UKIMWI upo, tambueni thamani yenu

UKIMWI upo, tambueni thamani yenu

Nashindwa kuelewa clinic wanakuja kujua mama ana ukimwi miezi 7 baada ya kujifungua

Na wakati kipindi cha mimba unaanza clinic mke na mume au wachumba mnatakiwa kwenda clinic kupima HIV wote
 
Mkuu nimepitia maelezo yako lakini ni kama mchumba wako huwenda anahili tatizo kitambo na hakutaka kukwambia maana mwanamke akishapata ujauzito mwanzoni kabisa kliniki anachekiwa ili kujua status yake kama anatatizo wanaanza utaratibu wa elimu na kumsaidia asipeleke maambukizi kwa mtoto,sasa kwanini akae kipindi chote hadi ajifungue na anyonyeshe kwa miezi 7 ndio aache kunyonyesha na kukwambia?


Kuhusu wewe kutopata maambukizi huwenda huyo binti alijijua kitambo hari yake na akawa katika mpangilio mzuri wa dawa,wanadai mtu akiwa katika mpangilio mzuri wa dawa kwa kipindi cha muda fulani mwanaume akija kumwingia peku hawezi pata tatizo,hebu fanya kuchunguza.
Nakazia
 
CD4 zipo vzr japo hataki kuanza dawa na hajajikubali kwasababu hakutegemea kama jambo hili halijatoka kwangu, bado ni changamoto japo ni miaka 5 sasa
Mkuu unamaanisha hili liligundulika maka 5 iliyopita na mkeo hajaanza dawa za ARV?
 
Mpenzi wangu wa sasa ndio wa kwanza ananisisitiza niende nae kupima. Ananipenda sana ila nafsi yangu inasita kweli kwenda pima.
Wiki hii napiga moyo konde naenda ila siendi nae, nitaenda kivyangu kwanza kisha majibu yakiwa mazuri nitamchukua nikapime nae sehemu nyingine.
Majibu yakiwa mazuri NAAPA nitaanza kwenda kanisani na nitamuoa huyu binti anayeonekana kunijali na nitatulia nae na pia nitaanza maisha mapya kwa kuachana na marafiki zangu wa sasa ambao kwa kweli sio wa kuwa nao. Nitabadili namba za simu na kuhama kabisa hata mkoa na kwenda anza "upya". Kuhama sio ishu, bado nitakapohamia nina mizizi hivyo haitakuwa ngumu. Kikubwa hili genge langu haliwezi fika huko. NIMEDHAMIRIA, MUNGU niongoze.
Ameen mkuu
 
Utaifurahisha jamii kwa story za maradhi? Waliosoma vema kwa utulivu wameelewa, endapo haukuelewa uandishi wangu ungeuliza au kutazama maswali ya kundi lililoelewa na namna ninavyojibu bila shaka ungepata majibu. mimi si mzuri katika uandishi. asante
Nimesoma comments zake zote jamaa anajichanganya Sana ni stori tu aliyoamua kuja kuifuraisha JF.

Ulichouliza ndicho kilichomuumbua, mjamzito akishafungua kadi hapo hapo wanampima HIV.
 
Sidhani kama kuna lolote, kwasababu kama malaria napata, flue napata, typhoid pia napata hivyo sioni kama kuna kinga yoyote ya tofauti.
Group O lina siri gani kwenye suala hili?
 
Back
Top Bottom