mfianchi
Platinum Member
- Jul 1, 2009
- 12,169
- 8,941
Penye kustahili sifa wacha mtu apewe sifa,pamoja na yote Mwakyembe kafanya kazi kwa uadilifu na dhamira kwenye wizara ya uchukuzi,wanofurahia kuondoka kwa Mwakyembe wizara ya uchukuzi hasa wale wa TPA nadiriki kusema ni wezi na wala rushwa waliokubuhu,kabla ya Mwakyembe pale bandarini palikuwa kama pango la wala rushwa,kwa msafirishaji yoyote wa mizigo hili analifahamu na sio siri,na kwa hilo Mwakyembe alijiwekea maadui wengi akiwemo yule wa Home Shopping Centre na balozi wetu mdogo wa Guazhong,yale makonteina yao yaliyokuwa yanapita bure ikawa mwisho.Kilichonishangaza ni uamuzi wa JK kumchomoa mtu ambaye alikuwa mchapakazi kwenye wizara nyeti na kumleta Mr porojo,halafu matokeo yake mapato yanashuka chini tunaanza kumtafuta mchawi,sana sana mi ningekuwa ndio mwenye dhamana ningempeleka wizara ya Nishati na Madini