Ukweli kuhusu maisha ya ughaibuni

Ukweli kuhusu maisha ya ughaibuni

Huyu ni tapeli lipo humuhumu bongo linajifunza kuuzia watu chai! Ati kawaambia ni under age lakini ana mke na watoto 3. Daah! Kwanza mtu ambaye kampuni inaweza kumpeleka hadi US kwa ajili ya workshop au training ni mtu anayejielewa, composed na atleast senior kwa hiyo hawezi kuzamia hata kidogo. Afterall kama umesoma vizuri kwanini uzamie? Si ufuate utaratibu ukafanye kazi kama expert? Halafu linajisifu ati limepata kazi ya uhotelia. Terrible! Yaani mtu uzamie ughaibuni, uache familia Tanzania halafu unakuwa hotelia huku ukitegemea kutoboa maisha? Ujinga.
Asante sana mkuu. hili suala la kupelekwa workshop USA alafu akazamia nililigusia humu watu wakaona kama vile tunawakatisha tamaa.
 
Nani aishi kwenye nchi inayonunua ndege wakati dawa hospitali hakuna.Na mnatangaza elimu bure wakati Walimu hakuna watoto watajifundisha wenyewe.Usilazimishe nifikirie Kama unavyofikiria wewe.Tanzania hatuna Serikali tuna kikundi cha watu wachache kinachoamua nani atawale kwa maslahi yao.Njoo Canada uone Raia wenye Serikali yao Kiongozi anaheshimu maamuzi ya Wananchi na havunji Katiba.Watu wanakosa maji Safi na Salama pesa inanunuliwa ndege.Tufike Mahala Watanzania tujitoe Muhanga ili kuokoa Kizazi chetu kinachofata

Sent using Jamii Forums mobile app
Umemwacha mke wako huku watu wanamkula umejiona mjanja. yaani nilikudharau pale upoamua kuzamia ukiwa na zaidi ya M7. Kwanza sijaaamini maana chai ni nyingi sana kwenye huu uzi.
 
[/QUOTE]
Habari za leo Wana JF,Natumai mko poa sana na wale ambao hawako vizuri kwa namna moja au nyingine namuomba mwenyezimungu awaondoe katika hali hiyo na awapeleke katika hali nzuri zaidi ili waweze kuendelea na mapambano ya maisha ya kila siku.Nichukue nafasi hii kipekee kabisa kuweza kumshukuru mwenyezimungu,Mwenyezimungu ambae anatupenda sana sisi Wanaadamu na ametuumba umbile zuri kuliko kiumbe mwingine yeyote yule na ametufanya kuwa na akili ya kufikiria na kuamua na kuchagua kile ambacho tunakitaka hivyo hatuna budi kumshukuru.Ntakuwa mchoyo wa Fadhila kama sitawashukuru wana JF ambao wamesoma na kucoment hadithi yangu ya ukweli na sio ya kutunga hivyo nawashukuru sana.

Inaendelea...........

