Uko wapi Udikteta wa Rais Magufuli?

Uko wapi Udikteta wa Rais Magufuli?

Vyama vinavyounda UKAWA vimetangaza kufanya maandamano yenye lengo la kupinga udikteta, UKUTA. Maana yake ni Kwamba serikali ya Rais Magufuli in ya kidikteta.

Niwakumbushe UKAWA yafuatayo:

1. Serikali ya Rais Magufuli imechaguliwa na watanzania kikatiba katika Uchaguzi mkuu 2015.

2. Kulingana na katiba, Rais hushauliwa na Baraza la mawaziri. Na pia Rais hushauriwa na Chama chake. Hivyo, Rais Magufuli anafanya maamuzi Kwa kushauriwa na taasisi hizi. Hivyo madai Kwamba anaamua bila kushauriwa hayana mashiko.

3. Madai Kwamba anawagandamiza baadhi ya watanzania, ni jambo la kushangaza. Tukumbuke wakati WA sakata la EPA, Chadema walipiga kelele sana wakati JK alipowaomba wezi WA fedha za EPA wazirudishe. Wakasema anaongea na wezi. Rais Magufuli amechukua msimamo tofauti, amekuwa dhabiti. Sasa Chadema wanadai dikteta. Hapana.

4. Rais Magufuli amekuwa na msimamo Mkali dhidi ya Ufisadi, wakwepa kodi, ubadhirifu kwenye serikali na halmadhauri na mashirika ya umma. Anapigania utajiri WA Nchi Yetu uwanufaishe watanzania wote. Ukweli Rais Magufuli ni Jibu Kwa maombi ya watanzania wengi kutokana na hali ilivyokuwa imefika.

4. Upinzani wanachokifanya ni kutaka kuwapotodha watanzania ili waichukie serikali yao. Upotodhaji lengo ni uchochezi.

Ukowapi udikteta wa Rais Magufuli? Lakini uchochezi wa UKAWA in dhahiri. UKAWA wanadai demokrasia inaminywa. Tukumbuke, mgombea UKAWA alivyopatikana. Ilikuwa ndani ya chopa na watu wachache siyo kwenye vikao. Hapakuwa na mchakato ulio wazi. Iko wapi demokrasia kwenye UKAWA ?

Pia tukumbuke, walimtuhumu Lowassa Kwa muda mrefu kuwa ni fisadi na wakawaeleza watanzania kuwa wanao ushahidi. Ghafla wakaamua awe mgombea urais. Uko wapi Uzalendo WA kweli ndani ya UKAWA ?

Watanzania tumuunge Mkono Rais Magufuli.
Ni kwenye katiba tu mkuu hapo ndo tatizo..... Na katiba ndo inatuongoza
 
Kwa sasa mapema sana kumpongeza na kumuunga mkono. mpaka sasa hakuna alichofanya kwa ufanisi zaid ya kufanya trial and error.
 
Mfano huu utasaidia sana kueleza hali iliyopo kati wanavyoona UKAWA na hali halisi:

One day a school teacher wrote on the board the following:
9×1=7
9×2=18
9×3=27
9×4=36
9×5=45
9×6=54
9×7=63
9×8=72
9×9=81
9×10=90
When she was done, she looked to the students and they were all laughing at her, because of the first equation which was wrong, and then the teacher said the following,
"I wrote that first one wrong on purpose, because I wanted you to learn something important. This was for you to know how the world out there will treat you. You can see that I wrote RIGHT 9 times, but none of you congratulated me for it; you all laughed and criticized me because of one wrong thing I did. So this is the lesson...:
'The world will never appreciate the good you do a million times, but will criticize the one wrong thing you do... But don't get discouraged, ALWAYS RISE ABOVE ALL THE LAUGHTER AND CRITICISM. STAY STRONG.' "

