Unamwona mtu kakonda lakini gafla unaona tumbo limetoka kubwa kweli kweli na kajasho eti ni kitambi,,,,,, anaijua siri yake na madawa anayotumia badala ya kutulia na kumuomba mungu amjalie maisha marefu yasiyo na dhambi basi ndio anafungulia mbwa sasa, vitoto vidogo maskani viwanafunzi nyumbani unakapenda na wala hujui kuwa kalishaanza jinsi kanavyozuga kana heshima nyumbani kumbe kalishaharibiwa na mdudu kashapewa, My God, unakuta na vijana wa umri wake nao wanakafukuzia wanafikiri ni katoto kenzao kumbe lo!!! kanao nako kanawagawia, wanavunzi wa vyou vikuu tamaa ya anasa, maisha ya kujirusha na kutaka kumiliki vitu vya garama mnakwisha na akili zenu. Unakuta mdada ana akili kweli darasani lakini mwili wake kauachia kama "open cheque" anamaliza chuo anaajiriwa maskini vijana wa mtaani wanaanza kujigonga "boss lady" wote wanagawiwa, sasa elimu uliyokuwa unaihangaikia tangu ukiwa chekechea ndio unaishia wapi? vipi wazo la kuwa na familia, mipango endelevu ya kuwatunza wanao na wazazi wako huku umeshaugua kwa ajili tuu ya kushindwa kuzuia tamaa za mwili!!!! tafakari chukua hatua