi wangependa kujua.

"Mwingira SIO NABII WALA MTUME! Ni MWIZI TU!"

ushauri wangu kwenu wana jamvi, Imeandikwa 'usimnyooshee mpakwa mafuta wa Bwana kidole'. Hukumu yake anayo Mungu mwenyewe. jamani msiwakashifu wala kuwahukumu ni laana kwako. Ni kweli sisi binadamu huwa tunaangalia matunda na Mungu ndiye anayeangalia roho. Na kama hatuoni matunda kwako hatuna haja na Mungu wako. lakini tusiwahukumu kama huoni matunda kwake usitake akuchunge tafuta ambaye ana matunda kwako akuchunge. juu ya hukumu au hata kisasi hiyo ni kazi ya Mungu.na uzuri Mungu huwa anajibu mapema sana wala tusiwe na wasiwasi.
 
Nakumbuka, takriban miaka 4 iliyopita, mtu anayejiita Nabii na Mtume, Josephat Mwingira, ambaye aliwahi kutamka kwamba kabla ya “kuokoka” alikuwa jambazi sugu, aliwafanyia unyama wa kutisha wafanyabiashara, wajasiriamali waliokuwa wamejiajiri wenyewe, kwa kuweka vibanda vyao vya biashara, eneo la Mwenge, nje ya eneo lililokuwa la kiwanda cha umma, Mang’ula Plant Works (jina ni langu, lakini “Mang’ula” ni jina rasmi), ambacho kilibinafsishwa chini ya iliyokuwa Parastatal Sector Reform Commission (PSRC), sasa inaitwa Consolidated Holdings Corporation (CHC).

Bila taarifa, Mwingira alikodi magari makubwa mawili ambayo ni mitambo ya kutengeneza barabara, aina ya Caterpillar Grader na Caterpillar Scoop, ambayo yalifanya kazi ya kubomoa vibanda hivyo, jambo ambalo liliwasababishia wafanyabiashara hao hasara kubwa SANA. Wengi walifilisika, walipoteza mali na mitaji yao. Waliowahi kuokoa mali zao, walifanikiwa kuondoka mahali hapo salama. Wengi walibaki kutazama, Grader na Scoop, yakifanya maangamizi hayo, bila ya kuwa na nguvu ya kufanya lolote, kwani siku hiyo kulikuwa na magari mawili ya Polisi, aina ya LandRover Defender Pickup, yakiwa na zaidi ya askari Polisi kumi wenye silaha, wakitokea Kituo cha Polisi OysterBay. Askari hao waliitwa hapo baada ya Mwingira kuwasiliana na Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD), ambaye baada ya “maelewano” yao, askari walitinga hapo, kuhakikisha “usalama” unakuwapo.

Unyama huu wa Mwingira haukuishia hapo. Wamiliki wa viwanda vidogo vilivyo ndani ya eneo hilo la Mang’ula, wanatambua kwamba wao walimilikishwa maeneo yao kihalali na Serikali, kupitia PSRC, baada ya Mang’ula kuvunjwa. Ieleweke kwamba Mang’ula lilikuwa Shirika la Umma, na sio mtu binafsi.

Kwa sasa, Mwingira anaendesha kampeni ili kuhakikisha kwamba anamiliki (kwa njia yoyote ile, kana kwamba HAKUNA SERIKALI ya KUMWAJIBISHA) eneo lote la Mang’ula! Ameanza na kubomoa na kuharibu mali ya kiwanda cha uchapaji cha AfroPlus, ambacho kiko kwenye eneo hilo. Kwa mujibu wa habari zilizochapishwa kwenye gazeti la Uwazi, ninanukuu:
“KIONGOZI wa Kanisa la Efatha, Nabii na Mtume Josephat Mwingira amekamatwa na polisi na kupewa kibano katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Dar es Salaam, akituhumiwa kuharibu mali za mfanyabiashara, Zain Sharifu.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, ACP Charles Kenyela, Mwingira alikamatwa wiki iliyopita na kushikiliwa kituoni hapo.


Hata hivyo, Kenyela alisema, Mwingira alidhamiwa baada ya kuhojiwa kuhusiana na tuhuma za kuvunja na kuharibu mali ndani ya Kiwanda cha Uchapaji cha Afroplus kinachomilikiwa na mlalamikaji.

“Tumemkamata kiongozi huyo ili atoe ufafanuzi wa kina baada ya kupokea malalamiko hayo, “ alisema Kenyela alipozungumza na mwandishi wetu wiki iliyopita ofisini kwake.

Kenyela alisema, mashtaka hayo yalifikishwa polisi na Zain, Januari 8, mwaka huu, akidai kwamba walinzi binafsi wa kiongozi huyo wa kanisa, walivamia kiwandani kwake na kuharibu mali baada ya kufanya fujo.

Aliongeza kuwa polisi baada ya kupata taarifa hizo, walikwenda eneo la tukio kushuhudia na kukuta mali zilizoharibiwa, hivyo walimtaka Mwingira kufika polisi ili atoe ufafanuzi lakini alikaidi ndipo polisi ikatumia nguvu kumkamata.”


Sasa kibano kimegeuka. Kumbe na yeye anaweza kufikishwa Polisi, tena kule kule OysterBay, alikowatumia maafande kuwaharibia mali zao wajasiriamali waliokuwa wakijitafutia riziki zao, tena barabarani, na sio kwenye eneo lake la “kanisa”?

Sasa tujiulize, ni Nabii na Mtume gani ambaye:


  1. Anataka kuwaondoa watu wanaomiliki maeneo yao ya kibiashara, kihalali, tena kwa nguvu, kwa kuwaharibia mali zao ili watishike, kwambe yeye ana NGUVU?
  2. Amekwishawaharibia watu, watafutaji, maskini, mali zao, na wengine kuwafilisi kabisa, chini ya mtutu wa bunduki, eti kwa kuwa alikuwa “anasafisha barabara” ya kuelekea kwenye “kanisa” lake?
  3. Anataka kujilimbikizia mali (Ardhi) bila kufuata sheria?

