Ukweli kuhusu Pyramids

Ukweli kuhusu Pyramids

Mawazo yako ndiyo matunda ya historia iliyochakachuliwa na maandiko ya kwenye vitabu vya imani.

Jiulize kabla ya imani za kigeni kuja kwetu, inamaana Babu zetu walikuwa wanaruhusu kuua, kuiba, kusema uongo na dhambi zingine zingine? Sio kweli, Babu zetu walikuwa well civilized sema wanaotaka kukutawala kifikra lazima waharibu historia yako nzuri na kukuhadaa na historia mbaya.

Nyie ndio bado mnaamini mlima kilimanjaro umegunduliwa na wazungu.
Umeongea facts tupu.. Shida ni waafrika wengi wamejazwa akili za kizungu kupitia movie
 
Lete vithibitisho kuwa hyo nd haijachakachuliwa? Halafu mtu unacriticise bible imeongea neno gani baya ambalo limeiathiri dunia? Kuwaambia watu wasiibe, wasiue, wasizini, wasiseme uongo, wapendane, wamuabudu Mungu mmoja, waheshimu baba na mama, shika sababato, usiabudu sanamu na mengine mazuri mengi uje uipe dosari kisa tu imesema kuwa pyramids walijenga waisrael chini ya utawala wa misri walipokuwa utumwani. Yani kweli binadamu Mungu atachoma aisee yani sidhani kama kutakuwa na msamaha mwepesi hivi. Halafu unakuja na mipaka waliokuchorea hao hao wazungu unataja nchi ambazo zinapakana na Misri hyo hyo. Je unajuaje kama kabla ya mkutano wa berlin ilkuwa nchi moja? Sorry kama nimeongea kwa uchungu sana na Mungu atusaidie sana tuje tuokoke huko mbinguni.
Biblia imeruhusu utumwa na Pia Quran imeruhusu utumwa.. Hivyo vitabu ni vimejaa uongo
 
Watu ww zamani walikuwa na MAUMBO MAKUBWA.warefu na wenye nguvu .sio kama wa sasa..
Unaambiwa adam alikuwa na urefu wa nguzo mbili za umeme uziunganishe pamoja ndo urefu wake
Watu wa zanani walikua na maumbo madogo mzee baba
 
Hizo pyramid zilijengwa na annunaki
Hao viumbe walikuja duniani yapata miaka 5000 iliyopita na ndio walioleta ustaarabu duniani na kuwafunza binadamu ujuzi wa mambo mbalimbali,
Ukiangalia hayo madude utayakuta Mexico,Egypt, Peru,Indonesia na baadhi ya sehemu,
Hao viumbe walikuja duniani kutafuta madini kama dhahabu ndio maana ukienda Zimbabwe kuna machimbo ya dhahabu ya mwenemutapa ni moja kati ya maeneo ya ajabu sana utajiuliza Yale machimbo enzi hizo walitumia zana gani maana inaonesha ni uchimaji advanced uliofanyika kuliko teknolojia tuliyonayo Leo,

Pia Annunaki walipoondoka duniani kuna jamii nyingi zilianza kuwaabudu kama miungu jua,huko mexico waaztec waliamini ipo siku watakuja kurudi tena na ndio maana wakawa wanatoa sadaka za binadamu walipoona hao viumbe hawarudi maana waliamini kwa kufanya vile hao annunaki watashuka tena toka mawinguni ili wawaletee ujuzi na baraka maana enzi hizo hao viumbe waliposhuka duniani walikuja na vyombo vya anga vya kustaajabisha na zawadi mbalimbali kwa watawala wa enzi hizo,

Pia kuna kabila linaitwa Dogon lipo huko Mali pia nao mbaka Leo wanakiri na wanaamini mababu zao waliwahi tembelewa na viumbe toka sayari ya Nibiru (planet X),
Nawakafundishwa elimu kubwa sababu hao dogon walikua wanajua elimu ya nyota toka kale kuna mpelelezi alifika kwao miaka ya 1600 huko hao watu wa kabila la dogon wakamwambia dunia ni duara na jua letu lina mfumo wa sayari zaidi ya 8
Pia walimwambia kuhusu dunia kujizungusha kwenye muhimili wake,
Kiufupi hao dogon tribe ni moja ya makabila ya kale waliobakia na kumbukumbu zote kuhusu hao viumbe hata wao nyumba zao hujenga kwa mfumo wa pyramid.



Kuna mengi sana nyuma ya haya sema muda ndo hautoshi!
Hayo machimbo huamini kama waafrika waliweza. Unajua wapare walikua wanaujuzi WA stainless steel mjerumani akawaua wahunzi wote
 
Pyramids zimejengwa na Mussa (Moses) na ndugu yake (Haaruni). Hii ni kwa mujibu wa Quran na yalijengwa kwa command maalum (wahyi) kutoka kwake ambapo structure ya ujenzi wake imefanywa kuwezesha watu wa misri wawe wakiswali humo na kuelekea katika true north (Qiblah) kwa wakati huo kabla Qiblah hakijabadilishwa. [We inspired Moses and his brother "Settle your people in Egypt in houses and make your houses (facing the Qiblah."...10.87).

Tafsiri: Na tukampelekea Musa na ndugu yake WAHYI huu: 'Watengenezeeni majumba watu wemu katika Misri na zifanyeni nyumba zenu ndio mwahali mwa ibada...'