Baada ya kuvuka ile border ya USA na Canada nilikutana na polisi na bila ya kunihoji walinipiga Pingu jambo ambalo lilinishitua sana na moyo wangu ukaanza kwenda mbio nikaona sasa nimejiingiza kwenye matatizo maana sikuambiwa kuwa ntapigwa Pingu niliambiwa ntasaidiwa tu.Nikasachiwa mwili mzima then nikapelekwa kwenye kituo cha polisi,Nilipofika mule ndani nikafunguliwa pingu kisha kikafunguliwa chumba kidogo sana ambacho kilikuwa na Choo chake nikaingizwa ndani kisha nikaambiwa na Polisi wawili wa CANADA nivue nguo zangu zote hivyo kubaki uchi kama nilivyozaliwa kisha wakanifungia mlango wakaondoka.Walipoondoka nikaanza kukiangalia kile chumba huku nikiwa na wasiwasi mkubwa na mawazo nikaona heater na Camera nne nikawasha heater maana kulikuwa na baridi kiukweli nilikuwa katika wakati mgumu sana nilikumbuka nyumbani hasa mama yangu,Watoto wangu,mke wangu na ndugu zangu nikaanza kutokwa na machozi nikikumbuka nilivyosoma kwa shida na kupata kazi na nikawa namudu maisha yangu na kusaidia ndugu zangu nikajiona katika watu wapumbavu mimi ni mpumbavu kwelikweli.Chumba hakikuwa hata na kigodoro hivyo sikuweza kulala Usiku mzima.
Ilipofika asubuhi majira ya saa tatu mlango ukafunguliwa na Polisi wawili wakafungua mlango kisha wakaingia ndani ya chumba changu wakanipa nguo zangu na kisha wakaniambia niwafuate.Tukaingia chumba kingine mulemule ndani nikakutana na Afisa mwengine wa Polisi akaniuliza kwa ukali "Why did you cross the border Illegally?" Nikamwambia kuwa mimi ni mkimbizi kutoka Somalia nimeletwa na Agent Marekani na amenipokea mtu ambae amenileta mpaka hapa akaniambia nivuke ntasaidiwa hivyo wakaniuliza tangu naianza hii Safari nimetokea wapi na nimepita wapi mpaka nimefika hapa,Waliniuliza maswali mengi sana ambayo sitaweza kuyaandika yote humu Pia waliniuliza kwanini nisiombe Asylum USA nikawaambia kuwa nimeambiwa USA hawapokei wakimbizi na uzuri nilishapangwa cha kusema hivyo nilikuwa naigiza vilevile nilivyofundishwa kujibu na wakati wananiuliza walikuwa wanaandika kwenye computer walipomaliza tu wakatoa Karatasi ambayo ilikuwa inaonesha maswali niliyoulizwa na nilichojibu kisha nikaambiwa nitie Signature yangu.

Baada ya hapo nikaambiwa niwafuate Polisi wale wawili walionitoa mule chumbani kisha tukatoka nje nikaambiwa nipande gari hivyo nikaingia kwenye gari ikiwa na Polisi wengine wapya watatu .Gari ikaanza mwendo ambapo nakumbuka ilituchukua masaa matatu mpaka Kufika mji mkubwa kidogo nakumbuka unaitwa Québec ambapo mji huo wanazungumza Sana Lugha ya Kifaransa.Nilipofika Quebec nikapelekwa sehemu kwenye mjengo mkubwa Sana ulivyo kama Hotel nikakabidhiwa kwa Ofisa mmoja mwanamke na akapewa karatasi zangu huku akiaambiwa kwa Kifaransa kisha wakaniaga wale walionileta wakaniambia wananitakia kila la kheri
Mwanamke huyo akaniuliza Je nkilichoandikwa kwenye zile karatasi ni kweli au uongo nikajibu ni kweli,Akatoka akaniletea kitambulisho kinachoonesha kuwa mimi Mkimbizi kutoka Somalia kisha ikapigwa simu kwa Security wakanipeleka sehemu humohumo ndani nikapewa Lotions,Sabuni za kuogea,Shuka na Blanket kisha nikapelekwa kwenye chumba ambacho kilikuwa na watu wawili tu ila kilikuwa ni chumba kidogo ambacho kilikuwa na vitanda vya Double decker viwili yaani kitanda kimoja mmoja analala juu na mwingine chini kwahiyo chumba kimoja hulala watu wanne japo nilikuta watu wawili tu ila ikiwa mtu na mkewe wanapewa chumba kimoja peke yao na kitanda kikubwa.Nilikaa pale mwezi mmoja huku nikapata breakfast na lunch na dinner kwenye Kantini kubwa iliyokuwa na watu wengi Sana ikiwa wengi wao ni Waarabu wa Syria,Yemen na Afghanistan pia kulikuwa na Wasomali wengi na Watanzania ambao wengi walikuwa Wazanzibari na Kutoka Dar ilikuwa nipo peke yangu ila hawakunibagua.
Niliiishi pale kwa miezi miwili huku nikiutembea mji maana tulipewa ticket za bure kwa mwezi mzima na ikiisha muda unapewa nyingine na tulikuwa tunalipwa kwa mwezi pesa kidogo bila ya kufanya kazi.Kwa kweli nilipata marafiki wengi wa Kizanzibar pale kambini na kupeana hope kuwa tutashinda kesi na kupata Papers za kuishi na kukubalika kisheria.Na tulipeana Technic nyingi za kushinda case maana kuna Wazanzibari walijiripua kuwa ni Wasomali na walipoulizwa kwenye Interview ya kesi zao walisema kuwa Walitoa rushwa ili wapate Passport za Tanzania na wengine walisema wao ni mashoga kwahiyo jamii zao zimewatenga na wanataka kuuliwa maana jambo hilo halikubaliki kisheria kwetu na wengine walisema wao ni Wanasiasa hivyo Serikali inawaua na kuwapoteza na wengine walisema kuwa ni Waandishi wa habari na vyeti feki wametengeneza vya Uandishi wa habari kwa kweli Wazanzibari uzamiaji upo kwenye Damu.
Baada ya mwezi mmoja niliitwa kwenye Interview yangu ya kwanza ya kuhojiwa kilichonikimbiza Somalia na nikienda nikahojiwa kwa muda wa masaa 6 na maswali niliyoulizwa ni mengi sana..........
ITAENDELEA................
Ntataja maswali yote niliyoulizwa kwasababu dhamira yangu sio kuwafundisha watu kuzamia ila wayajue maisha halisi ya kuzamia ili mtu akiamua kuja ajue nini kitakachotokea hivyo Kujiandaa kisaikolojia mapema