Ieleweke kwamba, (mosi) eneo ilipojengwa Ephata Bank pale Mwenge ni eneo la hifadhi ya barabara, na ipo siku itakuja kubomolewa na TANROADS, anatapozuka Mkurugenzi Mkuu “kichaa” asiyeogopa mtu, bali anayeheshimu na kufuata/kutekeleza sheria!!!

Mwingira hafanani na huo “utume na unabii” wake, kwani matendo yake yanamhukumu. Wafuasi (sio “waumini”) wake hukesha wakiomba na kufunga, wakimwomba “Mungu” alete maafa kwa watu fulani ambo kwa mujibu wa Mwingira ni “maadui” wake, kwa mfano, Mchungaji Ambilikile Mwaisapila (“Babu”), ambaye “wafuasi” wa Mwingira walikesha na kufunga mwezi mzima, wakiomba mauti yamfikie. Mpaka leo, “Babu” anadunda. Ni “Mungu” gani huyo anayeombwa kuwaua watu wasio na hatia? Iweje, “nabii na mchungaji” atake watu wafe kwa amri yake yeye mwenyewe? Huyo sio “Mungu”, bali ni IBLIS!

Eneo ambalo linasomeka kama EPHATA NURU CENTRE, ambao limejengwa kwa upande wa mbele (mabanda ….) unaopakana na Barabara Mpya ya Bagamoyo, bado linahesabiwa, kisheria, ni mali ya Serikali, kwani, kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo, eneo hilo HALIJABINAFSISHWA kwa mtu, watu au taasisi yoyote ile. Halikadhalika, eneo ambalo kuna viwanda na kampuni kadhaa, kama vile Simon Engineering, Metal Works, imber Malt Tech, Auto Ran Makongo, Container Global, Simon Engineering, Safe Man, Profession Investigation, Elbe Ltd, Zana za Kilimo Mbeya na Kilimanjaro Machine Tools Ltd, ni eneo linalomilikiwa kihalali kabisa, kwa mujibu wa Sheria, na kampuni hizo tajwa. Iweje leo, Mwingira adai kwamba anamiliki eneo lote hilo “tangu Juni 17, 2005, baada ya kulinunua kutoka kwa mtu mmoja aliyemtaja kwa jina la Mangula, hivyo anasubiri tamko la Mahakama ya Ardhi Tanzania ambako shitaka limepelekwa…”????

Kwanza, hakuna mtu anayeitwa “Mangula”. Eneo lilikuwa mali ya kiwanda cha “Mang’ula”, Shirika la Umma lililobinafsishwa! Pia, Mwingira alikuwa anatumia uhusiano wake na Waziri Mkuu Mstaafu, Sumaye, kuwatishia majirani wake wanaofanya shughuli zao kwenye eneo hilo. HUU NI UHUNI MKUBWA!

Mwingira alipeleka maombi ya kununua eneo lote, lakini akakataliwa na PSRC. Akapewa sehemu ya nyuma, lilipo kanisa lake la EPHATA. Ni eneo kubwa. Amekuwa akitumia uwanja wa mbele wa eneo hilo kuwafanyia semina za “brainwashing” vijana wasiokuwa na ajira, ili wawe watumwa wa kumpelekea pesa, kwa mfumo wa kuwalipisha ada za semina mbali mbali za “kiroho”. WIZI TU! Hakuna lolote!

Mwingira akifa leo, kama hao “wachungaji” wenzake, na “kanisa” hilo linakufa pia, kwani hataki mtu mwingine yeyote “ahubiri” madhabahuni kwake. Hafanani kitabia na Kakobe huyu?

Ninachojiuliza, kwa nini Serikali inakaa kimya ilhali ina taarifa zote kuhusu mambo haya? Wakati ule wale wajasiriamali walipoharibiwa mali zao na “tingatinga” na “kijiko” vya Manispaa ya Kinondoni, wakati ule Mkuu wa Wilaya akiwa Kanali Mstaafu Massawe, Kanali aliahidi kushughulikia suala lile ili wale walioharibiwa mali zao wafidiwe. Sijui nini kiliendekea.

Leo hii, “wafuasi” wa Mwingira wanawapiga watu na kuharibu mali za kiwanda. Hapa hakuna kesi ya jinai? Kwa nini Kamanda Kenyela awaite Mwingira na Zain Sharifu na “kuwapatanisha” ilhali Mwingira ameharibu, makusudi, mali za Sharifu? Kuna nini hapa? Kwa nini Mwingira analindwa huku anavunja sheria kwa makusudi kabisa?

Hapa hakuna suala la Kesi iliyopo Mahakamani. Hapa kuna uharibifu wa mali. Kuna watu wamepigwa, wameumizwa. Iweje ACP Kenyela awapatanishe? Hapa hakuna suala la KUPATANA. Mwambieni Zain Sharifu afungue kesi ya msingi, JINAI, dhidi ya Mwingira, kwani huyu SIO NABII WALA MTUME! Ni MWIZI TU!

Nimemaliza!

