Ama wasemaje Kaunga,yupi asali ya moyo?,
yule anayejigonga,au mwenye hisia za choyo?
Mapenzi ni kuungaunga,siyo ndiyo siyo siyo
Usiyachunguze.
Eti nisiyachunguze?Rudia tena nisiyachunguze?
wasemaje...nisiyachunguze!
Akisema nakupenda, hewala kwa muungwana,
ushahidi kakupenda, anajua maulana,
kuchunguza kakupenda, huko ni kutafutana
Usichunguze
Siyo rahisi kujua kilichoko ndani ya moyo wa mwanadamu
Mara nyingi kauli hupimika lakini kamwe siyo dira ya ukweli
Jicho laweza kurashiarashia nia lakini siyo kisemea moyo
Tabasamu laweza kukutikisa lakini lisitoboe la moyoni
Walakini magoti yanapomgonga-gonga jua kweli anajigonga.
Kilichoko moyoni ni kificho japo chakuchungulia-chungulia!
Mtihani wako ni kutafakari moyoni kwake kuna nini lakini?
Lengo ni kuujua moyo wake ili uthibiti hila kama zipo
Mwanadamu asilia yake ni usiri na usibwatuke na siha...
Walakini magoti yanapomgonga-gonga jua kweli anajigonga.
Moyo wa mwanadamu ni pasua kichwa na hata mmilikiwe kuzuzuliwa!
Anachodhani kipo moyoni leo, kesho kukikana yeye mwenyewe!
Moyo wa mwanadamu ni kizungumkuti kamwe usiuamini!
Kwani umekithiri hila na vitimbi, hivyo, kuwa tatanishi!
Walakini magoti yanapomgonga-gonga jua kweli anajigonga.
Mwanadamu hapendi kuanguka hivyo magoti kuyalinda vyema.
Sasa magoti yanapoweweseka ujue umemshika pabaya.
Hana ujanja wa kujitunzia siri hapo kwani hata wewe shahidi.
Chunga magoti yake na wala siyo moyo wake kuujua undani wake.
Walakini magoti yanapomgonga-gonga ujue kweli anajigonga.
Magoti yakigongana mbele yako ujue hana ujanja tena kwako.....
Na ya kuwa umemtia kabali na kibanio hicho hatoki kamwe!
Kufurukuta kamwe hawezi na saa ya kumkokota imewadia..
Mpeleke kichinjioni ili ufaidi kitoweo kabla hajageuza somo!
Walakini magoti yanapomgonga-gonga ujue kweli anajigonga.
N.B Haya siyo mashairi bali ni tenzi za nyimbo...........kwa hiyo hakuna swala la vina kushahibihana n.k kama ummu kulthum anavyopendelea na wengineo.....sentensi ya mwisho ni kibwagizo tu au chorus/kiitikio n.k
Ruta, kauga and kigarama mmenifanya nisahau mengi niwaze zenu fikira ambazo najiuliza huwa mnawezaje kuyapata haya mashairi? binafsi sijui hata kutunga kawimbo ka kumbembeleza mtoto u can imagine jins ambavyo nawafeel kwa haya mashairi. keep it up
Kaunga bwana, umeniacha nacheka,
kumbe umeshindwa vina,muwala ukaibuka,
Hoja zako si za tina, wala hazina shubaka,
Gangamala
ummu kulthum is too lovely and a hot subject for now...................sijui kama anahusika na huu uzi wa leo mie nimeutapika tu kwa manufaa ya jf nzima.......................ndetichia, si umeona rutashubanyuma anavyojitetea kama kuku mwenye mdondo?by the way kijana unanifurahishanga wewe,na mashairi yako yasiyo na vina keep it up!!!
gfsonwin sifa zako namba wani, haya si ya kustaajabu
Elfu huanza na namba wani, vijana nao huwa babu,
roho yako usihini, kushindwa nyambua silabu,
utaweza
Eti Rutashubanyuma, unajua wakufeel
nenda usirudi nyuma, usiache jambo hili
tunga tungo zenye nyama, zenye lugha si dhalili,
unapendwa
Nawe Kaunga, wenzio wakutamani,
wanataka kujiunga, waje kwako chamani
tatizo lao kutunga, wajue wafanye nini?
waeleze