Ni toka kwenye nukuu ya Mwl nyerere aliposema kuwa siku akiona wazungu wanampenda(hasa wamarekani) atajua kuna mahala kaanza kukosea...........sasa kwa hili la misaada kuzuia eti kisa zanzibar.....na kukaa kimya kwa marekani bila kutoa pongezi kwa magufuli jinsi alivyoanza ingawa benki ya dunia imepongeza na kutoa pesa kwa ajili ya mirad mbalimbali...........mabepari wameuchuna sababu wanaona zile enzi za kijamaa zinarud...zile enzi za rais kuwapenda wa tz kwa dhat kabisa, enzi za kushughurika na mambo ya wanachi bila kujipendekeza kwa wazungu.....enzi ya tanzania kuwa nchi yenye heshima........enzi ya tanzania kuanza kurudi kule ambapo wamarekani walikuwa wanakuogopa miaka yote.........kamwe marekani haijawahi wala haitawahi kuitakia mema nchinyingine....hasa afrika....zaidi ya kujali interest zake.........kwa historia ya tz tangu mwanzo na haya ya magufuli kwa sasa.....ni dhahili kuwa wamarekani wana hof ns tz ijayo na wenye akili hawashangai kwa lililotokea na tujiandae kwa mengine menhi zaid......hii ni vita ya ki itikadi sababu zingine ni mbwembwe tu!............Tusiogope dunia kwa sasa imebadilika sana...hao wamarekani hawana chao kwa sasa na kamwe hawatafanikiwa katika hii vita na tz.....magufuli upo sahihi na kamwe usirudi nyuma......"mbele kwa mbele"
Pamoja na hzo sababu ni za msing sana,lakn dalili hata kupongeza kuwa rais NO! Dr.uwe mjanja km sungura
Awe mjanja kwa Marekani? Tuna nini sisi!?
Wamarekani wanajaribu kuweka shinikizo kwa faida yenu watanzania ila watanzania wenyewe hata hawaelewi.Sheria ya mtandao ni mbaya kwa wananchi wa kawaida.Demokrasia imepokwa Zanzibar.Huhitaji kuwa na shahada kung'amua haya.
Ndio maana kipaumbele cha Lowassa kilikuwa Elimu Elimu Elimu.
Ni 'theory' kwa hiyo uko sahihi na pia umekosea.Wakati mwingine keep your mihemuko to yourself huna proof.
Kwan magufuli ana fikra za kijamaa?...kama zipi hasa?...kubana matumiz!?..kwan ni nchi za kijamaa peke yake ndo hiwa zinabna matumiz?...Na pia kwan ni nchi za kijamaa peke yake ndo zinapambana na ufisadi....Wazir mkuu mstaafu wa israel yuko jela 3yrs kwa ufisad..je israel n nchi ya kijamaa?...Hizo fikra za kijamaa ni zipi hasa unazozisema
😅😅😅😅😅 Marekani imchukie Magifuli ili iweje mkuu. Hebu kuwa na fikira huru. Hayo unayoyasema kwa sasa hayawezekani, yanahitaji muda kujipanga si kukurupuka. jembepori
Never on earth marekani hawezi kuwa rafiki mwema kwetu na hajawahi .
Eeeh baba Mungu umjarie kipenzi rais wetu Magufuli afya njema ,aivushe Tanzania kwenda kwenye uchimi wa kati.
Muuongoze aiongoze nchi yetu na Africa pia.
Hiyo imekuwa tabia ya wamarekani na mabepari duniani. Angalia Libya, Syria, Iraq(wakati wa Saddam). Kama nchi yako iko na resources ambazo kwao ni valuable na kama upo strong hutaki resources zako ziondoke bure, lazima Marekani, Ufaransa, Uingereza waingilie kati.
Tofauti kati ya Marekani na China ni kuwa, wachina wao hawaingilii politics za nchi wanazofanya nao deals, while Marekani anapenda kukuingilia, kudhoofisha utawala na kuchukua chake.
Hakuna watu wabaya duniani kama whites, they're hypocrites. Akikuchekea unaweza kudhani yupo nawe, Kumbe yupo kwa interests za nchi yake. Na kama nchi yako haina kitu, hutamuona.
Pengine hata Nyerere hakuwa sahihi! Kweli urafiki wa J Kenedy kwa Tanzania ulikuwa wa kinafiki? Fikra pevu hudai utafiti kwanzani kweli tupu ndugu yangu.naanza kuwachukia hawa wamarekani. bora tujiendee china au russia ingawa russia watakupenda wakiwa wanahitaji chochote kwako.
wamarekani wanafanya kwa faida ya nani?, kwani huko zanzibat maalim seif kaanza kuibiwa leo.....mbona miakayote walikuwa wanatoa misaada? kwa nini iwe mwaka huu tu?, halaf hili la mitandao...sisi tupo hapa jf na watu wanatukana tu na hiyo sheria siipo?.......hivi ingekuwa mbaya kiivyo watu wangeporomosha matusi ya ajabu hum jf......hebu tuachebushabiki......sasa hilo la elimu ya lowassa limekujaje kwenye hii mada?...
Una historia gani ya kuwa sahihi tangu dunia imeumbwa. Si ungekuwa na mchago wowote katika dunia hii?
Huna mchango na hujulikani na wenye dunia hii kama akina Marekani, UK, ICC, ICJ nk.
Magufuli anaonewa tu. Uchaguzi zenj ulifutwa wakati Tanzania na dunia haijui kama Magufuli ataibuka kidedea. Marekani wana yao. Mbona wanamwaga hela kwa kagame. kweli uhuru wa habari au mtandaoi uliopo tz unaweza kulinganishwa na hali halisi huko Rwanda. Thubutu. Mleta uzi huu uko sahihi. Kiongozi yeyote hasa Afrika akionekana anaelekea kutekeleza dhana ya kujitegemea lazima anunuwe. hoja hapa siyo ujamaa, bali kujitegemea. Mbona serikali ya uturuki inawadhalilisha wakurdi utadhani siyo raia wa taifa hilo lakini Marekani na mrafiki zake wanaendelea kuiunga mkono serikali hiyo na kuimwagia misaada. Hizi double standards hazina tija. ni wakati Waafrika tujitambue.