Che Mchochezi Excellent!
Huyo jamaa hata mimi sina imani naye lakini niseme neno kidogo
  • kuhusu luwafukuza wamachinga huwezi mlaumu labda alinunua eneo akaona ajenge nyumba ya Mungu ma sehemu iwe ya utulivu na amani kuwaacha watu tu pale haikuwa jambo jema,walitakiwa waende sehemu nyingine
  • kwa maelezo ya mwingira anasema alinunua eneo lote huku kwenye viwanda na kule kwenye kanisa,lakini hawa wenye wviwanda walipewa muda maalum kuondoka kama miaka kadhaa amabyo anasema muda huo umekwishapita,Hivyo ni bora tuiache mahakama ifanye kazi yake
  • Huwezi mlaumu Mwingira kwa kutomwamini Babu wa loliondo maana mpaka sasa inaonekana huyo babu asilimia kubwa ulikuwa msanii sasa hapo wale ambao hawakumuamini huwezi walaumu maana hata huyo babu naye ni utata
  • kitendo cha kuwaombea kifo kweli sio kizuri na hata mimi simuungi mkono,mambo ya unabii wake na utume nadhani MUNGU ndiye anayejua TUSIHUKUMU,wako mitume wengi zamani walifanya mabaya zaidi kabla ya kuokoka kama mtume Paul ambaye alikuwa anaitwa sauli,akina daudi,suleima wote kuna mahali waliteleza kwa mauaji au uzinzi hivyo background au kuteleza kwa dhambi sio kigezo sio mtumishi wa Mungu,ingawa nakubali kweli anawezekana amekosea yeye
 
jamani hebu tusikurupuke. hapa mgomvi ni nani? napata picha hao madalali mm nawaita(PSRC) ndio waliouza mara 2. utapeli huu jamani!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mnamwandama kwa sababu ni MUISLAAM. Angelikuwa Mgalatia kama nyie wala msingelisema.

Hii Tanzania yetu hii, kasheshe kweli kweli. Hivi yule mama wa Igunga mwenye Hijab, mumewe anafuga Mbuzi gani vile?
 
Hivi unajua eneo hilo liliuzwa na serikali kwa Mtume na Nabii na nyaraka zipo.Je wakulaumiwa ni hawa wavamizi ambao hawataki kutoka au serikali iliyouza kihalali....Hao wanaosema wamepewa kihalali wanazo nyaraka?
Jamani tusiwe washabiki tuzungumze tukiwa na vielelezo
 
Huyo jamaa hata mimi sina imani naye lakini niseme neno kidogo
  • kuhusu luwafukuza wamachinga huwezi mlaumu labda alinunua eneo akaona ajenge nyumba ya Mungu ma sehemu iwe ya utulivu na amani kuwaacha watu tu pale haikuwa jambo jema,walitakiwa waende sehemu nyingine
  • kwa maelezo ya mwingira anasema alinunua eneo lote huku kwenye viwanda na kule kwenye kanisa,lakini hawa wenye wviwanda walipewa muda maalum kuondoka kama miaka kadhaa amabyo anasema muda huo umekwishapita,Hivyo ni bora tuiache mahakama ifanye kazi yake
  • Huwezi mlaumu Mwingira kwa kutomwamini Babu wa loliondo maana mpaka sasa inaonekana huyo babu asilimia kubwa ulikuwa msanii sasa hapo wale ambao hawakumuamini huwezi walaumu maana hata huyo babu naye ni utata
  • kitendo cha kuwaombea kifo kweli sio kizuri na hata mimi simuungi mkono,mambo ya unabii wake na utume nadhani MUNGU ndiye anayejua TUSIHUKUMU,wako mitume wengi zamani walifanya mabaya zaidi kabla ya kuokoka kama mtume Paul ambaye alikuwa anaitwa sauli,akina daudi,suleima wote kuna mahali waliteleza kwa mauaji au uzinzi hivyo background au kuteleza kwa dhambi sio kigezo sio mtumishi wa Mungu,ingawa nakubali kweli anawezekana amekosea yeye
upo sahihi, lakini tamko la ephata wana lalamika kuvamiwa na polisi, wakati wao wamevamia kiwanda bila kujali kesi ya msing iliyopo mahakamani. wanalalamikia uhuru wa kuabudu ndani ya katiba lakini hawazungumzii kuvunja sheria ndani ya katiba........... HAWA KWELI NI WAHUNI
 
Nakumbuka, takriban miaka 4 iliyopita, mtu anayejiita Nabii na Mtume, Josephat Mwingira, ambaye aliwahi kutamka kwamba kabla ya “kuokoka” alikuwa jambazi sugu, aliwafanyia unyama wa kutisha wafanyabiashara, wajasiriamali waliokuwa wamejiajiri wenyewe, kwa kuweka vibanda vyao vya biashara, eneo la Mwenge, nje ya eneo lililokuwa la kiwanda cha umma, Mang’ula Plant Works (jina ni langu, lakini “Mang’ula” ni jina rasmi), ambacho kilibinafsishwa chini ya iliyokuwa Parastatal Sector Reform Commission (PSRC), sasa inaitwa Consolidated Holdings Corporation (CHC).

Bila taarifa, Mwingira alikodi magari makubwa mawili ambayo ni mitambo ya kutengeneza barabara, aina ya Caterpillar Grader na Caterpillar Scoop, ambayo yalifanya kazi ya kubomoa vibanda hivyo, jambo ambalo liliwasababishia wafanyabiashara hao hasara kubwa SANA. Wengi walifilisika, walipoteza mali na mitaji yao. Waliowahi kuokoa mali zao, walifanikiwa kuondoka mahali hapo salama. Wengi walibaki kutazama, Grader na Scoop, yakifanya maangamizi hayo, bila ya kuwa na nguvu ya kufanya lolote, kwani siku hiyo kulikuwa na magari mawili ya Polisi, aina ya LandRover Defender Pickup, yakiwa na zaidi ya askari Polisi kumi wenye silaha, wakitokea Kituo cha Polisi OysterBay. Askari hao waliitwa hapo baada ya Mwingira kuwasiliana na Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD), ambaye baada ya “maelewano” yao, askari walitinga hapo, kuhakikisha “usalama” unakuwapo.

Unyama huu wa Mwingira haukuishia hapo. Wamiliki wa viwanda vidogo vilivyo ndani ya eneo hilo la Mang’ula, wanatambua kwamba wao walimilikishwa maeneo yao kihalali na Serikali, kupitia PSRC, baada ya Mang’ula kuvunjwa. Ieleweke kwamba Mang’ula lilikuwa Shirika la Umma, na sio mtu binafsi.