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nimefuatilia toka episode ya kwanza. Baada ya kusoma hii na kabla ya kuanza episode ya tatu nina maswali mawili.
Hivi uliwapa passport yako polisi wa canada au uliachana nayo US kabla ya kuvuka boda?

Halafu hao polisi wa canada kukufungia na kukuacha uchi usiku mzima si udhalilishaji huo? Ni kwa nini walifanya hivi? Sikutegemea kama nchi kama canada inayoheshimu haki za binadam ingeweza kufanya hivi!!!

Nakupongeza kwa ujasiri!!!
 
Mkuu nimefuatilia toka episode ya kwanza. Baada ya kusoma hii na kabla ya kuanza episode ya tatu nina maswali mawili.
Hivi uliwapa passport yako polisi wa canada au uliachana nayo US kabla ya kuvuka boda?

Halafu hao polisi wa canada kukufungia na kukuacha uchi usiku mzima si udhalilishaji huo? Ni kwa nini walifanya hivi? Sikutegemea kama nchi kama canada inayoheshimu haki za binadam ingeweza kufanya hivi!!!

Nakupongeza kwa ujasiri!!!
[/QUOTE]
Hapo kama hauna afya nzuri muda huo wote lazima utaimba tu kikwenu. So kuachwa usiku ni kipimo cha kiafya yako kijeshi. Usiogope huko huko kwa mama yako.Uko kwa wanaume lazima uendeshwe kiume mkuu.
 
Hongera kwa kujilipua...

Omba Mungu tu waliokupeleka US kwenye mkutano wasipite hapa halafu wakaenda kukuchomea ubalozi wa US...

Kingine jiepushe na matumizi ya mitandao na kujiexpose kama hivi, dakika sifuri tu utapata hizi habari unaandika humu zipo kwenye jalada lako ofisi za uhamiaji ya huko...

Otherwise wakihakiki wewe ni Msomli basi jua ndio umeula hivyo hata wanao utaweza wasogeza huko

Yaani hata mimi kuna wakati nikisoma anachosema namuamini na kuna wakati simuamini!!! hasa hasa ukija kwenye uwezo wake wa kufanya maamuzi. Najiuliza ni kwanini katoa hii story kabla ya kupata papers na ku settle?

