Ukiuona utupu wa ajuza utalaanika?

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,174
Kenya kuna mambo. Huyu ajuza kachoshwa na kupigwa kalenda na mpangaji wake ambaye anadai au kusingizia matatizo ya kifamilia yamemfanya kushindwa kulipia kodi ya pango.

Ajuza alipoona miezi inakatika na kodi hailipwi basi akaja na staili nyingine ya kwenda kwa mdaiwa wake sugu akiwa uchi wa kuzaliwa huku akisindikizwa na binti yake mkubwa na wakamgongea mlango mdaiwa wao.

Huku matusi mazito yakiwatoka walidai afungue auone uchi wa ajuza kama hatapata laana na kufa kiroho cha papo kwa hapo. Mdaiwa kusikia hivyo aliongeza komeo na kujifungia ndani.

Umati wa watu ulianza kujikusanya na kutaka kujua kuna nini............................mtoto wa kiume wa yule ajuza alipoona mama'ake anamtia aibu akaamua kumtishia mama'ake ya kuwa kama hatavaa nguo basi atabana mlango na kumshughulikia mama'ake papo kwa hapo bila ya kumwonea soooo hata chembe!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Yaelekea yule ajuza anajua makali ya mwanawe kwani alikimbilia ndani na kuvaa nguo zake huku akiwaacha watazamaji wa filamu ya bwerere mbavu zikiwa hoi kutokana na burudani ya laivu............au niseme ya papo kwa hapo.....

Kwa wanaujua umombo kazi kwenu.........

Crazy Monday


Angry grandma undresses to ‘curse' tenant



Updated Sunday, May 27 2012 at 21:00 GMT+3
 
eeeeee makubwa jamani mmmh ina maana mtoto mkubwa alishindwa kumshauri mamaye kwani hajui mtu akizeeka anakuwa ka mtoto ?
 

[MENTION]mtoto Pole[/MENTION] Malezi ya watoto ndiyo huamua atakuaje.................unapoona watoto wanafanya vituko tena wanazaidi ya miaka 50 ujue malezi yalkuwa na mgogoro mkubwa....kama mtoto wa kiume anamtishia mama yake kumdu ujue ipo shughuli pale........
 
Mkuu Kenya kuna mambo kweli kweli!.
Sasa kuhusu swali lako jibu liko wazi yakuwa ni HAPANA haulaaniwi,
labda kama mwonyesha uchi amekulenga wewe mwonaji, maana kama ni kuona tu ikawa laana basi wale wote walioshuhudia hile live show walilaaniwa!
Alafu huyu mama asifikri kuwa ana binti, kama ni mtoto anaye mmoja tu wakiume japo naye sijui alitaka kumshughulikia kivipi! yawezekana ana hasara kotekote.
Nina maana kuanzia wapangaji, majirani hadi watoto wake!.
 
eeeeee makubwa jamani mmmh ina maana mtoto mkubwa alishindwa kumshauri mamaye kwani hajui mtu akizeeka anakuwa ka mtoto ?

biggirl watoto hao kwisha khabari yao.........wakike anamshangilia mama'ke..........wakiume anamkataza maama'ake kwa kumtishia kumbaka...........................ni makubwa kabisa haya.......
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kenya kuna mambo kweli kweli!.
Sasa kuhusu swali lako jibu liko wazi yakuwa ni HAPANA haulaaniwi,
labda kama mwonyesha uchi amekulenga wewe mwonaji, maana kama ni kuona tu ikawa laana basi wale wote walioshuhudia hile live show walilaaniwa!
Alafu huyu mama asifikri kuwa ana binti, kama ni mtoto anaye mmoja tu wakiume japo naye sijui alitaka kumshughulikia kivipi! yawezekana ana hasara kotekote.
Nina maana kuanzia wapangaji, majirani hadi watoto wake!.


Kyaiyembe hata mtoto wa kiume anayemtishia kumbaka mama'ake naye ana malezi bomu............
 