Hata kwa wana Ukawa, JPM kafanya mambo mengi mema. Lakini wanang'ang'ana na vitu vidogo dogo tu.
UKAWA Toeni Boliti Kwenye Macho yenu hakika mtaona vizuri na mtamuunga mkono JPM.
Fredy Mpendazoe, hata mimi nimeanza kukudharau japo sina tabia ya kumdharau binadamu mwenzangu. Rais Magufuli kutoa maagizo yanayovunja Katiba na Sheria za Nchi unaliona ni jambo dogo!! Hivi umeitafakari hotuba ya Baba wa Taifa kuhusu nyufa tatu kuu katika Taifa letu mwaka 1995? Moja ya nyufa hizo kwa mujibu wa Katiba ilikuwa kutojali katiba ya nchi hasa katika maamuzi ya serikali ya Rais Mwinyi kujiunga na OIC ambalo ni shirika la kidini kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Mwalimu alifika mbali zaidi hadi kusema kuwa Rais asiyeheshimu Katiba ya nchi hata kwa jambo dogo tu 'hatufai'. Mahali pake ni kukaribishwa kwenye chai ikiwa tunampenda sana na si Ikulu. Kumbuka ndugu Fredy, mate yasikudondoke kwenye UDC tu uksahau haya.
 
Vyama vinavyounda UKAWA vimetangaza kufanya maandamano yenye lengo la kupinga udikteta, UKUTA. Maana yake ni Kwamba serikali ya Rais Magufuli in ya kidikteta.

Niwakumbushe UKAWA yafuatayo:

1. Serikali ya Rais Magufuli imechaguliwa na watanzania kikatiba katika Uchaguzi mkuu 2015.

2. Kulingana na katiba, Rais hushauliwa na Baraza la mawaziri. Na pia Rais hushauriwa na Chama chake. Hivyo, Rais Magufuli anafanya maamuzi Kwa kushauriwa na taasisi hizi. Hivyo madai Kwamba anaamua bila kushauriwa hayana mashiko.

3. Madai Kwamba anawagandamiza baadhi ya watanzania, ni jambo la kushangaza. Tukumbuke wakati WA sakata la EPA, Chadema walipiga kelele sana wakati JK alipowaomba wezi WA fedha za EPA wazirudishe. Wakasema anaongea na wezi. Rais Magufuli amechukua msimamo tofauti, amekuwa dhabiti. Sasa Chadema wanadai dikteta. Hapana.

4. Rais Magufuli amekuwa na msimamo Mkali dhidi ya Ufisadi, wakwepa kodi, ubadhirifu kwenye serikali na halmadhauri na mashirika ya umma. Anapigania utajiri WA Nchi Yetu uwanufaishe watanzania wote. Ukweli Rais Magufuli ni Jibu Kwa maombi ya watanzania wengi kutokana na hali ilivyokuwa imefika.

4. Upinzani wanachokifanya ni kutaka kuwapotodha watanzania ili waichukie serikali yao. Upotodhaji lengo ni uchochezi.

Ukowapi udikteta wa Rais Magufuli? Lakini uchochezi wa UKAWA in dhahiri. UKAWA wanadai demokrasia inaminywa. Tukumbuke, mgombea UKAWA alivyopatikana. Ilikuwa ndani ya chopa na watu wachache siyo kwenye vikao. Hapakuwa na mchakato ulio wazi. Iko wapi demokrasia kwenye UKAWA ?

Pia tukumbuke, walimtuhumu Lowassa Kwa muda mrefu kuwa ni fisadi na wakawaeleza watanzania kuwa wanao ushahidi. Ghafla wakaamua awe mgombea urais. Uko wapi Uzalendo WA kweli ndani ya UKAWA ?

Watanzania tumuunge Mkono Rais Magufuli.
Wapo pia waliopata kuhoji: Uko wapi udikteta wa Idi Amini? Wapo waliopata kuhoji uko wapi udikteta wa Adolf Hitler? Upo wapi udikteta wa Marcias Francois Nguema? Uko wapi udikteta wa Muammar Ghaddafi?(Huyu hata mtawala wetu huwa anahoji)...lakini tunasumbuka nini?We know for certain that every devil on earth has got his/her own ardent worshippers!
 