Kwa sasa, Mwingira anaendesha kampeni ili kuhakikisha kwamba anamiliki (kwa njia yoyote ile, kana kwamba HAKUNA SERIKALI ya KUMWAJIBISHA) eneo lote la Mang’ula! Ameanza na kubomoa na kuharibu mali ya kiwanda cha uchapaji cha AfroPlus, ambacho kiko kwenye eneo hilo. Kwa mujibu wa habari zilizochapishwa kwenye gazeti la Uwazi, ninanukuu:
“KIONGOZI wa Kanisa la Efatha, Nabii na Mtume Josephat Mwingira amekamatwa na polisi na kupewa kibano katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Dar es Salaam, akituhumiwa kuharibu mali za mfanyabiashara, Zain Sharifu.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, ACP Charles Kenyela, Mwingira alikamatwa wiki iliyopita na kushikiliwa kituoni hapo.


Hata hivyo, Kenyela alisema, Mwingira alidhamiwa baada ya kuhojiwa kuhusiana na tuhuma za kuvunja na kuharibu mali ndani ya Kiwanda cha Uchapaji cha Afroplus kinachomilikiwa na mlalamikaji.

“Tumemkamata kiongozi huyo ili atoe ufafanuzi wa kina baada ya kupokea malalamiko hayo, “ alisema Kenyela alipozungumza na mwandishi wetu wiki iliyopita ofisini kwake.

Kenyela alisema, mashtaka hayo yalifikishwa polisi na Zain, Januari 8, mwaka huu, akidai kwamba walinzi binafsi wa kiongozi huyo wa kanisa, walivamia kiwandani kwake na kuharibu mali baada ya kufanya fujo.

Aliongeza kuwa polisi baada ya kupata taarifa hizo, walikwenda eneo la tukio kushuhudia na kukuta mali zilizoharibiwa, hivyo walimtaka Mwingira kufika polisi ili atoe ufafanuzi lakini alikaidi ndipo polisi ikatumia nguvu kumkamata.”


Sasa kibano kimegeuka. Kumbe na yeye anaweza kufikishwa Polisi, tena kule kule OysterBay, alikowatumia maafande kuwaharibia mali zao wajasiriamali waliokuwa wakijitafutia riziki zao, tena barabarani, na sio kwenye eneo lake la “kanisa”?

Sasa tujiulize, ni Nabii na Mtume gani ambaye:


  1. Anataka kuwaondoa watu wanaomiliki maeneo yao ya kibiashara, kihalali, tena kwa nguvu, kwa kuwaharibia mali zao ili watishike, kwambe yeye ana NGUVU?
  2. Amekwishawaharibia watu, watafutaji, maskini, mali zao, na wengine kuwafilisi kabisa, chini ya mtutu wa bunduki, eti kwa kuwa alikuwa “anasafisha barabara” ya kuelekea kwenye “kanisa” lake?
  3. Anataka kujilimbikizia mali (Ardhi) bila kufuata sheria?

Ieleweke kwamba, (mosi) eneo ilipojengwa Ephata Bank pale Mwenge ni eneo la hifadhi ya barabara, na ipo siku itakuja kubomolewa na TANROADS, anatapozuka Mkurugenzi Mkuu “kichaa” asiyeogopa mtu, bali anayeheshimu na kufuata/kutekeleza sheria!!!

Mwingira hafanani na huo “utume na unabii” wake, kwani matendo yake yanamhukumu. Wafuasi (sio “waumini”) wake hukesha wakiomba na kufunga, wakimwomba “Mungu” alete maafa kwa watu fulani ambo kwa mujibu wa Mwingira ni “maadui” wake, kwa mfano, Mchungaji Ambilikile Mwaisapila (“Babu”), ambaye “wafuasi” wa Mwingira walikesha na kufunga mwezi mzima, wakiomba mauti yamfikie. Mpaka leo, “Babu” anadunda. Ni “Mungu” gani huyo anayeombwa kuwaua watu wasio na hatia? Iweje, “nabii na mchungaji” atake watu wafe kwa amri yake yeye mwenyewe? Huyo sio “Mungu”, bali ni IBLIS!

Eneo ambalo linasomeka kama EPHATA NURU CENTRE, ambao limejengwa kwa upande wa mbele (mabanda ….) unaopakana na Barabara Mpya ya Bagamoyo, bado linahesabiwa, kisheria, ni mali ya Serikali, kwani, kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo, eneo hilo HALIJABINAFSISHWA kwa mtu, watu au taasisi yoyote ile. Halikadhalika, eneo ambalo kuna viwanda na kampuni kadhaa, kama vile Simon Engineering, Metal Works, imber Malt Tech, Auto Ran Makongo, Container Global, Simon Engineering, Safe Man, Profession Investigation, Elbe Ltd, Zana za Kilimo Mbeya na Kilimanjaro Machine Tools Ltd, ni eneo linalomilikiwa kihalali kabisa, kwa mujibu wa Sheria, na kampuni hizo tajwa. Iweje leo, Mwingira adai kwamba anamiliki eneo lote hilo “tangu Juni 17, 2005, baada ya kulinunua kutoka kwa mtu mmoja aliyemtaja kwa jina la Mangula, hivyo anasubiri tamko la Mahakama ya Ardhi Tanzania ambako shitaka limepelekwa…”????

Kwanza, hakuna mtu anayeitwa “Mangula”. Eneo lilikuwa mali ya kiwanda cha “Mang’ula”, Shirika la Umma lililobinafsishwa! Pia, Mwingira alikuwa anatumia uhusiano wake na Waziri Mkuu Mstaafu, Sumaye, kuwatishia majirani wake wanaofanya shughuli zao kwenye eneo hilo. HUU NI UHUNI MKUBWA!