Maana huku JF ni kichaka cha wengi wakiwemo watu wa balozi mbali mbali. Balozi wana maofisa wa kuchimba habari mbali mbali zenye maslahi kwa nchi yao. Sasa watu wa ubalozi wa canada/US dar wakifuatilia huu uzi si unaweza kumharibia yeye na hao wazanzibari?

Hata hivyo nakutakia heri mpambanaji, kama kweli story yote ya kweli....
 
Mkuu nimefuatilia toka episode ya kwanza. Baada ya kusoma hii na kabla ya kuanza episode ya tatu nina maswali mawili.
Hivi uliwapa passport yako polisi wa canada au uliachana nayo US kabla ya kuvuka boda?

Halafu hao polisi wa canada kukufungia na kukuacha uchi usiku mzima si udhalilishaji huo? Ni kwa nini walifanya hivi? Sikutegemea kama nchi kama canada inayoheshimu haki za binadam ingeweza kufanya hivi!!!

Nakupongeza kwa ujasiri!!!
Hapo kama hauna afya nzuri muda huo wote lazima utaimba tu kikwenu. So kuachwa usiku ni kipimo cha kiafya yako kijeshi. Usiogope huko huko kwa mama yako.Uko kwa wanaume lazima uendeshwe kiume mkuu.
[/QUOTE]
Aisee....
 
Mkuu mzamiaji A3M we endelea kutuporomoshea ma-experience! Huku bongo maisha ni magumu asikwambie mtu, impact yake inaonekana katika fikra za wachangiaji ...too negative kwenye kila jambo! Wanaodai ni uongo wanataka kutuambia kuwa mzamiaji wetu anatumia movie fulani na google map kutueleza hii story?!

Na je mbona mara kadhaa amekataa kuwa yeye hana msaada wa maana kwa anayetaka kufuata nyayo zake! Vinginevyo tungedhani anajitengenezea mazingira ya kutupiga pesa. Naamini sehemu chache anazotufunga kamba ni pale anapohisi akiweka ukweli atajulikana, hiyo si mbaya!

Kikubwa ni watanzania tukubali kuwa bado idadi ya wenye uthubutu kwenda kusaka maisha nje ni ndogo mno, tumebanana hapa kutwa kusuguana na Jiwe, kila mtu mwanasiasa, wanasiasa wenyewe hawana jibu muafaka la kuyaboresha maisha yetu... So akijitokeza mwenzetu akapenya bourders atupe picha nasi twende tu kama wanigeria, wakenya, waganda...

Kama west africans wanajazana kwenye mitumbwi kuvuka bahari despite the death risk wakielekea ughaibuni, it's obvious huko kuna asali na maziwa ukilinganisha na maisha ya hapa nyumbani ya kufight ili kupata nyumba, gari na kusomesha watoto baasi! Bongo hamna kitu, chenga tu!! Bro A3M komaa sana huko and never regret for leaving back the family, God will bless you with time utakuwa nao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu kama ninyi huwa hamkosekani duniani hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
No tunakustua tu na tushayaona,sasa hivi ndo ilikua kipindi cha kupiga kimya kuhusu kilichotokea,mambo ya interview migration mwana ni siri yako tu.hamna cha kuwaambia room mate wako au yoyote,piga kimya na kuuliza ushauri mdogo mdogo si mbaya.

kuhusu kuchomana imo nisikudanganye mambo hayo wengi wamekutana nayo huko immigration na hao hao wakalimani ndio wakitoka wanaenda kuya expose mtaani kwa marafiki zao.
 
Mkuu mzamiaji A3M we endelea kutuporomoshea ma-experience! Huku bongo maisha ni magumu asikwambie mtu, impact yake inaonekana katika fikra za wachangiaji ...too negative kwenye kila jambo! Wanaodai ni uongo wanataka kutuambia kuwa mzamiaji wetu anatumia movie fulani na google map kutueleza hii story?!

