Uko wapi Udikteta wa Rais Magufuli?

Uko wapi Udikteta wa Rais Magufuli?

Agizo la serikali kuzuia mikutano na maandamano ya kisiasa ni la kidikteta, linakandamiza haki yao ya kikatiba ya kufanya shughuli za kisiasa, na hawahitaji ruhusa ya Rais katika utekelezaji wa shughuli zao za kisiasa.
 
Unajitekenya huku unacheka..katiba inatoa Uhuru wa kutoa mawazo(freedom of expression) na association pia,yeye anakataza mikutano na maandamano huku akiwa wakwanza kuifanya tena kwa kuwaponda wapinzan..wajinga kama weww ndio wanaoamin hamna udikteta.

Kwahiyo watu milioni 20 (idadi ya watu wazima kuanzia miaka 18 kwa mfano) wakiamua kuandamana watu fulani ambao wao wanawaona ni wachawi/wazinzi wapigwe mawe mpaka kufa ili hao waishi kwa raha katiba inawaruhusu kufanya hivyo kwakua ni demokrasia siyo na wengi wape? Wala Mh. Rais hana chakufanya ni kutoa tu polisi wakasaidie hao "raia wema" waendelee na mchakato wao!

Demcracy has a context.....hakuna democracy inayopingana na uongozi wa kidemocracy....tumeambiwa Taifa letu linahitajika watu wake wafanye kazi na tuachr kutumia raia kwa shughuli zisizo na tija kama maandamano yasiyo na context....kesho mwingine ataitisha maandamano ya kiduku kechokutwa ya khanga mtondogoo ya injili siku nyingine ya kalumanzila; sasa hiyo democracy ya jinsi hiyo wapendwa tutaimaliza lini tuanze kazi?

Tusitafute ligi zisizo na marefa wala vikombe bila sababu....kutii ni bora kuliko sadaka na kiburi si maungwana!
 
Fred,

Uthabiti wa dikteta uchwara kwenye kupambana na ufisadi uko wapi? Yeye mwenyewe fisadi unategemea fisadi apambane na wale wanaokula naye sahani moja.

Yeye ndiyo mnunuzi wa MV uozo kwa shilingi bilioni ambalo sasa liko juu ya mawe. Lugumi kwa kuwa kachukua bulungutu "mchango wa kampeni" anaiogpa hata kuitaja na anaendelea kuikingoa kifua. Escrow, IPTL, wakwa[uzi wa mashirika ya umma wakiwemo akina Salma na Ridhwani Kikwete anawaogopa baada ya kuipora UDA mchana kweupe.

Uthabiti unaouzungumzia hapa ni upi huo? Kumbuka rushwa ya Escrow iligawiwa mpaka Bungeni na Ikulu umemsikia kasema lolote kuhusu hao wapokea rushwa!?

Wacha kuandika pumba eti, "Rais Magufuli amekuwa na msimamo Mkali dhidi ya Ufisadi, wakwepa kodi, ubadhirifu kwenye serikali na halmadhauri na mashirika ya umma." Yeye fisadi kanunua boti la uuzo kwa bilioni nane, Lugumi kachota bilioni 34, Ridhwan na Salma Kikwete wamekwapua UDA, IPTL, Escrow etc huo msimamo mkali dhidi ya ufisadi hawa hauwahusu!?

Wacha kuja hapa na kutufanya Watanzania ni wapumbavu kiasi hicho cha kujua ukweli kuhusu huyu fisadi, dikteta uchwara, mkurupukaji wa mwendo kasi na Rais hewa.
3. Madai Kwamba anawagandamiza baadhi ya watanzania, ni jambo la kushangaza. Tukumbuke wakati WA sakata la EPA, Chadema walipiga kelele sana wakati JK alipowaomba wezi WA fedha za EPA wazirudishe. Wakasema anaongea na wezi. Rais Magufuli amechukua msimamo tofauti, amekuwa dhabiti. Sasa Chadema wanadai dikteta. Hapana.

4. Rais Magufuli amekuwa na msimamo Mkali dhidi ya Ufisadi, wakwepa kodi, ubadhirifu kwenye serikali na halmadhauri na mashirika ya umma. Anapigania utajiri WA Nchi Yetu uwanufaishe watanzania wote. Ukweli Rais Magufuli ni Jibu Kwa maombi ya watanzania wengi kutokana na hali ilivyokuwa imefika.

4. Upinzani wanachokifanya ni kutaka kuwapotodha watanzania ili waichukie serikali yao. Upotodhaji lengo ni uchochezi.

Watanzania tumuunge Mkono Rais Magufuli.
 
