UKIMWI unavyotafuna vijana

UKIMWI unavyotafuna vijana

Siri nzito inayopelekea UKIMWI kutmalaki ni jambo moja tu, with kutangaza ugonjwa tofauti hasa wakati wa kusoma historia ya maremu, tungetangaza kuwa marehemu kaondoka na ngwengwe mke na michepuko yake isingeguswa na HIV -ve, TUPIMWE WOTE KISHA ATAKAEKUTWA POZITIVU APIGWE CHAPA KWENYE TAKO NA ITANGAZWE ILI KILA ATAKAEKUWAA MIADI KABLA YA KUTUMBUKIZA MBOYOGO a.k.MKUYENGE NI LAZIMA TUCHUGULIANE MAKALIONI
Naamini huu ushauri murua wizara husika itaufanyia kazi. Inabidi tupigwe chapa kama ng'ombe.
 
Mnajua hata maana ya ukimwi nyie??
Upungufu wa kinga mwilini ni ishu ya kawaida.
Ukila balanced diet, ukifanya mazoezi fresh na kutunza mwili wako ukimwi unapona.

Tangu lini ukimwi ukaambukizwa?
watu wanaupataje?
 
Ukimwi unaua Sana , tena unakata ghafla tuu, we ukisikia mtu amekata ghafla et Kwa ugonjwa wa mda mfupi, pigia mstari ngwengwe hiyo, Ephraim Kibonde in advance, na huyo bi mdada wa Cheka tuu
Kabisa yaani. Huyu Martha binti mdogo namna hii kafa kwa ngwengwe. Ataondoka na wengi.
 
Hakuna wakati mgumu kwa mgonjwa wa ukimwi kama wakati wa kudungwa ile sindano ya damu ya viral load, huwa nawaonea huruma sana.

Vijana jitahidini mjilinde acheni ngono zembe ukimwi Upo na unatisha kuliko unavyofahamu.
 
Na mm nishasema hivyo na hata nikienda kufunga ndoa kanisani wakataka wanilazimeshe nipime kwanza nitaachana na huo mpango wa ndoa.Sitaki stress mimi kama ni kufa kupo tu kwa nini uanze kuishi kwa mashaka.
Mimi nilikwisha vunja uchumba Mara 2 kwa issue za kulazimishwa nikapime. ivi napima ili iweje kwamba nikikutwa nimenasa napewa dawa napona au ndo kupeana mavidonge ya homa ya ini alafu tunadangwa eti zinarefusha maisha kwa wagonjwa was ukimwi. Mara nyingi ma Dr wanachanganya majibu anakupa mengine unaanza kuishi kwa mawazo vyakazi gani si bora niishi kwa amani nikiamini Niko fiti ikitokea basi ni ajari za kawaida kifo kipo hakikwepeki ata ukipima kila wiki utakufa
 
kwakweli ulilosema ni sawa kabisa ni haki yako kusema kwani sasa tunahitaji watu wasemakweli wanoona mbali. ukweli ni kwamba ukimwi upo na hauna dawa zaidi ya hizo Arv za kusukuma siku tuache utani kwenye hili jambo vijana wengi wa sasa sio wazima tena wanaishi kwa matumaini na wengine ni watu wazima wenye ndoa zao lakini bado wanasambazia watoto maradhi kwakweli Mungu aingilie kati ifike mahali watu wote walione hili ukifanya mzaha basi hata kwa mtoto wako litakuja kama sio kwako basi kwa ndugu yako pia. huku tuendako ukibahatika kupata mtu salama ukazaa naye mtoto mmoja aliyesalama basi mshukuru mungu manake hali inatisha. UKIMWI UPO NA HAUNA DAWA. msidanganywe wenye ndoa zenu tunzeni na wasiokuwa na ndoa basi ukipata mtu sahihi mpime. usidanganywe na utajiri wala pesa za mtu watu wana mihela lakini yote inaishia kwenye kubadilisha madamu na maARV tu sasa kwanini usijichunge? bora ule mchicha wako wa mia mbili ukaishi maisha safi ya amani kuliko kuwa na mahela yanayoishia kwenye madawa. hebu shtukeni wenye pesa zao wanaendelea kusambaza kwa nguvu na kwa makusudi kabisa ili wasife wenyewe matokeo yake mwenye pesa anaua watu 100 wakati yeye bado anadunda kisa ana pesa za kumsogeza kwa kubadilisha damu.
 
alafu siku hizi wamerahisisha sana maisha kwa hizi propaganda zao yan hawa wazungu hawa Mungu anawaona....utasikia Ukimwi siku hizi sio ishu tena ukiathirika una anza dozi tu mambo safi then na hii kusema ni ugonjwa wq tatu kupoteza watu nayo inapoteza attention kwake.. kiasi cha kuwa fumba macho wengi na kujisahahu
Miaka kumi ijaoyo watu maarufu na vijana wanaoonekna nyota wengi watakuwa wanaishi kwa matumaini
Nijambo ambalo sio siri na nina dhani Serikali pitia idara nyeti ya taifa kiusalama ni muda mwafaka wakaliangalia hili kwa macho sita watu wanakufa na ukweli hausemwi ila walio na macho ya mbali watakubaliana nami 99% ya vijana na watu maarufu nyuma yake kuna siri ya hiki kirusi ila hakuna anayesema tunaishia sema malaria na UTI kali.

Tunasahau kuwa kushuka kinga ya mwili huleta hayo magonjwa kwa kiwango kisichodhibitika.

Nani aliokoe taifa nani asimame kuwaambia vijana na watanzania Ukimwi unatumaliza silence na kesho yetu ni ya mashaka.
 
Ukimwi unaua Sana , tena unakata ghafla tuu, we ukisikia mtu amekata ghafla et Kwa ugonjwa wa mda mfupi, pigia mstari ngwengwe hiyo, Ephraim Kibonde in advance, na huyo bi mdada wa Cheka tuu
Umekaa kimbeya mbeya boss...tuwekee vyeti vyao vikionyesha ni +ve
 
Acha kabisa tena hawa jinsia KE akiwa na maradhi unaeza usijue unapiga mchomo kuibuka una kitu kingine...
nilikua mgumu wa kutumia kinga ila sasa hivi aisee, nmeanza kutumia kwa kuogopa magonjwa sitaki mipango yangu ikwame kisa kudhoofika na maradhi labda uzee panapo majaliwa
 
Siku hizi Kampeni ni "Visa Vi " hawaelimishi tena wana rahisisha mambo kuwa Ukimwi sio wa kuogopwa ni wa kawaida tu
Limeshakuwa gonjwa la kawaida tu sasa. Hivyo ndivyo jamii inavyofikiria, which is wrong. Hata kampeni elimisha zimefifia sana.
 
Hizi takwimu za kuletewa na wanao tuletea haya magonjwa kuna mda siziamini kabisa
Acha porojo, hii ndo shida ya watanzania mkisoma vijarida vya udaku mkaona kwamb kuna vifo vya ghafla bas mnachukulia wote ni ngoma

kitakwimu marelia inaua kuliko ukimwi na hatujaisha, ko mawazo haya yanabaki mawazo ya vijiweni
 
siku nikifanikiwa kupima Ukimwi alafu sina basi ntatulia sana, tatizo kila nikitaka kupima uoga wa hali ya juu unanijia sijui nitumie mbinu gani.
hahahaaaa ilo tatizo linawakumba wengi mi niliwai kupima 2014 nikakimbia majibu sasa nasubili mpaka dawa ipatikane ndo nikapime. Kwanza sina history ya kuugua hovyo hovyo kwaiyo Niko safi
 
Back
Top Bottom