Mwingira alipeleka maombi ya kununua eneo lote, lakini akakataliwa na PSRC. Akapewa sehemu ya nyuma, lilipo kanisa lake la EPHATA. Ni eneo kubwa. Amekuwa akitumia uwanja wa mbele wa eneo hilo kuwafanyia semina za “brainwashing” vijana wasiokuwa na ajira, ili wawe watumwa wa kumpelekea pesa, kwa mfumo wa kuwalipisha ada za semina mbali mbali za “kiroho”. WIZI TU! Hakuna lolote!

Mwingira akifa leo, kama hao “wachungaji” wenzake, na “kanisa” hilo linakufa pia, kwani hataki mtu mwingine yeyote “ahubiri” madhabahuni kwake. Hafanani kitabia na Kakobe huyu?

Ninachojiuliza, kwa nini Serikali inakaa kimya ilhali ina taarifa zote kuhusu mambo haya? Wakati ule wale wajasiriamali walipoharibiwa mali zao na “tingatinga” na “kijiko” vya Manispaa ya Kinondoni, wakati ule Mkuu wa Wilaya akiwa Kanali Mstaafu Massawe, Kanali aliahidi kushughulikia suala lile ili wale walioharibiwa mali zao wafidiwe. Sijui nini kiliendekea.

Leo hii, “wafuasi” wa Mwingira wanawapiga watu na kuharibu mali za kiwanda. Hapa hakuna kesi ya jinai? Kwa nini Kamanda Kenyela awaite Mwingira na Zain Sharifu na “kuwapatanisha” ilhali Mwingira ameharibu, makusudi, mali za Sharifu? Kuna nini hapa? Kwa nini Mwingira analindwa huku anavunja sheria kwa makusudi kabisa?

Hapa hakuna suala la Kesi iliyopo Mahakamani. Hapa kuna uharibifu wa mali. Kuna watu wamepigwa, wameumizwa. Iweje ACP Kenyela awapatanishe? Hapa hakuna suala la KUPATANA. Mwambieni Zain Sharifu afungue kesi ya msingi, JINAI, dhidi ya Mwingira, kwani huyu SIO NABII WALA MTUME! Ni MWIZI TU!

Nimemaliza!

Che Mchochezi Excellent!


soma ukweli huu upate kuelewa na kuongea ukiwa na data:

EFATHA FOUNDATION LTD
P.O BOX 32174, MWENGE, DAR ES SALAAM
TELEPHONE: +255732993196, FAX:+255732993196
WEBSITE: www.efathafoundation.org
EMAIL: efathafoundationltd@yahoo.com / info@efathafoundation.org
OUR REF: EFL/ADMN/4/2012
DATE:
11th April, 2012

TAARIFA KWA UMMA

1. UMILIKI WA KIWANJA NA. 90, ENEO LA MWENGE (NURU CENTRE)

1.1 Utangulizi

Tarehe 9 mwezi April 2012, Jumatatu ya Pasaka,baadhi ya vyombo vya habari vilitangaza
habari ya umiliki na matukio yaliyotokea katika eneo hilo. Habari zilizotangazwa ni za
upande mmoja na hazina usahihi. Huduma ya Efatha inapenda kuelezea umma taarifa
sahihi juu ya upatikanaji wa kiwanja na 90, umiliki na matukio yaliyotokea katika eneo
hilo.

1.2 Upatikanaji na umiliki wa eneo

Serikali kupitia Tume ya Kurekebisha na Kubinafsisha Mashirika ya Umma (PSRC)
ilitangaza zabuni ya uuzwaji wa eneo la Mang’ula Mechanical and Machine Tools
Company Ltd iliyofilisika, Kiwanja namba 90, Mwenge katika magazeti ya Uhuru na Daily
News ya tarehe 4 mwezi Mei 2005.

Tarehe 18 Mei 2005, huduma ya Efatha kupitia kitengo chake cha uchumi, Efatha
Foundation Ltd, ilipeleka maombi ya zabuni ya kununua eneo hilo PSRC.
Efatha Foundation Ltd ilipokea barua kutoka PSRC yenye kumbukumbu Na.
PSRC/1/13/93 ya tarehe 30 Mei 2005 ikiarifu kwamba zabuni yetu ya kununua eneo hilo
imeshinda kwa kiasi cha shilingi za kitanzania milioni mia nne.

Masharti ya Malipo ya zabuni yalikuwa asilimia kumi ilipwe wakati wa kupeleka maombi
na asilimia tisini ilipwe ndani ya miezi mitatu baada ya kushinda zabuni.

Efatha Foundation Ltd ililipa shilingi milioni arobaini yaani asilimia kumi ya bei siku ya
kupeleka maombi ya zabuni kwa hundi Na. 000261 ya benki ya Azania na kupewa risiti
ya PSRC Na. 6956 ya tarehe 31 Mei 2005. Na shilingi milioni mia tatu sitini ililipwa kupitia
hundi Na. 000319 ya benki ya Azania ambayo ni asilimia tisini tarehe 10 mwezi Juni 2005
na kupewa risiti ya PSRC Namba 6984 na hivyo malipo yote yakawa yamekamilishwa.

Baada ya kukamilisha malipo Efatha Foundation Ltd ilikabidhiwa hati miliki Namba
41641 ambayo ilipelekwa wizara ya Ardhi ili ibadilishwe jina kutoka mmiliki wa mwanzo
na kuandikishwa jina la Efatha Foundation Ltd. Kwa hiyo Serikali ikahamisha umiliki
kutoka Mang’ula Mechanical and Machine Tools Company Ltd iliyofilisika kwenda
Efatha Foundation ltd tarehe 15 Novemba 2005 saa sita kamili mchana kwa uhamisho
Namba 98648.

