Ukistaajabu ya Escrow utaona ya Mwakyembe

Ukistaajabu ya Escrow utaona ya Mwakyembe

unajua unachokiongea lakini wewe watu wengine mnafaa kuchunga mbuzi wala siyo kitu kingine umeandika ubwabwa kabisa hakuna cha maana hata kimoja unaongozwa na hisia za kishamba kabisa.

tatizo aliziba mianya yote ya kifisad, aliwazibia hata wakubwa kupitisha mirung yao ambayo ndo inawaweka mjini.

Chezea mirungi weye

wamwemeka wazir mdebwedo-6- ili mambo yawe kama yalivyopangwa, ili pesa za uchaguz mkuu zivunwe kwa biashara ya mihadarati kwa kipind hik muhimu,
mwakyembe mshenz sana anabania mpaka wakubwa zake dili (haram) zenye mkwanja mrefu???
Bora aende eac tumtumie huyu 6 kufanikisha dil zetu za sembe.
alichoandika huyo mwenzio hakina tofauti na unayoandika wewe simiyu yaani wote nyie akili zenu ni sawa ila kidogo mwenzio amekuzidi kasema ile kweli yake.
 
Tina haitashangaza kama nitaambiwa kwamba wewe ni mmoja wa wauza unga wakubwa au wakwepa kodi wa pale bandari. Hao vijana wapya aliowaweka wakiongozwa na msambichaka ndiyo waliowezesha ongezeko la mapato pale bandarini. Kama Mwakyembe alifanya hivyo kwa nia ya kufanya ufisadi, ni kwa vipi aliwezesha ongezeko la makusanyo ya kodi?
 
Last edited by a moderator:
Lingine aliaribu nipale alipodai hata MH MWIGULU AMWITE LEO HII NAKUMWAMBIA KUUNA BIL 20 UNUNUE NDEGE AMA BEHEWA AKAJIBU ATCL WATANZAMEHE KWA HILII...HII ILIKUWA DHIHAK NAAMINI WENGINE WALIENDA KUMFANYIA TALWA,,HATA KAMA HUNAMPANGO WAKUSAIDIA KITU. UKIIIWA. WAZIRIHUSIKA USITOE YAMOYONI MBELE YAKADAMNASI KUMBUKA ATCL NAYO IKO CHINIYAKE IMAGINE WAFANYAKAZI WAKE WAMEJISIKIAJE ALIVYOSEMA,,MAISHA YA WANGAPI AMEYADHARAU KIRAHISI HIVYO,,,NAHISI NIWAZIRI MZURI ILA KUNAMTU KAMWINGIZA CHOOCHAKIKE KUDILI NA MEDIA, ANYWAY ALL THEBEST TUSAIDIEEAC WANAVISA MOJA ILA NCHIYETU AIPO ANATUSAIDIAJE KWAHIKI??
 
atcl,trl,tazara mashirika yote yako hoi halafu mnasema anaonewa tatizo watu wanapenda viongozi wa porojo mpaka sasa hivi atcl anayeongoza anakaimu kwanini mashirika nyeti yanakuwa yanakaimiwa mwakyembe hafai kuwa waziri ni mganga njaa kama waganga njaa wengine
 
Wewe lazima utakuwa miongoni mwa wezi wa makontena ambao Mwakyembe aliwaamuru kitengo kizima kwa pesa zenu binafsi kumlipa yule mama Mcongo mwenye container Lake la vitenge lililopotea chini yenu!

Umeandika kwa akili yako au umeshikiwa akili! We ni janga!
 
kusema kweli mwakyembe ni jembe. hakuna binadamu asiye na mapungufu. kwanza amechukua wizara ikiwa na mapungufu kibao kwa miaka miwili amejitahidi
 
Umesema mfagizi ana nini ?
Mwizi! Mijizi yote ya bandari iliyofukuzwa au kuondolewa kwenye vitengo nyeti inaweweseka!
Wameiba mno TPA hasa idara ya uhasibu mpk mfagizi ana gorofa!
 
Dr. Harrison Mwakyembe! Mtanzania Mzalendo na Mchapakazi!
Ninyi mijizi ya pale TPA lazima mumchukie!
 
acha mambo yako umetumwa na ulicho andika hakina tofauti na hekaya za abunuas kazi aliyo fanya mwakyembe tunaijuwa na hata mpango wa mafisadi tunaujuwa na wanashangilia mwakyembe kubadirishiwa wizara

Sasa kwa nini usimpinge kwa hoja badala ya kukata viuno Tu hapa kwa maneno matupu, hoja hujibiwa kwa hoja. Au wewe ndio Mwakyembe umepaniki mambo yameharibika?
 
