MNYAMA WA 666/
PEMBE NDOGO:
MNYAMA = Ufalme, Serikali, Nguvu ya kisiasa
(utawala) - Daniali 7:23
PEMBE = Mfalme au Ufalme - Danieli 7:24; 8:5, 21,
22; Zekaria 1:18, 19; Ufunuo 17:12
“MNYAMA“ na "PEMBE NDOGO"
1) “Pembe ndogo" ana “macho ya mwanadamu."
Danieli 7:8.
... “Mnyama" ana “hesabu ya kibinadamu." Ufunuo
13:18.
2) “Pembe ndogo" “anawadhoofisha watakatifu
wake Aliye juu." Danieli 7:35.
... “Mnyama" pia “anafanya vita na watakatifu."
Ufunuo 13:7.
3) “Pembe ndogo" hunena " maneno makuu
kinyume chake Aliye juu." Danieli 7:25.
... “Mnyama" pia “Akafunua kinywa chake
amtukane Mungu." Ufunuo 13:6.
4) “Pembe ndogo" aliibuka kati ya pembe kumi
(Majimbo 10 ya Rumi.) Danieli 7:8.
... “Mnyama“ akapokea “nguvu, kiti cha enzi, na
uwezo mwingi" kutoka Rumi
... (baada ya kuundwa kwa majimbo 10). Ufunuo
13:2.
SIFA ZA MNYAMA WA 666/ PEMBE NDOGO:
Zipo sifa nyingi za kumtambulisha, hebu na
tuangalie baadhi ya sifa hizo:
1. Aliibuka kutoka kwa mnyama wa nne (Danieli
7:7,8)
2. Aliibuka kati ya pembe kumi (Danieli 7:8)
3. Aliibuka baada ya pembe kumi (Danieli 7:24)
4. Alikuwa tofauti/mbali na wale wa kwanza (Dan.
7:24)
5. Alikuwa hodari kuliko wenzake (Danieli 7:20)
6. Aliangusha falme tatu (Danieli 7:8,20).
Heruli A.D.493, Vandals A.D.534 na Ostrogoths
A.D. 538.
7. Alikuwa na macho kama ya mwanadamu na
alinena maneno makuu kinyume chake Aliye juu
(Danieli 7:8,25; Ufunuo 13:5).
“Papa si mwakilishi tu wa Kristo Yesu, bali ni Yesu
Kristo aliyefichwa ndani ya vazi la mwili.” The
Catholic National, Julai, 1895.
Hapa duniani tunashikilia pahali pa Mungu Aliye
Juu (Nafasi ya Mungu Mwenyezi). Papa Leo XIII,
Encyclopedia, Juni 20, 1894).
Lakini Petro akamuinua, akasema, Simama, mimi
nami ni mwanadamu; Matendo 10:25,26.
Anayestahili kupigiwa magoti (kusujudiwa) ni
Mungu pekee wala siyo mwanadamu. Soma pia
Ufunuo 19:10.
Luka 5:21; 1Timotheo 2:5
8. Kuwadhoofisha watakatifu (Danieli 7:25; Ufunuo
13:7)
Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao
wazishikao amri za Mungu, na imani ya YESU.
Ufunuo 14:12
Upapa uliwatesa na kuwaangamiza wale wote
waliokuwa kinyume nao, historia iko wazi kabisa
juu ya hili na hata Papa Yohana Paulo II aliwahi
kuomba msamaha kwa niaba ya kanisa la Rumi
(Katoliki) kwa mauaji na mateso yaliyofanywa na
kanisa.
9. Kubadili majira na sheria (Danieli 7:25)
“Jumapili ni amri ya Kikatoliki, na uabuduaji wake
waweza kuhifadhiwa tu chini ya misingi ya
kikatoliki…. toka mwanzo hadi mwisho wa
maandiko hapana kurasa hata moja inayoidhinisha
badiliko hili la ibada ya kila juma toka siku ya
mwisho kwenda ya kwanza.” Chapa ya Katolika
Sydney, Australia, Agosti 1900.
“Kanisa Katoliki linadai kwamba badiliko
walilifanya wao….na badiliko hilo ni alama ya
madaraka yake ya kanisa na mamlaka waliyo nayo
katika masuala ya kidini.” Letter, Oct. 28, 1895,
from C. F. Thomas
“Jumapili ni alama yetu ya madaraka…. Kanisa liko
juu ya Biblia, na huku kuhamishwa kwa utunzaji
wa Sabato ni kizibiti cha ukweli huo.” Catholic
Record, September 1, 1923.
“Papa ana mamlaka ya kubadilisha nyakati,
kubadili sheria, na kutupilia mbali vitu vyote, hata
mafundisho ya Kristo.” Decretal De Translat.
Espiscop. Cap.
“The Pope can modify divine law.” Prompta
Bibliotheca, Papa, art. 2.
Amebadili amri kumi za MUNGU – Amri ya pili
imetolewa na amri ya kumi imegawanywa ili
kutimiza idadi.
