Ukistaajabu ya Escrow utaona ya Mwakyembe

Ukistaajabu ya Escrow utaona ya Mwakyembe

Wadau mbalimbali wakiwemo wasomi, wachambuzi wa masuala ya kisiasa na wananchi wameonyesha kutoridhishwa na uteuzi alioufanyavrais Kikwete ikiwemo kumhamisha dr. Harrison Mwakyembe kutoka wizara ya uchukuzi hadi wizara ya uhusiano wa Afrika Mashariki kwani aliimudu sana nafasi yake.
Source: Magazeti ya leo: Mwananchi, Nipashe...
 
Mwakyembe alisababisha sembe tusipitishe kiurahisi si unajua uchaguzi mku unakaribia?kimbelembele chake kujifanya mchapakazi kimemponza,amewekwa 6 kwa kazi maalum baada ya kufanikisha letu la katiba hahahahaaa!!!
 
amani kwenu wadau,hivi kuhamishwa kwa mwakyembe kuna tija kwa taifa?maana katika serikali ya kikwete nilimchukulia mwakyembe kama waziri aliyekuwa anafanya kazi kwa viwango.ni chini ya dr mwakyembe tumeona mabadiliko na mageuzi makubwa wizara ya uchukuzi hususan kwenye bandari ambayo mimi na ichukuli kama moja ya nguzo za uchumi wetu.je kwa maamuzi yaliyofanywa na rais ya kumhamisha yamelenga kuleta ufanisi kwenye moja ya wizara nyeti hapa nchini?nawasilisha
 
Kila binadami ana mapungufu yake piA mtu anaweza kufanya mambo mazuri ktk jamii ili kuficha uovu anaoufanya kwa jamii
 
Kila mtanzania atakubaliana na mimi kwamba katika kipindi cha muda mfupi ambapo Dr. Mwakyembe amekaa katika wizara ya uchukuzi amefanya kazi nzuri kuanzia bandari hadi uwanja wa ndege.

Zile kelele za Tanzania kuwa kinara wa madawa ya kulevya na JKN International Airport kuwa kitovu cha upitishaji wa madawa ya kulevya hivi sasa zimekwisha kutokana na kazi nzuri ya Mwakyembe. Sasa hivi ukiachilia mbali matatizo ya system utoaji wa mizigo bandarini umekuwa na unafuu sana, huku wakwepa kodi huko bandarini wakiwa katika wakati mgumu. Ni wazi na dhahiri kwamba waziri Mwakyembe amefanya mageuzi makubwa katika wizara aliyokuwa anasimamia.

Lakini inashangaza sana kuona kwamba baada ya ufanisi huu wote, Rais Kikwete, ameona vema kumtoa Mwakyembe katika wizara hii na kumpa Samwel Sitta ambaye kiujumla hata huko wizara ya Afrika Mashariki ame-underperform.

Ni nani asiyejua kelele za Sitta na kauli zake wakati wa mgogoro kati ya Kikwete na Kagame? Mtu asiye na uadilifu katika wizara isiyo na kazi kama ya Africa mashariki atawezaje kubeba mikoba ya Mwakyembe kuwakabili wauza Unga wenye nguvu na mtandao mkubwa? Napata taabu kuamini kwamba mabadiliko haya ni ya kawaida.

Nashawishika kuamini kwamba Mwakyembe amemvurugia Kikwete biashara zake za madawa ya Kulevya. Maana wote tunajua kwamba Kikwete alipoingia madarakani alituambia anayo majina ya wauza unga, na hadi leo hajawahi kuyaweka hadharani wala kuchukua hatua za kuwakamata hao wauza unga anaowafahamu kwa majina. Ni dhahiri kwamba watu hawa waliingia naye ubia. Na kitendo cha Mwakyembe kusimama kidedea dhidi ya biashara hiyo kinaweza kuwa kimewakera washirika wa Kikwete katika biashara ya madawa ya kulevya na kumshawishi amuondoa.
 
Mwakyembe alisababisha sembe tusipitishe kiurahisi si unajua uchaguzi mku unakaribia?kimbelembele chake kujifanya mchapakazi kimemponza,amewekwa 6 kwa kazi maalum baada ya kufanikisha letu la katiba hahahahaaa!!!

Nahisi huu ndo ukweli wenyewe!
 
Ukweli ndio huo mwakyembe alikomesha hata uingizaji wa makontena bila kulipia,hawa home shopping center bandani ilikuwa mali yao.
 
Sembe zinapita kama kawaida wapendwa hakuna jipya.

Huyu aliharibu juzi aliposema atadili na mabehewa mizigo ianze pelekwa mikoani na treni; alipoulizwa vipi malori akajibu utumbo tutakaa nayo tuwaambie treni tunafikisha mzigo hapa, kuanzia hapa muanze kubeba mizigoyenu weeewee.

Asilimia50 ya wakubwa wanaishi na malori ya mizigo rest sembe unahisi wangemuacha never,,, ila ni fundisho ukipewa uwaziri hata kama unafanya jambo jema kuwa msiri sio unaropoka kila sehemu.

Alikuwa na uwezo wa kufanya haya bila ya kujulisha umma alipojitangaza akatoa aina ya silaha kwa maadui wakamshugulikia na ak49
 
Nadhani kila kitu kinakwenda kwa walivyopanga kuhakikisha masilahi yao yanabaki kama yalivyo maana wameshaathirika na biashara zao za kishetani
 
Ni kikubwa kipi Dr Mwakyembe alikifanya Wizara ya uchukuzi ambacho Sitta kitamshinda?
 
Akataka tutamrudisha Bungeni kwa chama tofauti ili atusaide kutekeleza yale aliyokusudia kwa kushirikiana na serikali mpya.
 
tatizo aliziba mianya yote ya kifisad, aliwazibia hata wakubwa kupitisha mirung yao ambayo ndo inawaweka mjini.

CHEZEA MIRUNGI WEYE

wamwemeka wazir MDEBWEDO-6- ili mambo yawe kama yalivyopangwa, ili pesa za uchaguz mkuu zivunwe kwa biashara ya mihadarati kwa kipind hik muhimu,
MWAKYEMBE MSHENZ SANA ANABANIA MPAKA WAKUBWA ZAKE DILI (HARAM) ZENYE MKWANJA MREFU???
BORA AENDE EAC TUMTUMIE HUYU 6 KUFANIKISHA DIL ZETU ZA SEMBE.
 
Prosoferi alimuondoa Mwakyembe then jioni yake akapita airport kwenda huko .......ipo shida?
 
Magazeti kama nipashe nalo gazeti kusoma mtu mwenye akili na kulichukulia kama chombo cha maana cha kutoa tarifa kwa umma wakati huandika kwa matakwa ya mengi.
 
Back
Top Bottom