Tafsri kwa kiingereza na kiswahili sio nzuri sana kuelezea maana ya aya hii lakini mambo ya msingi ya kuzingatia

1. Ujenzi wa Mapyramid ulifanywa katika kipindi cha Musa na ndugu yake Haaruni kwa amri ya (ya Kihimaya) au WAHYI kutoka kwa Mungu. Hivyo teknolojia yote iliyotumika katika ujenzi wa Pyramids si wa kiuwezo wa kawaida wa kibinaadamu ila ujenzi ulifanywa na binaadamu.
2. Majumba hayo yamejengwa kwa kuyaelekeza Qiblah ya wakati huo (Masjid Aqsa) ambapo Qibla hicho ni true north ya yalipo majumba hayo. Kumbuka Qiblah hapo mwanzo haikuwa Makkah kama ilivyo sasa.
3. Lengo la majumba hayo ni makazi na kuabudia(pamoja na mambo memgine).
Mambo ni mengi ila mida hautoshi lakini kwa ufupi pyramids yamejengwa kwa mfumo huo.
Quran ni kitabu cha uongo tuu.. Kwanzaa hamna record yoyote ya mtu anaitwa musa kwenye historia ya kemet, then kipindi yanajengwa hata yehova hajaongea na Abraham au allah hâta hajakuwepo
 
Quran ni kitabu cha uongo tuu.. Kwanzaa hamna record yoyote ya mtu anaitwa musa kwenye historia ya kemet, then kipindi yanajengwa hata yehova hajaongea na Abraham au allah hâta hajakuwepo
Kwa mtizamo na elimu uliyonayo upo sawa. Kwa elimu niliyonayo mimi, na vitabu mbalimbali nilivyofanikiwa kuvisoma na mpangilio wa hoja maandishi na ujumbe unaotolewa, sina shaka Quran na hata Biblia si vitabu vya uongo. Ni ufunuo kweli kutoka kwa somebody from somewhere with power, knowledge, wisdom and capability beyond human horizon. Ila kuna mfumo wa kihesabu unaotofautisha baina ya hivyo vitabu viwili. Lakini sina hofu na ujumbe unaotolewa.
 
Mi naamini hayo ma-pyramids yamejengwa na wanadamu, tena wanadamu wa kawaida kabisa,

Maana wanefili (majitu) waliangamizwa na waisrael kule caanan, japo zilibakia mbegu chache sana kama yule Goliath mfilisti .


Nani waliojenga na kwanini walijenga?!

Bila shaka pyramids zilijengwa na wamisri (wakale) au waisrael (watumwa wao) kwa kufuatisha elimu na ufundi wa hali ya juu waliokuwa nao enzi hizo!

Walijengaje?!

Mimi naamini sikweli kwamba eti walibeba tofali moja ambalo lina uzito wa tani 2500, bali inawezekana pia hao watu waliojenga enzi hizo walijenga hayo matofali huko huko juu,

Yaani walijenga tofali juu ya tofali lingine wakiyaacha mpaka yakauke, kama vile tunavyojenga linta ya nyumba! Walienda kwa mtindo huo mpaka kumaliza pyramid zima wakifuatisha mahesabu yao na ufundi wao.

Maana tukikazania na kung'ang'ania kwamba eti walibeba tofali la tani 2500 haileti sense, hawakuwa na mitambo (winchi) wala vifaa vya kubebea, wala hawakuwa na nguvu za kuyabeba physical hayo matofali,

Bali kuna uwezekano kuwa yalijengewa huko huko juu kama tunavyojenga linta za nyumba, hilo pia linawezekana, kwanini lisiwezekane??????!!!!!
inasemekana mawe yale hayakuwa ya eneo lile kwa sabab sio eneo la miamba, inaonekana yaliletwa site. Unazungumziaje hilo mkuu
 
Hayo machimbo huamini kama waafrika waliweza. Unajua wapare walikua wanaujuzi WA stainless steel mjerumani akawaua wahunzi wote
mkuu ielewe logic yangu sijakataa kama yalichimbwa na Africans ila namaanisha wakati wa ancient civilization inaanza kuwepo duniani miaka mingi iliyopita hao annunaki ndio waliokuja kufawafundisha binadamu kuhusu ustaarabu yaani binadamu akafundishwa elimu ya nyota,ujenzi,madini,sanaa nk
Kabla ya hao annunaki hawajaja binadamu tulikua primates yaani watu pori tukiishi mapangoni tu hatuna ustaarabu hao viumbe walimbadilisha binadamu na kua classic akaanza kujitambua na ndipo zikazaliwa himaya kubwa kama Assyrian, misri,Aztec, Babylon,Maya,Indonesia na nyingine nyingi na mbaka Leo ukienda huko utaona huo utamaduni na magofu ya kale zaidi yanayofanana maana pyramid hazipo misri tu hata mexico na Indonesia zipo
Pia kuna watafiti walichunguza na kugundua bara la Antarctica lenye barafu Kali nako kuna majengo ya pyramid sasa kwanini hayo madude yafanane kote huko ndo swala la hao annunaki ndio linakuja kua ndo waanzilishi wa ustaarabu duniani hapo kale!
 
inasemekana mawe yale hayakuwa ya eneo lile kwa sabab sio eneo la miamba, inaonekana yaliletwa site. Unazungumziaje hilo mkuu
Hakuna ushaidi kama yaliletwa mkuu, "inasemakana" bado ni dhana tu isiyo na ushaidi wowote mkuu!

Na kama waliyajenga?! Nipe ushaidi au mantiki waliyaletaje hapo hayo mawe yenye tani 2500?! Na waliyatoa wapi?!
 
Back
Top Bottom