Last edited by a moderator:
Kudadadeki umemsikia kijana alivyomwambia mama yake? Mkuu Ruta uliipunguza utamu wake!
{"So this is what you come to show me yet you know l started these things long ago? Let me show you what an expert l have become!" her son threatened, making for the door as if to close it.}
 
Hiyo ipo kule kwetu hasa sehemu za mpakani na kenya
wanaita 'nguma' anavua au anapandisha kabisa nguo zote kisha anakuinamia
bila shaka ni imani, lakini ni laana kama imefanyika bila maoneze.
 
kijana alikuwa na maana ya kumpiga
sizani kama ni ulivyoelewa mkuu.

Kudadadeki umemsikia kijana alivyomwambia mama yake? Mkuu Ruta uliipunguza utamu wake!
{"So this is what you come to show me yet you know l started these things long ago? Let me show you what an expert l have become!" her son threatened, making for the door as if to close it.}
 
omg! this granny and her son need to see a shrink asap.. stripping nude does NOT solve anything...
Im glad Im not related to them, it's total humiliation..


she is an attention wh0re
 
Hata kuko nitokako hii dhana ipo.
Mzazi akikuvulia nguo ni laana.

Kama ni kweli au si kweli inafanya kazi sijui, ila siwezi jiweka mazingira ya mzazi kufikiria kunifanyia hivi.
Huko sawa mkuu lakini nakushauri uwalee watoto wako kama ulivyolelewa!,
nina maana kuwa miaka ka 20 na zaidi iliyopita ilikuwa ni vigumu kumkuta mzazi akimtukana mwanae kwa kutumia viungo vyake vya siri au vya mzazi mwenzie.
Lakini siku hizi mzazi kumtukania uchi (hasa wamama) mwanae ni kitu cha kawaida, hata wasiwasi kuwa hiki nilichomtukania mtoto atatakajua ni kitu gani hatuna tena.
Huwezi kuzuia kujua lakini U-privacy uwepo ili kujenga heshima.
Kwa ujumla mtoto umleavyo ndivyo akuavyo aliyezoea kusikia uchi uchi! hataogopa kuuona au siyo!.
 
Hii kenya wazee wamekuwa nì vituko mara huyu kuvua kwa ajili ya kudai kodi,mwingine anataka kupigwa mtama na vijana ama kweli dunia imekalibia kufika mwisho.

:->ALWAYS A BIG LIAR SHOULD HAVE A BIG MEMORY:-"
 
Kenya kuna mambo. Huyu ajuza kachoshwa na kupigwa kalenda na mpangaji wake ambaye anadai au kusingizia matatizo ya kifamilia yamemfanya kushindwa kulipia kodi ya pango. Ajuza alipoona miezi inakatika na kodi hailipwi basi akaja na staili nyingine ya kwenda kwa mdaiwa wake sugu akiwa uchi wa kuzaliwa huku akisindikizwa na binti yake mkubwa na wakamgongea mlango mdaiwa wao. Huku matusi mazito yakiwatoka walidai afungue auone uchi wa ajuza kama hatapata laana na kufa kiroho cha papo kwa hapo. Mdaiwa kusikia hivyo aliongeza komeo na kujifungia ndani. Umati wa watu ulianza kujikusanya na kutaka kujua kuna nini............................mtoto wa kiume wa yule ajuza alipoona mama'ake anamtia aibu akaamua kumtishia mama'ake ya kuwa kama hatavaa nguo basi atabana mlango na kumshughulikia mama'ake papo kwa hapo bila ya kumwonea soooo hata chembe!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Yaelekea yule ajuza anajua makali ya mwanawe kwani alikimbilia ndani na kuvaa nguo zake huku akiwaacha watazamaji wa filamu ya bwerere mbavu zikiwa hoi kutokana na burudani ya laivu............au niseme ya papo kwa hapo..... Kwa wanaujua umombo kazi kwenu......... Crazy Monday Angry grandma undresses to ‘curse’ tenant Updated Sunday, May 27 2012 at 21:00 GMT+3
kumbe hii staili ya kupeana laana bado inatumika-huyo mama naona anafaham kichwa ya mwanae wa kiume ndo mana kafwata amri
 
Back
Top Bottom