UKIMWI unavyotafuna vijana

UKIMWI unavyotafuna vijana

Ukimwi unaua Sana , tena unakata ghafla tuu, we ukisikia mtu amekata ghafla et Kwa ugonjwa wa mda mfupi, pigia mstari ngwengwe hiyo, Ephraim Kibonde in advance, na huyo bi mdada wa Cheka tuu

Kwa hiyo yule dogo Mbosso naye tayari kashaingizwa kwenye +grid ya dunia?
 
Aisee natamani kama serikali na wizara yake ingetilia mkazo hili swala kama kipindi cha miaka ya nyuma,kulikuwa na warsha na makongamano mijadala kuhusu UKIMWI,matangazo kila stesheni za TV na radio ,watu walikuwa na uelewa mpana zaidi namna ya kujikinga na namna ya kumhandle mgonjwa wa VVU,aisee asikwambie mtu huu ugonjwa upo tena si kodogo, si watoto watoto wala watu wazima,tena vijijini ndo usiseme si ajabu kukuta nusu ya kijiji wanatumia dawa na hao no waliojitokeza kujua hali zao na kuanza dawa,sawa juhudi zinafanyika kuwasogezea huduma na kuwappa dawa za ARV lkn elimu bado iko chini sana kuwakinga ambao hawajapata maambukizi haswa vijana walio katika mazingira hatarishi.Ila for sure hali ni tete
 
Sawa, ila unaweza kujenga hoja bila kutaja waliotangulia mbele ya haki.

Tuwe na staha hasa kwenye kunyooshea wenzetu vidole wakati nasi tuna makandokando yetu.
Mkuu kutaja ma celeb na mastar ndio kunasaidia kuelimisha wengine kwani wao walikuwa kama mfano,kwa hiyo kutangaza au kutaja majina sio kukosea waliotangulia mbele za haki,hakuna sheria inayosema tusiwataje marehemu kwa maradhi yaliyowapeleka kaburini,sote tunapita ta hapa duniani lakini lazima pia tuelimishane kwa ajili ya faida ya vijana wanaokuja nyuma yetu,ndio maana hata kwa walioendelea hawa ma celeb hujitaja au hutajwa kuwa ana grid ya taifa ,si dhambi na tukizingatia kuwa ugonjwa huu phuchangiwa sanana mambo ya ngono ingawa kwa kiasi kidogo inaweza ikawa kupewa damu isiyo salama.
 
Maoni yangu! Kuna ugonjwa hatari sana kwa sasa ambao unaua kwa kasi kuliko hata ukimwi, nao ni HOMA YA INI.

Tofauti na HIV, virusi vya homa ya ini vinasambaa kwa njia rahisi sana, mfano jasho, mate, damu, nk.

Mbaya zaidi, virusi vya homa ya ini vikiwa sugu lazima ufe, tofauti na HIV ambapo kuna ARV, ukizingatia masharti unaishi miaka mingi tu.

Homa ya INI ni tishio kuliko HIV
 
Hakuna wakati mgumu kwa mgonjwa wa ukimwi kama wakati wa kudungwa ile sindano ya damu ya viral load, huwa nawaonea huruma sana.

Vijana jitahidini mjilinde acheni ngono zembe ukimwi Upo na unatisha kuliko unavyofahamu.
Ipoje hio sindano mkuu? Ni kubwa sana au embu tupe habari yake..kidogo
 
Back
Top Bottom