Kabla ya Huduma ya Efatha kununua eneo hilo kulikuwa na wavamizi ambao ni
makampuni na watu binafsi kumi na moja ambao walikuwa wamewekwa katika eneo
hilo na Mang’ula Mechanical and Machine Tools Company Ltd iliyofilisika bila kibali cha
mfilisi yaani PSRC. Kwa kuwa hawakuwa wapangaji halali walikuwa wavamizi
(trespassers). Wavamizi hao wakapewa notisi ya kuondoka na PSRC lakini
hawakuondoka. Baadae shughuli za mfilisi, PSRC, zikachukuliwa kisheria na Consolidated
Holding Corporation (CHC). CHC nao wakawapa wale wavamizi notisi kuwa waondoke
kwa sababu eneo hilo limeuzwa lakini hawakuondoka. Efatha Foundation Ltd ilipomiliki
eneo hili kihalali na kisheria wakawapa wavamizi notisi ya kuondoka mwaka 2005,
wavamizi nane wakatii amri wakaondoka na wavamizi watatu walikaidi kuondoka
ambao ni pamoja na Afro Plus Industries Ltd.

Baada ya hapo wavamizi watatu waliokataa kuhama wakafungua kesi mahakamani
dhidi ya Efatha Foundation Ltd wakipinga kuhamishwa.

Ni vyema ieleweke kuwa Efatha Foundation Ltd iliponunua eneo hili thamani yake
ilijumuisha majengo yaliyokuwa yamejengwa humo na Mang’ula Mechanical and
Machine Tools Company Ltd iliyofilisika. Hii ni pamoja na jengo alilokuwa anatumia Afro
Plus Industries Ltd ambalo linalalamikiwa kubomolewa na kwamba tumeharibu mali.
Jengo lililobomolewa ni mali ya Efatha Foundation Ltd na siyo mali ya Afro Plus
Industries Ltd kama ilivyodaiwa.

2. UVAMIZI WA POLISI NDANI YA KANISA LA EFATHA MWENGE

Tarehe 9 Aprili 2012, jumatatu ya pasaka, majira ya saa kumi na mbili asubuhi waumini
wa Efatha walikuwa katika ibada ya morning glory katika kanisa la Efatha Mwenge
wakiongozwa katika ibada hiyo na Mchungaji David Mwakisole ndani ya kanisa. Kanisa
limezungushiwa ukuta pande zote nne na lina mageti ya kuingilia kanisani ambayo
yanafungwa. Polisi walipanda ukuta wakachungulia wakasikika wakisema hawa huku
ndani. Baadae polisi wakarukia ndani kupitia ukutani. Wakati ibada inaendelea ghafla
waumini walivamiwa kutoka nje na watu ambao baadae walitambuliwa kuwa ni polisi.
Walipoingia kwa nguvu wakatupa mabomu ya machozi ndani ya kanisa huku wakifyatua
risasi za moto wakati ibada ikiendelea. Kwa kitendo hicho ibada ilivurugika na kusimama
na waumini wakaanza kukimbia ovyo ndani ya kanisa. Risasi na mabomu ya machozi
yalitupwa kuelekea madhabahuni na kuelekea kwa waumini waliokuwa katika ibada.
Waumini wengine waliokuwa wakija kwenye ibada walizuiliwa nje na kukamatwa.
Kilichofuata ni vurugu huku waumini wakikimbia na polisi wakiwapiga kwa virungu,
vitako vya bunduki na mateke. Baadhi ya waumini walijeruhiwa vibaya sehemu
mbalimbali za mwili na ukumbi wa kanisa ulitapakaa damu. Pia polisi walivunja
madirisha, viti, milango na spika kama ilivyoonyeshwa katika baadhi ya vyombo vya
habari hasa ITV. Kabla hawajavamia, mmoja wa askari aliwatahadharisha wenzake kuwa
wasipige mabomu na risasi kwa kuwa hapo ni kanisani lakini wenzake walipinga
wakisema kuwa huyu mtu ana kiburi na watu hawa ni wakorofi. Wakati risasi na
mabomu yakipigwa baadhi ya askari walikuwa wakiokota maganda ya risasi na mabaki
ya mabomu ya machozi ili kuondoa ushahidi. Hata hivyo baadhi ya risasi za moto,
maganda ya risasi za moto na mabaki ya mabomu yalibaki kanisani na yamehifadhiwa
mahali maalum kwa hatua zaidi.

Kanisani kulikuwa na idadi ya waumini kati ya sitini na sabini waliokuwa wanaabudu.
Polisi waliwakamata jumla ya waumini 53 pamoja na wachungaji waliokuwa wakiongoza
ibada wakiwapiga na kuwasweka katika magari ya polisi kuwapeleka kituoni pamoja na
kuvuta gari zilizokuwa zimeegeshwa nje ya kanisa kwa breakdown. Tumepata habari
kuwa walikuja na baadhi ya waandishi wa habari walioandaliwa kabla ili kurekodi tukio
hilo na ushahidi tunao. Kwetu sisi inaonyesha kuwa tukio hilo liliandaliwa kwa makusudi
ili likatekelezwe katika kanisa la Efatha. Tukio hili linatupa hisia kuwa kuna chuki kubwa
kwa Huduma ya Efatha.

Kitendo cha polisi kuvamia na kuvuruga ibada ni kinyume na sheria na katiba ya jamhuri
ya Muungano wa Tanzania iliyoweka uhuru wa kuabudu na sheria za nchi zinazoeleza
kwamba ibada ziheshimiwe na zisiingiliwe. Tunajiuliza kulikuwa na tatizo gani polisi
wasisubiri nje ibada iishe na wawachukue watu wanaotaka kuwachukua. Ndani ya
kanisa hakukuwa na vita, wala mtu mwenye silaha, wala mtu anayeuawa ambaye polisi
walilazimika kwenda kumwokoa. Sisi tunaliona hili kuwa ni kumdharau Mungu,
kuvuruga ibada na kuwadhalilisha waumini wa Efatha waliokuwa wakitumia uhuru wao
wa kuabudu. Leo wamefanya hivyo kwa dharau ndani ya kanisa la Efatha, kesho
tutegemee watakwenda kufanya nini kwa dhehebu jingine, Msikiti, Dini nyingine au
watu waliokusanyika kihalali na kwa sababu halali?