Vyeo vya kuteuliwa vinatufanya tuwe vipofu wa yanayoendelea katika nchi hii.
Nadhani Sanduku la kupigia KURA 2015,lilikuwa na siri Nzito,kutokana na nguvu kubwa inayotumika kuwanyamazisha upinzani hata kama wanahoja yenye tija kwa Taifa letu.
 
Ile makala yako ya "Lowassa tusamehe" ungali unaiamini?

Hahahah ajizi ni nyumba ya njaa!!!

Utadhalilika sana mbele ya watoto wako.

Kama ile makala ilivyo kituko,
Kuna zile kauli za mwenyekiti wa ukuta, TL, kubenea, Msigwa, Mnyika na wengineo jus to mention a few...
Hivi nazo bado wanaziamini??
Well nasubiri watu wakapimwe akili kwanza alafu ndio nikomenti..( in Msigwa's voice)
 
Fredy Mpendazoe, hata mimi nimeanza kukudharau japo sina tabia ya kumdharau binadamu mwenzangu. Rais Magufuli kutoa maagizo yanayovunja Katiba na Sheria za Nchi unaliona ni jambo dogo!! Hivi umeitafakari hotuba ya Baba wa Taifa kuhusu nyufa tatu kuu katika Taifa letu mwaka 1995? Moja ya nyufa hizo kwa mujibu wa Katiba ilikuwa kutojali katiba ya nchi hasa katika maamuzi ya serikali ya Rais Mwinyi kujiunga na OIC ambalo ni shirika la kidini kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Mwalimu alifika mbali zaidi hadi kusema kuwa Rais asiyeheshimu Katiba ya nchi hata kwa jambo dogo tu 'hatufai'. Mahali pake ni kukaribishwa kwenye chai ikiwa tunampenda sana na si Ikulu. Kumbuka ndugu Fredy, mate yasikudondoke kwenye UDC tu uksahau haya.
Hakuna kiongozi yoyote iwe wa siasa au dini anayeeleza kama jambo hilo lipo kisheria .
Kila mmoja anakuja na hoja zake kutaka kubadili hoja

Hoja ya mikutano haiuhusiana kabisa na suala la ufisadi.
Mikutano ipo kwa mujibu wa sharia zote ndani ya katiba.
Tena wamezianisha kupitia sharia ya msajili wa vyama na hata jeshi la Polisi

Akina Mpendazoe hawaelezi chanzo cha tatizo, wanajitokeza kuzungumzia eti kuchaonganisha wananchi na serikali yao.

Wanadhani Watanzania ni wajinga wasioweza kuchambua mchele na pumba

Wananchi wanapoipenda serikali yao kama alivyoanza Magufuli hakuna mwanasiasa aliyesimama katika jukwaa kuwashawishi. Waliona hatua na kupendezwa nazo.

Vivyo hivyo, inapotokea kinyume wananchi hawafundishwi, wanaona kwa macho yao.

Akina Mpendazoe watueleze, ni kifungu gani cha sheria za nchi kinachokataza shughuli za kisiasa baada ya uchaguzi mkuu?

Watueleza sababu za kuzuia mikutano ni zipi hasa kwani zimetajwa nyingi.

Hayo akina Mpendazoe hawataki kuyagusia wanaleta vihoja vya ufisadi

Ukitazama hali ilivyo sasa hivi, wapiga debe huzawadiwa hizi nafasi za kuteuliwa
Kila mmoja atasema, atafanya kila awezalo hata kama ni kinyume ili tu aonekane

Mpendazoe ulipohama CCMilikuwa haki yako, Uliporudi CCM ni haki yao.
Tena ulirudi ndani ya mkutano mkuu, ni fursa nzuri tu. Subiri wakati ukifika utafikiwa.

