Ukweli kuhusu maisha ya ughaibuni

Ukweli kuhusu maisha ya ughaibuni

Ukiwa na fingerprint ya Kwa Mnyamwezi ukiingia Canada kuomba ukimbizi lazima wataviona na watajua kuwa umetokea bongo,kwahiyo almost haiwezekani kujipiga kusonjo(kisomali)Unless uwe na plan B,

Sent using Jamii Forums mobile app
Unamaanisha fingerprints za NIDA na UHAMIAJI zinasoma hadi Canada?

Tupe shule kidogo sisi wa St. Kayumba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe umewahi kufika hata Nairobi tu??? Yaani unafananisha maisha ya Toronto na kwenu Shinyanga? Una akili kweli wewe?

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe itakuwa ni choko, mimi nimeanza kusafiri 1995 nimezunguka Europe nchi kibao,,Canada nimeishi sana,nilikuwa namwelesha huyu jamaa asifikiri maisha ya Canada ni rahisi kama wengi walivyokariri,
 
Umeenda mbele kutafuta maisha/hela au umeenda kutaka kua huru kama wazungu?

Ukitaka kua huru bora ubaki tu huku Igunga boss.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sikwenda kwa ajili ya kutafuta lolote mkuu, nilienda kwa kazi yangu maalumu .... Nilitumwa na nchi yangu.. pesa haziji ghafla hivo japo mpaka uwe na moyo sana na subra ni miaka karibuni kumi na ndo una make unachotaka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lililopo ni kwamba hakuna guarantee ya moja kwa moja kama angebaki akaizungusha hiyo pesa angefanikiwa.

Na pia sio kwamba mbele nako kurahisi kivileee. Ila mimi mtu akiniambia bongo maisha ya utafutaji marahisi kuliko Canada nitabisha maana tumezaliwa Bongo tunaijua vizuri...
Bongo lazima ufanywe fulsa kwnza uhujumiwe na wabongo wenzio kwqnzia unao wajua na usiowajua .Bongo kugumu sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: A3M
Pole kwa changamoto ulizopitia, lakini kwa wenye elimu na ujuzi kuna njia halali za kuhamia kama skilled labour.
Mkuu hukuletewa mzungumzaji wa kisomali kukuhoji? Wengi wanaojisingizia usomali hukwama kwenye lugha.
 
Sikuletewa mkuu kwasababu maeneo niliyotaja ya Somalia hawaongei Kisomali wanaongea kibajuni na kibajuni kinafanana sana na kiswahili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumbe njaa zenu ndizo zinaichafua nchi yetu,kisa tu mupate kibali cha kuishi Kanada.
Nani aishi kwenye nchi inayonunua ndege wakati dawa hospitali hakuna.Na mnatangaza elimu bure wakati Walimu hakuna watoto watajifundisha wenyewe.Usilazimishe nifikirie Kama unavyofikiria wewe.Tanzania hatuna Serikali tuna kikundi cha watu wachache kinachoamua nani atawale kwa maslahi yao.Njoo Canada uone Raia wenye Serikali yao Kiongozi anaheshimu maamuzi ya Wananchi na havunji Katiba.Watu wanakosa maji Safi na Salama pesa inanunuliwa ndege.Tufike Mahala Watanzania tujitoe Muhanga ili kuokoa Kizazi chetu kinachofata

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Iko hivi,unapoingia marekani ukuwa kwenye system za nchi ya marekani.unapokuwa unasafiri popote marekani wanajua kuwa hyu mtu iko wapi na watakutafutia watu.mfano umeenda marekani kwasababu ya shule,ukikarbia kumalzia shule wanaanza kukutumia barua za visa yako kwisha muda wake.na wanajua watakupata wapi maana marekani umeingia una wenyeji wako.kama umepewa siku tatu na ziwe siku tatu unapozidisha wanaanza kufatia kwa wenyej wako na wenyej wako wasipojua ulipo iyo ni kesi kwao.

Ndo umefanikiwa kuingia nchini marekani kwenda canada huwezi kuvuka border ya marekani kuingia canada bila vitambulisho vinavyokutambulisha wewe ni nani na unaenda canada kufanya nini.wanapokuingiza kwenye system zao wanajua kabisa wazi kuwa wewe ni mgeni ulikuja kwa visa ya kutembea hiyo ni kesi nyngine na huwez kuruhusiwa kuingia canada kamwe.


Acha kudanganya watu mkuu,marekani kwenda state nyingine tu lazima uwe na vitambulisha sembuse kuvuka border ya nchi kuingia lazma wawe na taarifa zao na kutoka lazima wapata taarifa zako

Kwaiyo marekani haiwezi kukuruhusu kuvuka border kuingia canada kama wewe uko umekuka marekani kwa njia na vikao mkuu.

Mimi niko marekani,nimeenda canada mara nyingi na nimetembea marekani sehemu nyingi na utaratbu huu wa kusafr naufahamu vizuri sana.

NB:hakuna mkimbizi nchini canada kutokea mpaka wa marekani na sheria ya canada na marekani hairuhusu ukimbiz wa mipakani.

Na kama utakataa nitakuzibishia kwa vitendo.

Na wanaoruhusiwa kuvuka mpaka wa marekani bila ukaguzi ni raia wa marekani ambao wana pasport na ukitoka kuingia canada wanajua kuwa kuna raia wetu ipo kama na hata gari uliotumia utatambulika.hata namba za gari tu wanatambua kuwa gari hii imeshaingia nchi canada au kifika kwenye mipaka ya nchi fulani

Na kama na hili unabisha nitadhibitiha hapa

Marekani kila ktu kipo kwenye system unapofinga tu tayar unashikwa.
Mkuu Kama kitu hukielewi Bora unyamaze sikatai kwamba Marekani Wana System nakubaliana na wewe ila nataka nikwambie ukitaka kuvuka kihalali ni lazima uoneshe Passport ikiwa ni Mgeni ila ukiwa Mmarekani unachohitaji ni kitambulisho tu kuingia Canada lakini wazamiaji wote hupita border za panya ambapo hakuna kizuizi chochote cha kukuzuia usivuke kuelekea Canada kwa njia za Panya offcourse ukiingia utakamatwa tu kwasababu ni kosa kisheria lakini hawajadhibiti kwa kujenga ukuta kama ilivyo Mexico na USA.Canada ni rahisi kuingia kutokea Marekani yaani unanibishia mimi ambae nipo Canada na nimevuka Illegally.Na nimeongea na wengi tu hapa wanaeleza kuwa waliomba Visa za Canada wakakosa wakaamua kuomba ya Marekani wakapata kwahiyo wakaingia Canada Illegally na wapo hapa Kambini.Acha ujuaji mambo ya Kibaharia tuachie wenyewe wewe huna unachokijua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nani aishi kwenye nchi inayonunua ndege wakati dawa hospitali hakuna.Na mnatangaza elimu bure wakati Walimu hakuna watoto watajifundisha wenyewe.Usilazimishe nifikirie Kama unavyofikiria wewe.Tanzania hatuna Serikali tuna kikundi cha watu wachache kinachoamua nani atawale kwa maslahi yao.Njoo Canada uone Raia wenye Serikali yao Kiongozi anaheshimu maamuzi ya Wananchi na havunji Katiba.Watu wanakosa maji Safi na Salama pesa inanunuliwa ndege.Tufike Mahala Watanzania tujitoe Muhanga ili kuokoa Kizazi chetu kinachofata

Sent using Jamii Forums mobile app
kwa hiyo hayo yote yatabadilika kwa kila Mtanzania kukimbilia nje kuomba ukimbizi?
 
Back
Top Bottom