3. MAJUMUISHO

Vielelezo vyote kuhusu umiliki wetu halali wa eneo hili vilishawasilishwa polisi mkoani
na wilayani. Kutokana na maelezo haya Efatha Foundation Ltd inapenda kuuthibitishia
umma kuwa EFATHA FOUNDATION LTD ndiyo mmiliki halali wa KIWANJA NA. 90, ENEO
LA MWENGE (NURU CENTRE) na si vinginevyo.


KATIBU
EFATHA FOUNDATION LTD
 
Ya Kaizari apewe Kaizari na ya Mungu apewe Mungu. Nashauri tusitumie muda kuwajadili viongozi wa dini. Napita tu
 
Nakumbuka, takriban miaka 4 iliyopita, mtu anayejiita Nabii na Mtume, Josephat Mwingira, ambaye aliwahi kutamka kwamba kabla ya “kuokoka” alikuwa jambazi sugu, aliwafanyia unyama wa kutisha wafanyabiashara, wajasiriamali waliokuwa wamejiajiri wenyewe, kwa kuweka vibanda vyao vya biashara, eneo la Mwenge, nje ya eneo lililokuwa la kiwanda cha umma, Mang’ula Plant Works (jina ni langu, lakini “Mang’ula” ni jina rasmi), ambacho kilibinafsishwa chini ya iliyokuwa Parastatal Sector Reform Commission (PSRC), sasa inaitwa Consolidated Holdings Corporation (CHC).

Bila taarifa, Mwingira alikodi magari makubwa mawili ambayo ni mitambo ya kutengeneza barabara, aina ya Caterpillar Grader na Caterpillar Scoop, ambayo yalifanya kazi ya kubomoa vibanda hivyo, jambo ambalo liliwasababishia wafanyabiashara hao hasara kubwa SANA. Wengi walifilisika, walipoteza mali na mitaji yao. Waliowahi kuokoa mali zao, walifanikiwa kuondoka mahali hapo salama. Wengi walibaki kutazama, Grader na Scoop, yakifanya maangamizi hayo, bila ya kuwa na nguvu ya kufanya lolote, kwani siku hiyo kulikuwa na magari mawili ya Polisi, aina ya LandRover Defender Pickup, yakiwa na zaidi ya askari Polisi kumi wenye silaha, wakitokea Kituo cha Polisi OysterBay. Askari hao waliitwa hapo baada ya Mwingira kuwasiliana na Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD), ambaye baada ya “maelewano” yao, askari walitinga hapo, kuhakikisha “usalama” unakuwapo.

Unyama huu wa Mwingira haukuishia hapo. Wamiliki wa viwanda vidogo vilivyo ndani ya eneo hilo la Mang’ula, wanatambua kwamba wao walimilikishwa maeneo yao kihalali na Serikali, kupitia PSRC, baada ya Mang’ula kuvunjwa. Ieleweke kwamba Mang’ula lilikuwa Shirika la Umma, na sio mtu binafsi.

Kwa sasa, Mwingira anaendesha kampeni ili kuhakikisha kwamba anamiliki (kwa njia yoyote ile, kana kwamba HAKUNA SERIKALI ya KUMWAJIBISHA) eneo lote la Mang’ula! Ameanza na kubomoa na kuharibu mali ya kiwanda cha uchapaji cha AfroPlus, ambacho kiko kwenye eneo hilo. Kwa mujibu wa habari zilizochapishwa kwenye gazeti la Uwazi, ninanukuu:
“KIONGOZI wa Kanisa la Efatha, Nabii na Mtume Josephat Mwingira amekamatwa na polisi na kupewa kibano katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Dar es Salaam, akituhumiwa kuharibu mali za mfanyabiashara, Zain Sharifu.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, ACP Charles Kenyela, Mwingira alikamatwa wiki iliyopita na kushikiliwa kituoni hapo.


Hata hivyo, Kenyela alisema, Mwingira alidhamiwa baada ya kuhojiwa kuhusiana na tuhuma za kuvunja na kuharibu mali ndani ya Kiwanda cha Uchapaji cha Afroplus kinachomilikiwa na mlalamikaji.

“Tumemkamata kiongozi huyo ili atoe ufafanuzi wa kina baada ya kupokea malalamiko hayo, “ alisema Kenyela alipozungumza na mwandishi wetu wiki iliyopita ofisini kwake.

Kenyela alisema, mashtaka hayo yalifikishwa polisi na Zain, Januari 8, mwaka huu, akidai kwamba walinzi binafsi wa kiongozi huyo wa kanisa, walivamia kiwandani kwake na kuharibu mali baada ya kufanya fujo.

Aliongeza kuwa polisi baada ya kupata taarifa hizo, walikwenda eneo la tukio kushuhudia na kukuta mali zilizoharibiwa, hivyo walimtaka Mwingira kufika polisi ili atoe ufafanuzi lakini alikaidi ndipo polisi ikatumia nguvu kumkamata.”


Sasa kibano kimegeuka. Kumbe na yeye anaweza kufikishwa Polisi, tena kule kule OysterBay, alikowatumia maafande kuwaharibia mali zao wajasiriamali waliokuwa wakijitafutia riziki zao, tena barabarani, na sio kwenye eneo lake la “kanisa”?

Sasa tujiulize, ni Nabii na Mtume gani ambaye:


  1. Anataka kuwaondoa watu wanaomiliki maeneo yao ya kibiashara, kihalali, tena kwa nguvu, kwa kuwaharibia mali zao ili watishike, kwambe yeye ana NGUVU?
  2. Amekwishawaharibia watu, watafutaji, maskini, mali zao, na wengine kuwafilisi kabisa, chini ya mtutu wa bunduki, eti kwa kuwa alikuwa “anasafisha barabara” ya kuelekea kwenye “kanisa” lake?
  3. Anataka kujilimbikizia mali (Ardhi) bila kufuata sheria?

