Ukweli kuhusu ATCL Boeing 787-8

Ethiopian Airline na Air Austral yalichukua ndege hizi kwa sababu masafa marefu haikuwa ishu kwao!
Unaa uhakika na ulichokisema? Majawabu ya namna hii hutolewa huko vijiweni, umelipata huko? Na ukitaka kuelewa juzi juzi nimepanda ET Dreamliner 787-8 kutoka Sao Paulo (Brazil) nonstop (masaa 14 angani) hadi Addis. Kama jambo hulijui tumia muda kujifunza jambo/suala husika badala ya kukimbilia ku-comment.
 
Jiulize ni kwanini serikali iko kimya kuhusu tuhuma hizi ndio utapata jibu.
Hapa hakuna tuhuma yoyote ndugu; kuna spin doctors na wajinga wana-buzi-buzi. Labda kwa kuwa spin doctor master amezungumza suala hili Bungeni, hivyo serikali kulazimika kulizungumzia wakati wa ku-windup budget speech, vinginevyo serikali ingewapuuzia mbali stories za spin doctors na wajinga fulani.
 
Embu nifupishie kuwa nani ameitumia hiyo ndege na ilitumika kwa muda gani? Na pia hizo tarehe zote vipengele kwa kifupi vinaashiria nini hadi Dec 2016. macho yananiuma nimeshindwa kusoma yote vizuri.
Ndege haijatumika mkuu IPO tu uwanjani.. Hizo ni tarehe za Kutengenezwa, Matengenezo, na Makampuni yalio jaribu kuinunua
 
Naona 0019 Ethiopian airlines waeioder kwa maana hiyo nao wameamua kuchukua hiyo terribe teens,je wao wamenunu kwa USD ngapi je ni USD 99 au? Wamepigwa kama sisi
Ethiopian airlines wamenunua hizo ndege kwa nusu... Taarifa zote zipo kwenye mtandao Mkuu.
 
Mkuu hebu nijuze hapa kwanza.

Hizo ndege unazosema ziliwadadea mpaka wakafanya punguzo ndo zikauzwa je Bado zipo hadi leo au zilikwisha?????

Kama bado zipo kwanini ndege yetu mpaka Leo bado IPO kiwandani haijakamilika kutengenezwa?????

Kulikuwa na ulazima gani wa kututengenezea ndege mpya wakati bado wanazo za aina hiyo hiyo???

Kama ziliisha, inamaana bado wanarudia tena kutengeneza ndege kwa mfumo ule ule ambao ndege zinadoda???

(Watakuwa wapumbavu wa karne wakifanya hivi)
 
Sidhani kama ni jambo la kuficha Boeing wameweka wazi wanaziuza kwa bei chee anayetaka aje,

Na uzuri listi ya ndege zao zilizo nunuliwa iko wazi kwa kila mtu.

Na kwa kuwa listi zao wanaweka Serial number na Line number kwa niyo kila mtu anajua unandege ya namna gani.

Uzuri biashara ya ndege haina mambo Ya kuficha ficha.
 

Hebu tuachane nao hawa mkuu
Naona wanang'ang'ania mambo ya kipumbavu hapa.
 


Mkuu UKWELI NI HUU: lazima Una vyeti original........ LAZIMA.
 
Ethiopian Airline na Air Austral yalichukua ndege hizi kwa sababu masafa marefu haikuwa ishu kwao!
Kwani Tanzania itapiga masafa mafupi? Kama hiyo ndege imekaa store ikidoda mbona rais kasema tunaisubiri inatengenezwa kwanini tusiichukue right away wakati pesa zipo?
 
Mkuu labda tujue Ethiopia pia wamenunua kiasia ngani
 
Kwa Ethiopia kununua huo mtumba kwa kwa bei ya juu siyo rahisi watakuwa wameokota kwa 99 m$
Tatizo ninyi akina Mmawia mnapenda ku-draw conclusions, kwa masuala yanayohitaji technical knowhow, kwa kutumia general knowledge. Unatakiwa kufahamu kuwa kampuni ya Boeing ina strict business code ili kulinda integrity ya kampuni na biashara ya bidhaa zake (ndege). Sasa kama Boeing wameandika kwenye tovuti yao kuwa bei ya ndege yao B.787-8 ni US$224.6 milioni, sasa wewe ni nani kusema kuwa bei halisi/halai ni US$99 milioni? Hiyo bei imeandikwa wapi? Ni wapi ET walitangaza kuwa wamenunua Dreamliner kwa hizo dola milioni 99? Si watanzania wote ni wajinga/watu wa aina yenu.
 
Rudi post #1, percent kubwa ya maswali yako yamejibiwa
 
SABABU YA KULETA UZI HUU SIO KULETA MALUMBANO WALA KUKASHIFU JUHUDI ZA SERIKALI

HOJA YANGU YA MSINGI KAMA NDEGE TUNAYO ITEGEMEA NI MPYA NA SI ZILE ZA ZAMANI

KWANINI KWENYE WEB YA BOEING WAMEONESHA TUME WEKA ODA NDEGE YENYE SERIAL NUMBER 35508 LINE PRODUCTION 19 YA MWAKA 2009?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…