1.Kuudhibiti ufisadi
2.Kuasisi mmahakamaya mmafisadi.
3.Kudhibiti MMatumizi.
4.Kusimamia nidhamu ya utumishi wa umma.
5.Kufufua ATC,TRL,Meli....Nk
6.Kuimarisha huduma za afya,elimu nk.
7.Kuongeza mapato ya serikali nk..
Acha ushabiki wewe, Elimu imeimarika wapi wakati Elimu bure hata mitihani ya mock kwa sasa hakuna, Afya imeimarika wapi wakati Hospitalin hakuna chanjo, madawa hakuna, au we unaishi nje ya Tanzania
 
Njaa mbaya sana, kama mtu mzee kama wewe unajidhalilisha kiasi hiki, basi kazi ipo! Nime-kuignore to the maximum! Fred Mpendazoe
Njaa ilianza na Chadema. Kumkubali Lowasa katika genge Lao.. Mtu waliomsema miaka zaidi 8 kua ni fisadi na kusema wana ushahidi
 
Lkn...ni kweli mikutano imekatazwa?
...mbona tunapata taarifa mikutano inayoendelea?
...hata sasa CUF wako kwenye mikutano yao mchakato wa kujichagulia viongozi wa vyama vyao....CDM na CCM pia tumepata taarifa za mikutano yao!
.....lazima tujielimishe, tukishafundishwa, ili tuijue kweli na tusimame nayo!
Unataka kusema mikutano ya tarehe 1 September imeruhusiwa au hiyo siyo mikutano?
 
Ile makala yako ya Lowassa tusamehe ungali unaiamini?

Hahahah ajizi ni nyumba ya njaa!!!

Utadhalilika sana mbele ya watoto wako.
Mkuu hebu ishee hapa basi hiyo Makala
 
Waliwahadaa watanzania kuwa Lowassa ni fisadi toka 2007 pale Mwembeyanga leo hii wanatuambia eti walitumia report ya Mwakyembe ambayo ilitoka 2008,huu si upumbavu?

Leo hii wameanza tena kutuimbia ngonjera nyingine kwamba Magufuli dikteta kama walivyofanya kwa Lowassa.

Huwezi kuwapumbaza watu wote kwa muda wote.

Dikteta gani hatujasikia hata mkosoaji mmoja wa serikali yake kaokotwa bila kichwa?

Leo hii watu mnaharisha tu mnavyojisikia sababu mnajua mtapelekwa mahakamani,hebu nendeni hata Bunjumbura tu hapo mkaulize waandishi wangapi wameokotwa mizoga ndani ya mwezi huu.

Nashagaa Ndugai naye analeta habari ya maridhiano huko bungeni.

I've never seen people negotiating with hooligans!!
 
Unauhakika kuhamia Dodoma kumepitishwa na cabinet au bunge? Ulirudia kusoma na kutafakari ulichoandika? Kama hujafanya hivyo rudia sasa, unahisi uliyemsemea au mwakilisha atafurahia hoja ulizozitoa? Kuna wakati unawezawakilishwa na mtu ukajilaumu heri usingewakilishwa!
 
1. Serikali ya Rais Magufuli imechaguliwa na watanzania kikatiba katika Uchaguzi mkuu 2015.

Naona niongelee hii moja kwa ufupi, Mwaka 1936 wananchi wa ujerumani walimchagua Hitler ambaye alikuja kuiharibu kabisa ujerumani. hivyo kuchaguliwa siyo hoja ya kumzuia mtu kuwa dikteta.kaka mpendazoe uwe mkweli kuzuia mikutano ya siasa kwa kisingizio cha kazi tu, ni sawa kweli? mazuri anayofanya Rais siyo bonus niwajibu wake kama Rais,mikutano ya kisiasa ipo kikatiba na yeye aliapa kuilinda,kama anawashauri halafu hawamwambii hili naona wanajua anataka kushauliwa vipi.j2 njema.
 
1.Kuudhibiti ufisadi
2.Kuasisi mmahakamaya mmafisadi.
3.Kudhibiti MMatumizi.
4.Kusimamia nidhamu ya utumishi wa umma.
5.Kufufua ATC,TRL,Meli....Nk
6.Kuimarisha huduma za afya,elimu nk.
7.Kuongeza mapato ya serikali nk..

Nani aliviua hivyo vyote? kwanini alieviua asipelekwe mahakamani? coz wakati nyerere anaondoka alituachia hivi vitu vyote vikiwa parfect
 
Yetu macho tunanasubiri hiyo tarehe moja mtakavyoparuana. Siasa ni mchezo mchafu leo hii Chadema wanapigania demokrasia! wakati wa uchaguzi wa Mwenyekiti hawakuruhusu mgombea mwingine zaidi yake mbaya zaidi jina la mgombea uraisi halikupitia mchakato wowote wa uchaguzi. Mwanzo walituaminisha kuwa wanapambana na ufisadi leo hii wanawatetea wanaotumbuliwa kutokana na ufisadi. Tuwaeleweje nyinyi wanaasiasa wanafiki? niliwaamini sana mwanzo kwa kutetea masilahi ya nchi leo hii kiko wapi! bora tarehe moja ifike mapema mpate kichapo sawasawa sitawahurumia mmetusaliti wananchi tuliowapigania usiku na mchana.
 