Ieleweke kwamba, (mosi) eneo ilipojengwa Ephata Bank pale Mwenge ni eneo la hifadhi ya barabara, na ipo siku itakuja kubomolewa na TANROADS, anatapozuka Mkurugenzi Mkuu “kichaa” asiyeogopa mtu, bali anayeheshimu na kufuata/kutekeleza sheria!!!

Mwingira hafanani na huo “utume na unabii” wake, kwani matendo yake yanamhukumu. Wafuasi (sio “waumini”) wake hukesha wakiomba na kufunga, wakimwomba “Mungu” alete maafa kwa watu fulani ambo kwa mujibu wa Mwingira ni “maadui” wake, kwa mfano, Mchungaji Ambilikile Mwaisapila (“Babu”), ambaye “wafuasi” wa Mwingira walikesha na kufunga mwezi mzima, wakiomba mauti yamfikie. Mpaka leo, “Babu” anadunda. Ni “Mungu” gani huyo anayeombwa kuwaua watu wasio na hatia? Iweje, “nabii na mchungaji” atake watu wafe kwa amri yake yeye mwenyewe? Huyo sio “Mungu”, bali ni IBLIS!

Eneo ambalo linasomeka kama EPHATA NURU CENTRE, ambao limejengwa kwa upande wa mbele (mabanda ….) unaopakana na Barabara Mpya ya Bagamoyo, bado linahesabiwa, kisheria, ni mali ya Serikali, kwani, kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo, eneo hilo HALIJABINAFSISHWA kwa mtu, watu au taasisi yoyote ile. Halikadhalika, eneo ambalo kuna viwanda na kampuni kadhaa, kama vile Simon Engineering, Metal Works, imber Malt Tech, Auto Ran Makongo, Container Global, Simon Engineering, Safe Man, Profession Investigation, Elbe Ltd, Zana za Kilimo Mbeya na Kilimanjaro Machine Tools Ltd, ni eneo linalomilikiwa kihalali kabisa, kwa mujibu wa Sheria, na kampuni hizo tajwa. Iweje leo, Mwingira adai kwamba anamiliki eneo lote hilo “tangu Juni 17, 2005, baada ya kulinunua kutoka kwa mtu mmoja aliyemtaja kwa jina la Mangula, hivyo anasubiri tamko la Mahakama ya Ardhi Tanzania ambako shitaka limepelekwa…”????

Kwanza, hakuna mtu anayeitwa “Mangula”. Eneo lilikuwa mali ya kiwanda cha “Mang’ula”, Shirika la Umma lililobinafsishwa! Pia, Mwingira alikuwa anatumia uhusiano wake na Waziri Mkuu Mstaafu, Sumaye, kuwatishia majirani wake wanaofanya shughuli zao kwenye eneo hilo. HUU NI UHUNI MKUBWA!

Mwingira alipeleka maombi ya kununua eneo lote, lakini akakataliwa na PSRC. Akapewa sehemu ya nyuma, lilipo kanisa lake la EPHATA. Ni eneo kubwa. Amekuwa akitumia uwanja wa mbele wa eneo hilo kuwafanyia semina za “brainwashing” vijana wasiokuwa na ajira, ili wawe watumwa wa kumpelekea pesa, kwa mfumo wa kuwalipisha ada za semina mbali mbali za “kiroho”. WIZI TU! Hakuna lolote!

Mwingira akifa leo, kama hao “wachungaji” wenzake, na “kanisa” hilo linakufa pia, kwani hataki mtu mwingine yeyote “ahubiri” madhabahuni kwake. Hafanani kitabia na Kakobe huyu?

Ninachojiuliza, kwa nini Serikali inakaa kimya ilhali ina taarifa zote kuhusu mambo haya? Wakati ule wale wajasiriamali walipoharibiwa mali zao na “tingatinga” na “kijiko” vya Manispaa ya Kinondoni, wakati ule Mkuu wa Wilaya akiwa Kanali Mstaafu Massawe, Kanali aliahidi kushughulikia suala lile ili wale walioharibiwa mali zao wafidiwe. Sijui nini kiliendekea.

Leo hii, “wafuasi” wa Mwingira wanawapiga watu na kuharibu mali za kiwanda. Hapa hakuna kesi ya jinai? Kwa nini Kamanda Kenyela awaite Mwingira na Zain Sharifu na “kuwapatanisha” ilhali Mwingira ameharibu, makusudi, mali za Sharifu? Kuna nini hapa? Kwa nini Mwingira analindwa huku anavunja sheria kwa makusudi kabisa?

Hapa hakuna suala la Kesi iliyopo Mahakamani. Hapa kuna uharibifu wa mali. Kuna watu wamepigwa, wameumizwa. Iweje ACP Kenyela awapatanishe? Hapa hakuna suala la KUPATANA. Mwambieni Zain Sharifu afungue kesi ya msingi, JINAI, dhidi ya Mwingira, kwani huyu SIO NABII WALA MTUME! Ni MWIZI TU!

Nimemaliza!

Che Mchochezi Excellent!
Hio ni chuki juu ya Mwingira.Sisi hatutaki chuki zenu hapa tunataka uthibitisho kwasababu kila mtu anadai anauhalali wa eneo,na yeye kama Mwingira anahaki ya kusimamia haki yake.Kwa hiyo mnachotaka akaye kimya wakati anahaki.Kakobe amewahi wapi kutapeli viwanja?Muache chuki kama humpendi kakobe au mwingira bora uwaache kwasababu wengene tunawapenda na kuwaamini kuliko kutaka kila kitu kuwapakazia
 
Back
Top Bottom