Ukitaka ukosane na rafiki omba akukopeshe fedha...

Ukitaka ukosane na rafiki omba akukopeshe fedha...

Huu ni uswahili ambao huwa sipendi maishani. Mtu mnafiki unamuitaje rafiki? Yani ukubali kunisaidia afu badae uzime simu! Ni kwamba unaogopa kunisaidia sikatai sasa kwanini unikwamishe kunipa ahadi hewa. Ukiona huwezi unasema dhahiri ili nitafute njia nyingine. Kukaa kimya ni tafsiri ya kunionea wivu na kutopenda nifanikiwe. Na ndo mwisho wa urafiki wetu.
Bora unafiki kuliko kusumbuana baadaye tena kwa hela yangu aroo!

Aliyegongwa nyoka kila apitapo eneo hilo huwa makini na jani likimgusa tu lazima aruke

Watu wameacha uungwana na hasa hupotea baada ya kukopa, mifano mingi sana!

Kwa nn tugombane tena na hela yangu!?

Wanasema mtu akikusaidia jua kwamba anao ndugu zake amewaacha na shida zao akakuthamini wewe just a friend!

Nisipozima mie muda wako utazima yako, why¿¿?

Take your time baby

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kwani hujui Jamii Forum ni ikulu ndogo. Mimi nimecomment kuhusu nilivonyimwa mkopo jamaa flani akafyatuka kudai nirudi kulima. Kucheki uzi wake anauliza connection ya watoto wa kishua akalelewe. Sasa sijui kati ya anayekopa na marioo nani ana njaa.
Tatizo watu wanajifanya wajuaji,ukifuatilia maisha yake si ajabu anaishi kwa shemeji au yupo chumba kimoja amepanga
 
Huu ni uswahili ambao huwa sipendi maishani. Mtu mnafiki unamuitaje rafiki? Yani ukubali kunisaidia afu badae uzime simu! Ni kwamba unaogopa kunisaidia sikatai sasa kwanini unikwamishe kunipa ahadi hewa. Ukiona huwezi unasema dhahiri ili nitafute njia nyingine. Kukaa kimya ni tafsiri ya kunionea wivu na kutopenda nifanikiwe. Na ndo mwisho wa urafiki wetu.
Kweli mkuu,uko sahihi.
 
Ukitaka ukosane na rafiki omba akukopeshe fedha..
Siku mbili tatu zilizopita nilipata changamoto kidogo za kiuchumi,kutokana na mambo ya ujenzi....wajuzi wanasema zege hali lali,nikajishauri nikaona ngoja niombe fedha ya dharura kwa marafiki zangu.Majadiliano yakawa hivi:-
Mimi: mambo vipi mkuu?naomba unisaidie kiasi fulani cha dharura by alhamisi nitakurudishia hata kwa riba.
Rafiki 1: Sawa haina shida kaka nitakucheki baadaye
Baada ya hapo kimya,ukimpigia simu hapokei
Rafiki 2: Ok nitakupatia kesho
Kesho inafika kimya,ukimpigia simu hapokei
Rafiki 3: Siko vizuri kiuchumi,biashara zimesimama kaka
Bora huyu alikuwa muwazi na nilimuelewa
Rafiki 4 : Siko vizuri kaka,nitakupatia nusu yake
Mimi: Nashukuru nilikuwa naitaji full

Kutokana na hali hiyo,nilichoweza kujifunza ili usikosane na rafiki yako inabidi mahusiano yenu yasihusu mambo ya fedha.
si bora rafiki,mimi nimekosana na ndugu wa damu kisa laki tatu.
 
Sio Kila ahadi lazima utimiziwe.

Wengine anakuahidi atakupa,

Afu anawatafuta wawili watatu anawaulizia khs mwenendo wako kwny maswala ya fedha.

Wakionesha kukutilia mashaka.

NA YEYE ANAKUCHINJIA BAHARINI.



Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa huo ni ushamba niendeshe usafiri wa cc 4600 halafu nikutapeli laki 2;huo utakuwa ni uzwazwa.
 
Kukopesha rafiki hela imekuwa ni chanzo cha kuvunja urafiki-zingatia hilo pia
Kuna rafiki nilimkopesha hela niliyopata kama mkopo wangu wa kwanza kazini mwaka 2003 shilingi 1,700,000
mpaka leo hajanilipa
Wapo wa namna hiyo wasiokumbuka fadhila
 
Bora unafiki kuliko kusumbuana baadaye tena kwa hela yangu aroo!

Aliyegongwa nyoka kila apitapo eneo hilo huwa makini na jani likimgusa tu lazima aruke

Watu wameacha uungwana na hasa hupotea baada ya kukopa, mifano mingi sana!

Kwa nn tugombane tena na hela yangu!?

Wanasema mtu akikusaidia jua kwamba anao ndugu zake amewaacha na shida zao akakuthamini wewe just a friend!

Nisipozima mie muda wako utazima yako, why¿¿?

Take your time baby

Sent using Jamii Forums mobile app
"...Take your time baby...."
Apo juu means wewe ni mwanamke! Masuala ya kuanza kuniita baby mi lini nimekuwa mumeo?
 
Back
Top Bottom