“Labda jambo la kijasiri la mabadiliko yaliyofanywa
na kanisa yalitokea katika karne ya kwanza. Siku
takatifu, Sabato, zilibadilishwa kutoka jumamosi
kwenda jumapili….sio kwa maagizo yoyote
yaliyoandikwa katika Biblia, lakini kwa kanisa
kujisikia lina mamlaka…. watu wanaofikiri kwamba
Biblia ndiyo mamlaka ya pekee, inabidi wawe Wa
Sabato, watunze Jumamosi.” Saint Catherine
Catholic Church, Sentinel, May 21, 1995.
10. Alitawala kwa wakati, nyakati mbili na nusu
wakati, au miezi 42 (Danieli 7:25; Ufunuo 13:5).
Upapa ulipata nguvu nyingi sana mwaka A.D
538-1798, uliwatesa na kuwaangamiza wale wote
waliokuwa kinyume nao.
“Vigilus…alikuwa Papa mwaka 538 BK chini ya
ulinzi wa majeshi ya Belisarius.” History of the
Christian Church, vol. 3, p.271
Miaka 1260: 538 BK 1798 BK
Kanuni ya siku = mwaka (Kiunabii) soma Ezra 4:6;
Hesabu 14:34; Ezekieli 4:6.
11. Alipata jeraha la mauti na jeraha la mauti
likapona (Ufunuo 13:3)
“Berthier entered Rome on the Tenth of February,
1798, and proclaimed a republic…. the Pope and
the Papacy was dead.” The Modern Papacy, Rev.
Joseph Rickaby. S.J… p. 1, Catholic Truth Society,
London
“Katika mwaka wa 1798 yeye (Berthier)…aliingia
Roma, AKAFUTA SERIKALI YA PAPA akasimamisha
utawala usio wa kidini.” The Encyclopedia
Americana, 1941 edition
POPE PIUS VI
Pontificated:
- 15 February 1775 – 29 August 1799
Died on 29th August, 1799
Condemned the French Revolution and was
expelled from the Papal States by French troops
from 1798 until his death.
Upapa ulirejeshewa mamlaka yake uliyokuwa
umenyang’anywa (10.02.1798), baada ya
kusainiwa mkataba wa Lateran (The Lateran
Treaty) uliosainiwa tarehe 11.02.1929 kati ya
PIETRO Cardinal GASPARRI [Kwa niaba ya Papa
PIUS XI (Papa PIUS Undecimus)] na BENITO
MUSSOLINI. Ingia kwenye mtandao utaupata huo
mkataba.
12. Jina lake huleta hesabu ya 666 (Ufunuo 13:18)
“What are the letters inscribed in the pope’s crown,
and what do they signify if anything?”
“The letters inscribed in the Pope’s mitre are these:
VICARIUS FILII DEI, which is the Latin for Vicar of
the Son of God.” Our Sunday Visitor, April 18, 1915
V . . 5 F . . 0 D . . 500
I . . 1 I . . 1 E . . 0
C . . 100 L . . 50 I . . 1
A . . 0 I . . 1
R . . 0 I . . 1 TOTAL 501
I . . 1
U . . 5 TOTAL 53
S . . 0
TOTAL 112
GRAND TOTAL 112 + 53+ 501 = 666
13. Yeye ni mama wa makahaba (Ufunuo 17:5 )
Woman, Pure - True Church - Jeremiah 6:2; 2
Corinthians 11:2; Ephesians 5:23-27
Woman, Corrupt - Apostate church - Ezk.
16:15-58; 23:2-21; Hos. 2:5; 3:1; Rev. 14:4
Ukahaba unaosemwa hapa ni ukahaba wa kiroho,
yaani kutofuata maagizo na mafundisho ya Kristo
aliye kichwa cha kanisa (mwanamke).
Kanisa Mama: “Lakini kwa vile Jumamosi, si
Jumapili, ndiyo imetamkwa katika Biblia, ni jambo
la kujiuliza kwamba ambao si wakatoliki
wanaosema wanachukua dini yao moja kwa moja
ndani ya Biblia na sio kutoka kwa kanisa
wanaitunza Jumapili badala ya Jumamosi? Ndiyo
kwa kweli kuna utata, lakini mabadiliko yalifanywa
karne ya 15 kabla uprotestanti haujazaliwa….
Wameendelea kutunza desturi hata kama ni juu ya
mamlaka ya kanisa katoliki na siyo katika Biblia.
Kule kutunza Jumapili kunabaki kukumbushia
kanisa Mama ambalo makanisa yasiyo ya kikatoliki
yalitoka – kama mvulana anayekimbia kutoka kwa
mama yake lakini bado mfukoni ana picha ya
mama yake au kifungio cha nywele zake.” The
Faith of Millions, Rev. John O’Brian, pp. 421,422
14. Ambaye wafalme wa nchi wamezini naye, nao
wakaao juu ya nchi wamelevywa kwa mvinyo wa
uasherati wake (Ufunuo 17:2 )
Ufunuo 17:18
Mvinyo wa uasherati – mafundisho ya uongo
yaliyo kinyume na mafundisho ya Kristo, Matendo
20:28-30; Warumi 16:17-20