Ukitaka ukosane na rafiki omba akukopeshe fedha...

Ukitaka ukosane na rafiki omba akukopeshe fedha...

Umesuka nondo 250,zikahitajika zingine 80 ambazo hazikuwa kwenye mahesabu...wakati huo mashine ziko saiti na zote zinalipiwa kwa siku,wakati huo huo inabidi uweke mlinzi kwa sababu zege haijamwaga;utafanyaje
Acha kulia lia mkuu.Hivi una umri gani? Mbona jamaa hapo juu amekufafanulia vizuri tu Lakini.SIO LAZIMA UKOPESHWE,NI HIYARI YA MTU.
 
Ila Mtoa mada post zake anaonekana kama msumbufu ana jazba kumdai mtu kama huyu anaweza kukutukana kabisa
Mimi mwenyewe kuna jamaa yangu nilimuazima pesa hivi karibuni ila naona siku zinazidi kwenda tu muda aliohaidi umepita naona kimya tu naona dalili za kulipwa kama zinafifi kwahiyo nawaza huyu mtu inakuwaje
Hapo ndio basi tena,inabidi uwe mpole tu
 
Yaani ni shida,, ukimkopesha rafiki yako mara nyingi hazirudi kama ulivyo mkopesha, Kama ulimpa laki 5 yeye anaanza kukurudishia mara akupe elfu 20, 70, 90, 30 yaani mpaka unajuta.
Wengine ndiyo inakuwa kama umewapa kumbe ni mkopa.
Kwa sasa sikopeshi tena, kwanza wanarudisha nyuma maendeleo yako!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani ni shida,, ukimkopesha rafiki yako mara nyingi hazirudi kama ulivyo mkopesha, Kama ulimpa laki 5 yeye anaanza kukurudishia mara akupe elfu 20, 70, 90, 30 yaani mpaka unajuta.
Wengine ndiyo inakuwa kama umewapa kumbe ni mkopa.
Kwa sasa sikopeshi tena, kwanza wanarudisha nyuma maendeleo yako!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Vipi mda wa kurejesha wanaweka na ya kutolea??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukitaka ukosane na rafiki omba akukopeshe fedha..
Siku mbili tatu zilizopita nilipata changamoto kidogo za kiuchumi,kutokana na mambo ya ujenzi....wajuzi wanasema zege hali lali,nikajishauri nikaona ngoja niombe fedha ya dharura kwa marafiki zangu.Majadiliano yakawa hivi:-
Mimi: mambo vipi mkuu?naomba unisaidie kiasi fulani cha dharura by alhamisi nitakurudishia hata kwa riba.
Rafiki 1: Sawa haina shida kaka nitakucheki baadaye
Baada ya hapo kimya,ukimpigia simu hapokei
Rafiki 2: Ok nitakupatia kesho
Kesho inafika kimya,ukimpigia simu hapokei
Rafiki 3: Siko vizuri kiuchumi,biashara zimesimama kaka
Bora huyu alikuwa muwazi na nilimuelewa
Rafiki 4 : Siko vizuri kaka,nitakupatia nusu yake
Mimi: Nashukuru nilikuwa naitaji full

Kutokana na hali hiyo,nilichoweza kujifunza ili usikosane na rafiki yako inabidi mahusiano yenu yasihusu mambo ya fedha.
Kukopesha rafiki hela imekuwa ni chanzo cha kuvunja urafiki-zingatia hilo pia
Kuna rafiki nilimkopesha hela niliyopata kama mkopo wangu wa kwanza kazini mwaka 2003 shilingi 1,700,000
mpaka leo hajanilipa
 
Yaani ni shida,, ukimkopesha rafiki yako mara nyingi hazirudi kama ulivyo mkopesha, Kama ulimpa laki 5 yeye anaanza kukurudishia mara akupe elfu 20, 70, 90, 30 yaani mpaka unajuta.
Wengine ndiyo inakuwa kama umewapa kumbe ni mkopa.
Kwa sasa sikopeshi tena, kwanza wanarudisha nyuma maendeleo yako!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Daah hyo ya kurudisha hela robo robo inaboa sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huko unakoanza wenzako tushapita. Jifunze kuwa na nidhamu. Badala ya kulaumu rafiki zako hawakusaidii jichunguze wewe unakosea wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndo maana na mm nkamwambia atakua Ana tatizo kwny ulipaji huyu.

Huenda akiazimwa zile ela ndogo ndogo Kama buku, buku 2 huwa harudishi.

Sasa inapotokea anahitaji Pakubwa,

WATU WANAKUNA VICHWA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nikuulize swali,kwa muda huu hapo ulipo umepofuka macho ghafla...na daktari anasema ndani ya dakika 20 unatakiwa uwe umetibiwa lasivyo utakufa;na ili akuhudumie unatakiwa utoe 20,000/= kama huna hupati matibabu.Na kwa bahati mbaya wewe huna,utafanyaje?
Hela ndogo Kama hizo hukopi, unaazima.

Na Kama Ni mtu Safi, Hata Dokta mwenyewe anaweza kukudhamini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo ni ile kujitikisa baada ya kunywa dawa badala ya kutikisa dawa yenyewe!

Ni kutafakari baada ya kukubali, anapima uongo na ukweli, anaona bora kukaa kimya maana kimya nalo ni jibu

Sent using Jamii Forums mobile app
Huu ni uswahili ambao huwa sipendi maishani. Mtu mnafiki unamuitaje rafiki? Yani ukubali kunisaidia afu badae uzime simu! Ni kwamba unaogopa kunisaidia sikatai sasa kwanini unikwamishe kunipa ahadi hewa. Ukiona huwezi unasema dhahiri ili nitafute njia nyingine. Kukaa kimya ni tafsiri ya kunionea wivu na kutopenda nifanikiwe. Na ndo mwisho wa urafiki wetu.
 
Duuh ! Asilimia kubwa sana waliochangia inaonyesha hawajawahi kuomba mkopo kwa Rafiki ila wameombwa wao tu MEMBERS WA JAMII FORUM OYEE!

Sent using Jamii Forums mobile app
Nnachoamini Mimi
,
Rafiki yako hutakiwi kuomba/kuombwa mkopo na rafiki yako

Rafiki yako anatakiwa akuazimishe pesa

MASWALA YA KUKOPESHANA, UNATAKIWA KWENDA SEHHEMU SAHIHI

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duuh ! Asilimia kubwa sana waliochangia inaonyesha hawajawahi kuomba mkopo kwa Rafiki ila wameombwa wao tu MEMBERS WA JAMII FORUM OYEE!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kwani hujui Jamii Forum ni ikulu ndogo. Mimi nimecomment kuhusu nilivonyimwa mkopo jamaa flani akafyatuka kudai nirudi kulima. Kucheki uzi wake anauliza connection ya watoto wa kishua akalelewe. Sasa sijui kati ya anayekopa na marioo nani ana njaa.
 
Back
Top Bottom