Buzi Maarufu
JF-Expert Member
- Oct 30, 2019
- 422
- 330
Nimejifunza kitu kikubwa Sana kutoka kwako,Mimi nalizwa sana na ndugu na marafiki halafu mimi nikikopa kwao Wala siwasumbui, mwaka huu nimeamua sikopeshi nng'oo bora nionekane mbaya kuliko kuonekana mwema halafu nadhulumiwa kila siku,Kuna huyu mmoja baada ya kunidhulumu na kuonyesha dharau nimemua kufuta hata namba yake,na nina mpango nikamwambie hata shangazi yake(mama yangu) udugu na mtoto wa Kaka yake umekwisha.Equation x, Usimkope rafiki yako mwambie naomba kiasi fulani sio kwa mkopo.
Na wala usimkopeshe rafiki yako inabidi umpe tu usimdai na kama huna sema huna.
Na hata Ndugu akikuomba umkopeshe muambie sina hela labda nikupe kiasi kidogo ufabye na mipango mingine upate kujazilia.
Na hata wewe ndugu Muombe hela usimkope.
Mimi kama unanikopa unaniambia utanirudishia kesho si bora usubiri hiyo kesho tu utumie pesa yako.omba bwana.
Sasa mfano wewe mtoa mada sijui kwa nini hukusubiri hiyo alhamisi tu ukatumia pesa yako.
Mkopo wa uhakika uende kwa watu ambao wapo kwa ajili ya kutoa huduma hiyo.
Saikolojia zetu sisi watu hatupendi kuombwa Mungu ndo hupenda watu wakimuomba.kwa hyo hakuna mtu atafurahi ukienda kumuomba kitu.
Fuata hii principle kisha rudi hapa
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app