Tusichokitaka ni kauli za kutaka kubabaisha umma na kuendelea kujenga 'hasira' miongoni mwa jamii jkwa kudhani Watanzania ni wajinga wa kupumbazwa

Hii ni nchi yetu , tunaipenda na tunahitaji utulivu.
Hatuhitaji akina Mpendazoe watuelekeze nini cha kufanya kwa kauli zao na si sheria

Kama umeridhika na ukiukwaji wa katiba hilo liwe suala lako, wananchi wanahitaji sheria si kwa mafisadi na wala rushwa, bali zionekane zikitendwa na kutendeka kwa dhati

Mpendazoe, shariahazikutengenezwa kwa mafisadi tu, zimetengenezwa kwetu sote na tunapaswa kuzitii hata nayakati zinapokinzana na matakwa au matamanio yetu
 
"Fred Mpendazoe, post: 17295947, member: 382107"]
1. Serikali ya Rais Magufuli imechaguliwa na watanzania kikatiba katika Uchaguzi mkuu 2015.
Mpendazoe nani amekuambia uchaguzi unaondoa haiba ya udikteta duniani?

Kuna nchi ngapi zinafanya uchaguzi chini ya madikteta.
Hoja hapa ni kuwa,uchaguzi ni hatua moja, kusimamia sheria za nchi ni hatua nyingine.

Ni sawa na mzazi anayejifungua mtoto. Uzazi haumaanishi mzazi huyo mwema lazima atatoa mtoto mwema. Umeelewa! Uchaguzi una lengo la kupata viongozii! hauelezi Zaidi
2. Kulingana na katiba, Rais hushauliwa na Baraza la mawaziri. Na pia Raishushauriwa na Chama chake. Hivyo, Rais Magufuli anafanya maamuzi Kwa kushauriwa na taasisi hizi. Hivyo madai Kwamba anaamua bila kushauriwa hayana mashiko.
Hivyo ana dhima ya kukubali kila ushauri?

Kwa Mpendazoe hata kama ingalitokea kipande cha nchi kikauzwa, midhali kuna ushauri basi mamlaka zifuate tu.

Rais anashauriwa, dhima ya kupima ushauri na matokeo ya ushauri huwa mikononi mwake. Rais alipoapa kwa katiba, hakushirikisha CCM au baraza
3. Madai Kwamba anawagandamiza baadhi ya watanzania, ni jambo la kushangaza. Tukumbuke wakati WA sakata la EPA, Chadema walipiga kelele sana wakati JK alipowaomba wezi WA fedha za EPA wazirudishe. Wakasema anaongea na wezi. Rais Magufuli amechukua msimamo tofauti, amekuwa dhabiti. Sasa Chadema wanadai dikteta. Hapana.
Hapa unapindisha hoja. Sijui kama kuna hoja ya kupinga hatua zinazochukuliwa. Hoja ni kupinga marufuku ya mikutano.

Mpendazoe, huu ulaghai unakusiadiaje katika kujenga taswira na haiba yako?

Labda onyesha sehemu moja tu wapinzani waliposema hatua zinazochukuliwa dhidi ya ufisadi na rushwa ni za kidikteta ili nasi tuunge tela
4. Rais Magufuli amekuwa na msimamo Mkali dhidi ya Ufisadi, wakwepa kodi, ubadhirifu kwenye serikali na halmadhauri na mashirika ya umma. Anapigania utajiri WA Nchi Yetu uwanufaishe watanzania wote. Ukweli Rais Magufuli ni Jibu Kwa maombi ya watanzania wengi kutokana na hali ilivyokuwa imefika.
Hali ilifika pabaya kutokana na usimamizi wa hapo CCM! Hakuna anayepinga hatua ilimradi tu ziwe ndani ya sharia
4. Upinzani wanachokifanya ni kutaka kuwapotodha watanzania ili waichukie serikali yao. Upotodhaji lengo ni uchochezi
Tusaidie kuelewa, marufuku ya mikutano ya kisiasa yapo katika sharia gani za nchi, yanatumika wapi na kwasababu zipi.
Hapo tutajua uchochezi wa vyama vya siasa

Kama huna kifungu cha sheria, kuna tatizo gani ukakaa kimya! kuliko kuendelea na 'uchochezi' huu unaoufanya! Kumbuka kuongea jambo bila ushahidi ndio uchochezi
Ukowapi udikteta wa Rais Magufuli? Lakini uchochezi wa UKAWA in dhahiri. UKAWA wanadai demokrasia inaminywa. Tukumbuke, mgombea UKAWA alivyopatikana. Ilikuwa ndani ya chopa na watu wachache siyo kwenye vikao. Hapakuwa na mchakato ulio wazi. Iko wapi demokrasia kwenye UKAWA ?
Mpendazoe, unawekaje demokrasia ya chama cha siasa katika mizani na demokrasia ya Taifa?