Na je mbona mara kadhaa amekataa kuwa yeye hana msaada wa maana kwa anayetaka kufuata nyayo zake! Vinginevyo tungedhani anajitengenezea mazingira ya kutupiga pesa. Naamini sehemu chache anazotufunga kamba ni pale anapohisi akiweka ukweli atajulikana, hiyo si mbaya!

Kikubwa ni watanzania tukubali kuwa bado idadi ya wenye uthubutu kwenda kusaka maisha nje ni ndogo mno, tumebanana hapa kutwa kusuguana na Jiwe, kila mtu mwanasiasa, wanasiasa wenyewe hawana jibu muafaka la kuyaboresha maisha yetu... So akijitokeza mwenzetu akapenya bourders atupe picha nasi twende tu kama wanigeria, wakenya, waganda...

Kama west africans wanajazana kwenye mitumbwi kuvuka bahari despite the death risk wakielekea ughaibuni, it's obvious huko kuna asali na maziwa ukilinganisha na maisha ya hapa nyumbani ya kufight ili kupata nyumba, gari na kusomesha watoto baasi! Bongo hamna kitu, chenga tu!! Bro A3M komaa sana huko and never regret for leaving back the family, God will bless you with time utakuwa nao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante mkuu,tatizo watu hawayajui haya mambo ya Kuzamia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu wewe muongo sana
Mkuu acha kupotosha watu
Mkuu nilikuambia wewe muongo
Mkuu tabia ya kufanganya watu sio nzuri
Mkuu malengo yako toka post ya kwanza nikikuambia


Nasisitiza acha kudanganya watu
Huu uongo wako sio mzuri,kuna seheme mbili umeongea uongo.
 
Habari za humu wa wadau wa JF,

Nichukue nafasi hii kumshukuru mwenyezi mungu kwa neema na baraka nyingi ambazo ametupa na kikubwa zaidi ni afya njema na maarifa mazuri aliyoturuzuku. Lakini pia nitakuwa mchoyo wa fadhila iwapo sitawashukuru Great thinkers wote wa JF ambao walitoa mawazo yao juu ya Mpango wangu wa kuzamia Nchini Marekani mara baada ya kupata Visa ya nchi hiyo.

Nafahamu wapo watu ambao walitamani sana kujua nini kilichojiri baada ya mimi kufika USA na kilichoendelea baada ya kuzamia huku Ughaibuni. Niwakumbushe tu kidogo kuwa nilisafiri tarehe 15 August mwaka huu 2019 kwaajili ya kuhudhuria mkutano ambao ulifanyika na nilihudhuria Nchini Marekani katika mji wa Washington DC ambapo ilinichukua siku 3 kukamilisha kile nilichotumwa na ofisi yangu kukikamilisha.

Nakumbuka watu wengi wa JF walinipa ushauri baada ya kumaliza mkutano nirudi Bongo kwa sababu sina pa kuanzia Marekani ila kwangu mimi hiyo haikuwa sababu ya kunizuia nisizamie Marekani.Kiukweli Marekani ni kuzuri mno japokuwa sijawahi kwenda nchi yeyote hiyo ndio Mara yangu ya kwanza tangu nizaliwe ila sidhani kama kuna nchi nzuri kuliko Marekani hapa duniani,Ni kuzuri nashindwa hata kuelezea kwa kweli.

Mara baada ya kutuma ile Post hapa jukwaani kuna jamaa alinitafuta Private kabla ya kuruka akanipa mchongo akaniambia hapo Marekani hapafai akasema atanipa njia niende Canada ila nikifika nijiripue kama mkimbizi wa Kisomali ndivyo Wazanzibari wengi hufanya hivyo na alinitumia Makaratasi ya Somalia niyasome ili niijue vizuri Somalia kuna maeneo Somalia wanaongea kiswahili.

