Nimeisoma hiyo news ila kuna sehemu umekosea kuelezea.
ni hivi bibi alimvulia nguo mpangaji wake kumdai akiwa na binti yake, mtoto wa kiume akawa anamwambia mama yake avae nguo, mama hakusikia , mama akamgeuzia kibao kijana wake anamtetea mpangaji. kwahiyo kama anamtetea amilipie deni yeye, mama akampandishia hasira kijana wake , kijana akaingia chumbani kwake, mama akazidi kumpandishia kijana wake huku akimfuata hadi chumbani kwake.
hapo kijana na yeye ndipo alipomtolea uvivu mama yake akamwambia aondoke hapo chumbani kwake haraka na akavae nguo la sivyo atamuonyesha alivyo mahiri sana kwani ameanza siku nyingi sana. kijana akawa kama vile anakwenda kufunga mlango wa chumbani , mama alipoona amechenjiwa na kijana wake, akakimbia akipiga kelele na kupotelea kwenda kuvaa nguo!!
Pale kwetu kuna mama alikuwa anaibiwa ndizi na magimbi (sowe) kila mara
alipojua ni watoto wa jirani alichofanya ni kuvua nguo na kuzunguka mipaka ya
shamba huku akipiga debe tupu akisema mtoto wa fulani lazima utakufa
kwa kuwa umefanya so and so,
Baada ya miaka zaidi ya 20 nasikia ile familia ya yule jirani watoto
wote wamekufa. Nilipoambia hivyo nilikumbuka mimi japo najua watu
hawawezi kukumbuka hiyo kitu. Kwa hiyo nataka kusema kuwa
laana huwa inakuja hata kama ni baada ya miaka mingi kupita.