Kumbuka Rais alipoapishwa alitumia katiba ya JMT ya mwaka 1977.

Ni Rais wa kila mmoja, anachokifanya ni kwa ajili ya Taifa.
Unapochukua mambo ya vyama ukayaweka katika mizani na hadhi ya Rais, humtendei haki. Hadhi ya Rais ni kubwa kuliko chochote kile unachokifikiria.

Please hebu jaribu kuheshimu mamlaka za nchi kwa kutoziweka katika mizani na vyama vya siasa.
Pia tukumbuke, walimtuhumu Lowassa Kwa muda mrefu kuwa ni fisadi na wakawaeleza watanzania kuwa wanao ushahidi. Ghafla wakaamua awe mgombea urais.Uko wapi Uzalendo WA kweli ndani ya UKAWA ?
Uzalendo ungeanzia kumshtaki kwanza.

Hapo CCM hawakuweza kumfikisha katika sheria, walikuwa naye hadi hatua ya mwisho ya mchujo wa Urais. Hawakuweza hata kumzuia.

Aliotuhumiwa nao wapo Bungeni tena wakiwa na nyadhifa.

CCM imekaa kimya , uzalendo upi unaongelea Mpendazoe?
Hivi magamba tuliyoambiwa yalivuliwa?

Wizi unaoendelea hadi kwenye taasisi nyeti ukifunikwa kwa 'wamalize kazi' ndio uzalendo? Mpendazoe, unaongelea uzalendo gani?
 
1.Hitler alichaaguliwa kwa kura nyingi kuliko hata za huyo wa kwako.
2. Rais afanye yote lakini kwa mujibu wa sheria, kinyume na hivyo ni udikteta bila chenga.
3. Kujaribu kuhalalisha anayofanya rais kwa sbabu nyepesi nyepesi ni kukosa hoja
4. Mpendazoe unajiaibisha bora ungenyamaza tu kwani hamna uteuzi kwa vile huna mkia sasa
5. Kusema UKAWA wanawapotosha Watanzania ni kujaribu kutuaminisha kwamba Watanzania hawana akili huru.
6. Matumizi ya neno uchochezi katika muktadha huu ni ishara ya kuchukua maneno kikasuku. Kaulize BAKITA na TATAKI wakueleza maana ya hilo neno.
7. Pole sana Fred utahangaika sana ila ukweli ni kuwa unajidhalilisha sana.
 
Mpendazoe nani amekuambia uchaguzi unaondoa haiba ya udikteta duniani?

Kuna nchi ngapi zinafanya uchaguzi chini ya madikteta.
Hoja hapa ni kuwa,uchaguzi ni hatua moja, kusimamia sheria za nchi ni hatua nyingine.

Ni sawa na mzazi anayejifungua mtoto. Uzazi haumaanishi mzazi huyo mwema lazima atatoa mtoto mwema. Umeelewa! Uchaguzi una lengo la kupata viongozii! hauelezi Zaidi Hivyo ana dhima ya kukubali kila ushauri?

Kwa Mpendazoe hata kama ingalitokea kipande cha nchi kikauzwa, midhali kuna ushauri basi mamlaka zifuate tu.

Rais anashauriwa, dhima ya kupima ushauri na matokeo ya ushauri huwa mikononi mwake. Rais alipoapa kwa katiba, hakushirikisha CCM au baraza
Hapa unapindisha hoja. Sijui kama kuna hoja ya kupinga hatua zinazochukuliwa. Hoja ni kupinga marufuku ya mikutano.

Mpendazoe, huu ulaghai unakusiadiaje katika kujenga taswira na haiba yako?