Mwizi #Tina ....na bado Mwakyembe ndio dawa yenu thieves like you...!!!

Hamna kitu, porojo tu, I DOUGHT HATA HUJUI KUTOA USHAHIDI WA UFISADI WW MTOTO....i believe ww ni kati ya wezi rungu la Mwakyembe liliwakuta...!!!

Kuhusu uhusiano wa Mwakyembe, Tizeba Na Mwinjaka ww ni muongo MKUBWA, MWIZI WEEE...wana mahusiano mazuri sana sana, tena hapa ndio nikajua ww mwizi mkubwa, i hope umefukuzwa BANDARI WW...!!

Mwizi wee,,,!!
 
Watu wanaoona uchapakazi wa mwakyembe ni wanyakyusa tu sijui kwanini
 
Wizara ya Uchukuzi ina taasisi nyingine lakini msisitizo wa mwandishi ni TPA nafikiri mwandishi ana maslahi huko. Ingekuwa bora anaetaka maslahi yake ili tunaposoma tuwe na mwanga mzuri wa kuchambua. Maoni yangu ni kuwa serikali havijaweza vya kutosha katika Wizara hii ya Uchukuzi ambayo Kwangu ni mhimili mkuu wa uchumi wetu. Hatuna kipaumbele sahihi katika kushughulikia miundombinu ya Uchukuzi. Kwahiyo inawapa nafasi wanasiasa na watendaji kubuni miradi yenye faida binafsi kwao na siyo kwa nchi. Lakini pia inawafanya waende kwa propoganda zisizo na faida. Wenzetu ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki wanatenda kwa weledi na baada ya muda mfupi hatutakuwa na cha kuuza - na yawezekana hata watu wetu wa ndani wakaanza kutegemea miundombinu ya nchi jirani kusafirisha mizigo yao! Udimore Mwakyembe kama mtu binafsi kwani yote uliyoorodhesha anafanya kama Mawaziri wote w navyo fanya katika Wizara zao. Hili ni tatizo la mfumo na wala halitatatuliwa kwa kufuatia mtu mmoja mmoja.
 
Huyu mwanamke ana genye, na kazibiwa mirija ya kifisadi ndo mana anabwabwaja tuu, ningemwona wa maana endapo angeweka mafanikio ya mwakyembe na mapungufu/ ufisadi wa mwakyembe (angetuorodheshea mema na mabaya ya mwaki). Bt kitendo cha kuorodhesha mabaya weeee inaleta picha kuwa ana chuki binafsi.

Na ukitafakari kwa jicho kali kutokana na hekaya yako hiyo, moja kwa moja mimi ntamkimbilia mzee wa tezi dume kuwa ndiye zezeta coz kama hayo yote mteule wake kayafanya, kwann asingemtimua mapema? Pili kama kweli mwaki kafanya hayo mkulu hajaliona hilo? Na kama hajaliona basi huo ndo udhaifu wake mkubwa alionao, na kama kaliona hilo kwanini asimtimue kabsa badala yake anamhamisha wizara?
In unaweza dhani unamchafua mwakyembe kumbe kupitia hekaya yako hiyo unamgusa waziri mkuu na rais.
 
Hii inchi inachekesha,
Tunaowana ni wachapa kazi kumbe nao ni mafisadi?
Kweli hakuna aliye msafi.
 
SIYO TPA tu mkuu ambako Mwakyembe amekuwa akifanya ufisadi. Mwakyembe amekuwa akiwatumia ndugu na jamaa zake kuchota pesa sehemu nyingi za taasisi zilizo chini ya wizara ya uchukuzi. Kuna ndugu yake pale Wizarani anaitwa Tumpe Mwaijande, Huyu mama ni Director wa Maritime safety and security.

Mwakyembe amekuwa akimtumia huyu mama kukamilisha ufisadi wake. Huyu Mama ni mpuuzi tu. Miaka ya 2003, huyu mama alikuwa na scandal ya kuuza vyeti vya mabaharia pale wizarani. Lakini Baada ya Mwakyembe kuingia pale alimpandisha cheo huyu mama fisadi kwa sababu tu wanatoka sehemu moja. Hiyo ya hali ya hewa kuchafuka pale wizari ni kweli kabisa mkuu, Huyu MWAKYMBE alikuwa hashirikiana na watendaji waaandamizi wenzake.

