Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Siyo rahisi kujua kilichoko ndani ya moyo wa mwanadamu
Mara nyingi kauli hupimika lakini kamwe siyo dira ya ukweli
Jicho laweza kurashiarashia nia lakini siyo kisemea moyo
Tabasamu laweza kukutikisa lakini lisitoboe la moyoni
Walakini magoti yanapomgonga-gonga jua kweli anajigonga.
Kilichoko moyoni ni kificho japo chakuchungulia-chungulia!
Mtihani wako ni kutafakari moyoni kwake kuna nini lakini?
Lengo ni kuujua moyo wake ili uthibiti hila kama zipo
Mwanadamu asilia yake ni usiri na usibwatuke na siha...
Walakini magoti yanapomgonga-gonga jua kweli anajigonga.
Moyo wa mwanadamu ni pasua kichwa na hata mmilikiwe kuzuzuliwa!
Anachodhani kipo moyoni leo, kesho kukikana yeye mwenyewe!
Moyo wa mwanadamu ni kizungumkuti kamwe usiuamini!
Kwani umekithiri hila na vitimbi, hivyo, kuwa tatanishi!
Walakini magoti yanapomgonga-gonga jua kweli anajigonga.
Mwanadamu hapendi kuanguka hivyo magoti kuyalinda vyema.
Sasa magoti yanapoweweseka ujue umemshika pabaya.
Hana ujanja wa kujitunzia siri hapo kwani hata wewe shahidi.
Chunga magoti yake na wala siyo moyo wake kuujua undani wake.
Walakini magoti yanapomgonga-gonga ujue kweli anajigonga.
Magoti yakigongana mbele yako ujue hana ujanja tena kwako.....
Na ya kuwa umemtia kabali na kibanio hicho hatoki kamwe!
Kufurukuta kamwe hawezi na saa ya kumkokota imewadia..
Mpeleke kichinjioni ili ufaidi kitoweo kabla hajageuza somo!
Walakini magoti yanapomgonga-gonga ujue kweli anajigonga.
N.B Haya siyo mashairi bali ni tenzi za nyimbo...........kwa hiyo hakuna swala la vina kushahibihana n.k kama ummu kulthum anavyopendelea na wengineo.....sentensi ya mwisho ni kibwagizo tu au chorus/kiitikio n.k
Mara nyingi kauli hupimika lakini kamwe siyo dira ya ukweli
Jicho laweza kurashiarashia nia lakini siyo kisemea moyo
Tabasamu laweza kukutikisa lakini lisitoboe la moyoni
Walakini magoti yanapomgonga-gonga jua kweli anajigonga.
Kilichoko moyoni ni kificho japo chakuchungulia-chungulia!
Mtihani wako ni kutafakari moyoni kwake kuna nini lakini?
Lengo ni kuujua moyo wake ili uthibiti hila kama zipo
Mwanadamu asilia yake ni usiri na usibwatuke na siha...
Walakini magoti yanapomgonga-gonga jua kweli anajigonga.
Moyo wa mwanadamu ni pasua kichwa na hata mmilikiwe kuzuzuliwa!
Anachodhani kipo moyoni leo, kesho kukikana yeye mwenyewe!
Moyo wa mwanadamu ni kizungumkuti kamwe usiuamini!
Kwani umekithiri hila na vitimbi, hivyo, kuwa tatanishi!
Walakini magoti yanapomgonga-gonga jua kweli anajigonga.
Mwanadamu hapendi kuanguka hivyo magoti kuyalinda vyema.
Sasa magoti yanapoweweseka ujue umemshika pabaya.
Hana ujanja wa kujitunzia siri hapo kwani hata wewe shahidi.
Chunga magoti yake na wala siyo moyo wake kuujua undani wake.
Walakini magoti yanapomgonga-gonga ujue kweli anajigonga.
Magoti yakigongana mbele yako ujue hana ujanja tena kwako.....
Na ya kuwa umemtia kabali na kibanio hicho hatoki kamwe!
Kufurukuta kamwe hawezi na saa ya kumkokota imewadia..
Mpeleke kichinjioni ili ufaidi kitoweo kabla hajageuza somo!
Walakini magoti yanapomgonga-gonga ujue kweli anajigonga.
N.B Haya siyo mashairi bali ni tenzi za nyimbo...........kwa hiyo hakuna swala la vina kushahibihana n.k kama ummu kulthum anavyopendelea na wengineo.....sentensi ya mwisho ni kibwagizo tu au chorus/kiitikio n.k