Labda onyesha sehemu moja tu wapinzani waliposema hatua zinazochukuliwa dhidi ya ufisadi na rushwa ni za kidikteta ili nasi tuunge tela Hali ilifika pabaya kutokana na usimamizi wa hapo CCM! Hakuna anayepinga hatua ilimradi tu ziwe ndani ya sharia Tusaidie kuelewa, marufuku ya mikutano ya kisiasa yapo katika sharia gani za nchi, yanatumika wapi na kwasababu zipi.
Hapo tutajua uchochezi wa vyama vya siasa

Kama huna kifungu cha sheria, kuna tatizo gani ukakaa kimya! kuliko kuendelea na 'uchochezi' huu unaoufanya! Kumbuka kuongea jambo bila ushahidi ndio uchochezi Mpendazoe, unawekaje demokrasia ya chama cha siasa katika mizani na demokrasia ya Taifa?

Kumbuka Rais alipoapishwa alitumia katiba ya JMT ya mwaka 1977.

Ni Rais wa kila mmoja, anachokifanya ni kwa ajili ya Taifa.
Unapochukua mambo ya vyama ukayaweka katika mizani na hadhi ya Rais, humtendei haki. Hadhi ya Rais ni kubwa kuliko chochote kile unachokifikiria.

Please hebu jaribu kuheshimu mamlaka za nchi kwa kutoziweka katika mizani na vyama vya siasa. Uzalendo ungeanzia kumshtaki kwanza.

Hapo CCM hawakuweza kumfikisha katika sheria, walikuwa naye hadi hatua ya mwisho ya mchujo wa Urais. Hawakuweza hata kumzuia.

Aliotuhumiwa nao wapo Bungeni tena wakiwa na nyadhifa.

CCM imekaa kimya , uzalendo upi unaongelea Mpendazoe?
Hivi magamba tuliyoambiwa yalivuliwa?

Wizi unaoendelea hadi kwenye taasisi nyeti ukifunikwa kwa 'wamalize kazi' ndio uzalendo? Mpendazoe, unaongelea uzalendo gani?
Mueleze huyo Fred Mpendazoe kuwa kama Magufuli ana nia njema na anaamini Katiba, kama ilivyo inamkwamisha, zipo njia halali na sahihi kwake kukabiliana na hali hiyo. Swali la kujiuliza ni kwa nini anakwepa kutumia njia hizo ambazo hata Katiba yenyewe tuliyo nayo inamruhusu kuzitumia bila kuvunja sheria?

Jibu rahisi linawezekana kuwa hana ujasiri na sababu ni woga wa kukabiliana na athari zinazoweza kujitokeza akiamua kuzitumia na hii ni dalili ya kongozi asiyejiamini. Ndiyo maana sisi wengine hatusiti hata mara moja kumuona kama dikteta uchwara kwani dikteta hangeogopa kufanya analotaka ndani ya Katiba.

Sababu nyingine ni kuwa huyu mtu kwa kweli hakujitayarisha na hana sifa za kuwa Kiongozi Mkuu wa nchi na mpaka leo bado hajaamini alishinda kihalali. Ubabe anaoutumia kwa sasa ni kama mwamvuli tu wa kuficha madhaifu yake kiuongozi, hana na hajawahi kutumia busara katika maamuzi yake kama kiongozi.
 
Vyama vinavyounda UKAWA vimetangaza kufanya maandamano yenye lengo la kupinga udikteta, UKUTA. Maana yake ni Kwamba serikali ya Rais Magufuli in ya kidikteta.

Niwakumbushe UKAWA yafuatayo:

1. Serikali ya Rais Magufuli imechaguliwa na watanzania kikatiba katika Uchaguzi mkuu 2015.

2. Kulingana na katiba, Rais hushauliwa na Baraza la mawaziri. Na pia Rais hushauriwa na Chama chake. Hivyo, Rais Magufuli anafanya maamuzi Kwa kushauriwa na taasisi hizi. Hivyo madai Kwamba anaamua bila kushauriwa hayana mashiko.