Alijifanya yeye anajua sana, kumbe ilikuwa ni mbinu yake ya kuficha ufisadi wake. Kuna tetesi kuwa Naibu waziri wa Uchukuzi alitembelea moja ya taasisi za wizara hiyo, baada ya kuambiwa kero na changamoto zilizokuwa zikiwakabiri wafanyakazi wa taasisi hiyo ya umma, Dk. Tizeba aliahidi kuzitafutia kero ufumbuzi kero hizo. Lakini cha kushangaza mwakyembe aliivyopata taarifa ya ziara ya Tizeba kwenye taasisi hiyo, Mwakymbe alitoa maneno ya Kejeli kwa Dk. Tizeba akisema yeye ndo waziri, Dk. Tizeba hana uwezo wa kuwatatulia wafanyakazi kero zao. "Hayo aliyoahidi alikuwa akifurahisha nafsi yake". Na kweli hakuna chochote kilichofanyika kwenye taasisi hiyo.

Mwakyembe Fisadi tu. Ila alikuwa akitumia media ili aonekane anafanyakazi, Lakini ukweli uliopo ni kwamba TPA, TAA, SUMATRA amekuwa akijichotea pesa. Alioondosha uongozi wa taasisi hizi na kuweka watu wake ili kufanikisha ufisadi wake: Huyu nifisadi anayepaswa kuchunguzwa.

Hizo unazosema ni porojo tu..... bado hujaonesha Mwakyembe kachota wapi pesa na vipi amechota!!!!!??????
Kusema tu alichota pesa pale SUMATRA, TPA kwa mtu makini hawezi kuamini moja kwa moja..... maana kujataja kafisadi kule mara hapa kwenye miradi ya kifisadi (bila ya kutaja hata mradi mmoja alioufisidi na jinsi alivyofisidi) hata ushahidi mmoja. hujaweka...
 
Naona wezi wa makontena na vifaa vya magar pale bandarini wanashangilia.

Ama ukiangalia andiko zima la mtoa mada, 95% ni majungu matupu!

Kwa miaka ya hivi karibuni, Waziri Mwakyembe ndo angalau kaleta tija pale Uchukuzi. Kasi yake na umaarufu ulikuwa juu kabisa na ndo maana waliokuwa chini yake na ulegelege wao waliomuona yeye ni CEO, lakini ukweli utakuwa ni kuwa kasi yake haikuwa sawa na hao wa chini yake yaaan Naibu Wake na Katibu Mkuu wake, hiyo ndo tafsir rahisi kabisa!

Anyway ngoja tuone kama wizi pale bandarini utakoma au ndo tunarudi tulikotoka.

Katika muda uliobaki, hakukuwa na TIJA kwa TAIFA kubadilisha sehem ambazo hazikuwa na shida, ni kuyumbisha mambo tu. Miez yenyewe iliyobaki ni hardly 7 tu ili ije serikali mpya. Inashangaza kwa kweli!
 
Wameogopa kashfa ya mabehewa hewa ya Mwakyembe na Sakata la Sukari.

Kwa kumuondoa Chiza.

Hakika maCCM hamtapona kwenye hili
 
Mimi binafsi namkubali sana Mwakyembe, huyu jamaa alikuwa mwiba mkali kwa mafisadi pale bandarini. Kwa muda mfupi ameifanya bandari yetu kuaminika kwa watumiaji kutoka nchi jirani waliokuwa wamehamia bandari ya Mombasa. Pia amewezesha mapato ya bandari kuongezeka ukilinganisha na hali ilivyokuwa mwanzo. Chini ya Mwakyembe ikitokea hata taa ya gari la mteja imeibiwa ni lazima bandari au kampuni iliyohusika ilipe mara moja, ama kweli bandari yetu ilianza kuaminika.

Bila shaka sasa wafanyakazi wa bandarini watakuwa wanafuraha isiyo na kifani maana mwenye nyumba sasa ameondoka, kama Sitta asipokuwa makini ni wazi kuwa watu wataikimbia tena hiyo bandari kwa kuwa bandari yetu imejaa mchwa wa kutosha. Ukiagiza gari utakuwa huna uhakika kama utaipata ikiwa na taa zake kama. Pia ni vigumu kuwa na uhakika kama kontena lako kama litafika salama

Kabla ya kuja Mwakyembe, hata mfumgua geti la Bandarini alikuwa anatembelea magari ya kifahari, maana ili upitishe bidhaa za wizi ni lazima umuhusishe mlinzi wa getini
 
Back
Top Bottom