Nilipomtumia picha yangu akasema nafanana sana na Msomali hivyo nikifika Marekani nimtafute ataniunganisha na mtu nitakayemlipa anivushe upande wa pili yaani Nchini CANADA. Kwa kweli nilikuwa naogopa sana na niliogopa isije ikawa anataka kunipoteza ila nilikuwa na moyo wa ujasiri na nilishachunguza kuwa watu wengi wanatoka Marekani na kuingia Canada kupitia Illegal borders.hivyo nilijipa moyo na kusema ntaweza.

Hivyo nilipomaliza mkutano nikawasiliana na jamaa mvushaji akasema niende New York atakuja kunipokea Airport,kwasababu nilikuwa na Pocket money ya kutosha nilijiamini sana.Baada ya kufika akanipeleka hoteli fulani akasema atakuja kesho asubuhi, Ilipofika majira ya saa 4 asubuhi akafika akiwa yeye na mwenzake ambae alikuwa ni Mmexico na huyo alienipokea alikuwa ni Mzanzibari.

Kwa hiyo tukapanda bus mpaka sehemu ambapo tulishuka na tukachukua Taxi tukawa tunaenda nikaona msitu tu nilipouliza akaniambia kuwa huku sasa ndio tunaelekea CANADA nikashangaa sana tuliposimama sehemu tukashuka na kukutana na watu watano na wale wawili wakawa saba wakaniambia niwape hela tuliyokubaliana yaani Dollar 3000 ikabidi niwape then tukaendelea na safari nikiwa nahofia kuwa nisije nikawa naenda kuchinjwa na kutolewa viungo vya mwili wangu maana hakuna ninaemjua pale na hata huyo Connector wangu nilikuwa simjui ila ilikuwa balaa la hofu limetanda naona sifiki.

Hatimaye nilifika sehemu nikaoneshwa bendera ya Canada na kuambiwa nenda pale na waeleze kuwa wewe ni mkimbizi kutoka Somalia utasaidiwa.Nikaenda na nikavuka mpaka nilipofika nikapigwa pingu palepale kwa kosa la kuvuka kinyume na utaratibu.

Itaendelea...

Nitawaeleza siku nyingine baada ya Pale ila kwasasa nipo Canada.

Sent using Jamii Forums mobile app
@client3

Hiii hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu wewe muongo sana
Mkuu acha kupotosha watu
Mkuu nilikuambia wewe muongo
Mkuu tabia ya kufanganya watu sio nzuri
Mkuu malengo yako toka post ya kwanza nikikuambia


Nasisitiza acha kudanganya watu
Huu uongo wako sio mzuri,kuna seheme mbili umeongea uongo.
Zitaje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daby Mrs Bishanga canada haina sheria ngumu za uhamiaji kama ilivyo USA Na Australia . pia ni nchi ambayo inahamasisha watu wenye ujuzi mbali mbali kuhamia huko kufanya kazi zipo nyingi watu wanahitajika kwa wingi ,hivyo wana program mbali mbali kwa ajili ya watu wanaopenda kwenda kuishi Canada ,hapa chini ni baadhi ya program ambazo unaweza ku apply na kupata kibali cha kuishi huko ,

Express Entry is an electronic management application system for immigration to Canada. It facilitates the selection and processing of Canada’s economic immigration programs:
- Federal Skilled Worker Program,
- Federal Skilled Trades Program,
- Canadian Experience Class,
- Provincial Nominee Program

Ingia google na uchimbe mwenyewe kujua ni namna gani uta apply na njia ipi inaweza kukufaa zaidi wewe,lakini endapo una ndugu au jamaa anaishi Canada basi inakuwa rahisi zaidi kupata kibali,google pia kama una ndugu unafata process gani ktk izo program za ku apply
Bila "connection" kutoboa ni mtihani.
 
Back
Top Bottom