Bora tuendelee na huyu mnayemwita dikteta anayeyepigania masilahi ya nchi kuliko nyinyi wanafiki uchwara.
 
Hii nchi itakuja kupata maendeleo ya kweli pindi wazee kama wewe/ wanafki kama wewe/ wasiojielewa kama wewe... Pindi mtakapokufa na kizazi cha rika lenu kufutika nchi itarndelea kwa spidi ya ajabu.
 
.
....masikini Mpendazoe kapotea maboya kadanganyika, wanamsifu machoni huku wakimcheka moyoni. Wanampa moyo ashughulikie usajili, awe ndio msemaji na wao wako nyuma yake, kumbe moyoni wanajua fika hawajiunga nae, time will tell, na Mpendazoe atakapo ujua ukweli, atauweka bayana, by that time wenzake watakuwa wamerejea bungeni kwa tiketi za chama kile kile, huku yeye akiend-up with frustrations na kuishia kurejea CCM kwa aibu.
Hii ni post no .130, Jun 7, 2010
ukipata muda tembelea mitaa hizi
CCJ yazidi kukomba... usajili wa kudumu wanukia! | Page 2 ...
Swali Kuhusu Kulamba Matapishi: Kwanini Iwe ni Kinyaa Wakati ...

CC.
Fred Mpendazoe
Pasco
 
Vyama vinavyounda UKAWA vimetangaza kufanya maandamano yenye lengo la kupinga udikteta, UKUTA. Maana yake ni Kwamba serikali ya Rais Magufuli in ya kidikteta.

Niwakumbushe UKAWA yafuatayo:
1. Serikali ya Rais Magufuli imechaguliwa na watanzania kikatiba katika Uchaguzi mkuu 2015.

2. Kulingana na katiba, Rais hushauliwa na Baraza la mawaziri. Na pia Rais hushauriwa na Chama chake. Hivyo, Rais Magufuli anafanya maamuzi Kwa kushauriwa na taasisi hizi. Hivyo madai Kwamba anaamua bila kushauriwa hayana mashiko.

3. Madai Kwamba anawagandamiza baadhi ya watanzania, ni jambo la kushangaza. Tukumbuke wakati WA sakata la EPA, Chadema walipiga kelele sana wakati JK alipowaomba wezi WA fedha za EPA wazirudishe. Wakasema anaongea na wezi. Rais Magufuli amechukua msimamo tofauti, amekuwa dhabiti. Sasa Chadema wanadai dikteta. Hapana.

4. Rais Magufuli amekuwa na msimamo Mkali dhidi ya Ufisadi, wakwepa kodi, ubadhirifu kwenye serikali na halmadhauri na mashirika ya umma. Anapigania utajiri WA Nchi Yetu uwanufaishe watanzania wote. Ukweli Rais Magufuli ni Jibu Kwa maombi ya watanzania wengi kutokana na hali ilivyokuwa imefika.

4. Upinzani wanachokifanya ni kutaka kuwapotodha watanzania ili waichukie serikali yao. Upotodhaji lengo ni uchochezi.

Ukowapi udikteta wa Rais Magufuli?, lakini uchochezi wa UKAWA in dhahiri.
UKAWA wanadai demokrasia inaminywa. Tukumbuke, mgombea UKAWA alivyopatikana. Ilikuwa ndani ya chopa na watu wachache siyo kwenye vikao. Hapakuwa na mchakato ulio wazi. Ikowapi demokrasia kwenye UKAWA ?

Pia tukumbuke, walimtuhumuLowassa Kwa muda mrefu kuwa no fisadi na wakawaeleza watanzania kuwa wanao udhahidi. Ghafla wakaamua awe mgombea urais. Uko wapi Uzalendo WA kweli ndani ya UKAWA ?

Watanzania tumuunge Mkono Rais Magufuli.
Hii ni sawa na vita ya Sadam wa Iraq na USA, Askari wake baada ya kushindwa kupambana msituni walivua mavazi ya kivita wakabaki kuwa Raia wapambanaji,
Niliwahi kusema kushindwa kwa Mh Lowasa na watu wake kuingia IKURU hii vita bado ni kubwa, ona sasa anapigana akiwa kavua gwanda.
Sijaona kiukweli UKAWA wanataka nini, kikubwa ilikuwa kutoa muda kwa aliyepo madarakani.
 
Back
Top Bottom