3. Madai Kwamba anawagandamiza baadhi ya watanzania, ni jambo la kushangaza. Tukumbuke wakati WA sakata la EPA, Chadema walipiga kelele sana wakati JK alipowaomba wezi WA fedha za EPA wazirudishe. Wakasema anaongea na wezi. Rais Magufuli amechukua msimamo tofauti, amekuwa dhabiti. Sasa Chadema wanadai dikteta. Hapana.

4. Rais Magufuli amekuwa na msimamo Mkali dhidi ya Ufisadi, wakwepa kodi, ubadhirifu kwenye serikali na halmadhauri na mashirika ya umma. Anapigania utajiri WA Nchi Yetu uwanufaishe watanzania wote. Ukweli Rais Magufuli ni Jibu Kwa maombi ya watanzania wengi kutokana na hali ilivyokuwa imefika.

4. Upinzani wanachokifanya ni kutaka kuwapotodha watanzania ili waichukie serikali yao. Upotodhaji lengo ni uchochezi.

Ukowapi udikteta wa Rais Magufuli? Lakini uchochezi wa UKAWA in dhahiri. UKAWA wanadai demokrasia inaminywa. Tukumbuke, mgombea UKAWA alivyopatikana. Ilikuwa ndani ya chopa na watu wachache siyo kwenye vikao. Hapakuwa na mchakato ulio wazi. Iko wapi demokrasia kwenye UKAWA ?

Pia tukumbuke, walimtuhumu Lowassa Kwa muda mrefu kuwa ni fisadi na wakawaeleza watanzania kuwa wanao ushahidi. Ghafla wakaamua awe mgombea urais. Uko wapi Uzalendo WA kweli ndani ya UKAWA ?

Watanzania tumuunge Mkono Rais Magufuli.
Huu uandishi huu aisee,
bora hata ulivyokosa ubunge
 
Ungekuwa baba yangu wewe leo ndiyo ungekuwa mwisho ningejitenga kbs,
 
Ni dhahiri Mpendazoe anafanya " Rhetoric", mada yake hii haina Substance.

Hoja siyo kupambana na Ufisadi, Infact sisi tunataka Rais apambane na Ufisadi kwelikweli tena kama ikiwezekana akaze zaidi LAKINI hiyo ni sehemu mojawapo ya kazi yake tu, Sehemu nyingine ya Kazi yake ni KUHESHIMU, KULINDA na KUITETEA KATIBA, katika hili kwa maoni yangu naona amefeli vibaya sana, na sisi wananchi tutamwambia!.

Kiufupi yeye Rais ni zao la Demokrasia, ameikuta wenzie wameijenga, Ameikuta wananchi wanaiheshimu na kuienzi, Namshauri na yeye aiheshimu, aienzi, aijenge na pindi wakati wake wa kukabidhi kijiti kwa mwenzie utakapofika, basi aikabidhi nchi iliyopiga hatua pana katika uhuru wa wananchi na demokrasia zaidi ya kipindi alivyoipokea kwa watangulizi wake
.

Katika nchi yoyote duniani, Kama mtu aliapa kuilinda na kuitetea Katiba, basi ni dhahiri hana budi kuheshimu vipengele vyote vilivyomo humo kwa dhati, hapaswi kutekeleza baadhi na kuviminya vingine, kufanya hivyo ni udhaifu katika uongozi.

Lakini kama mtu huyo anaona Kutawala kwa mujibu wa katiba kunamchelewesha kuwaletea watu wa nchi hiyo manna, ipo njia mbadala nayo ni Kususpend Katiba na kutawala kwa mujibu wa decrees!, Kana hilo halifanyiki basi ni dhahiri watu hawatokubali
 
Unajitekenya huku unacheka..katiba inatoa Uhuru wa kutoa mawazo(freedom of expression) na association pia,yeye anakataza mikutano na maandamano huku akiwa wakwanza kuifanya tena kwa kuwaponda wapinzan..wajinga kama weww ndio wanaoamin hamna udikteta.
Njaa mbaya sana.Huyu jamaa amepoteza mwelekeo hajui aende wapi maskini.
 
.... a transition none had expected. The burden friends expected they would pass over to neighbours; alas, has turned over their shoulders. No more free money changing hands. JPM on the right move and correct direction.
 
Back
Top Bottom