UKIMWI umeua wengi jamani

UKIMWI umeua wengi jamani

Ushauri mzuri ila ugonjwa wenyewe umekaa sehemu mbaya sana. Kama mtu akishindwa kuvumilia basi kinga zipo.
 
Acheni ngono zembe na mkiweza msubiri,Mi sasa hivi nshaamua sidate na mwanaume hadi tukapime..Maana kuna watu nliwahi kuambiwa wameathirika sikuamini..Sasa ntajuaje kwa mtu wa kukutana nae njiani??
twabd tupme wote
 
Nadhani Avata yako (Profile Picture) inakinzana na mada nzuri uliyoianzisha. Hivi itakugharimu chochote kubadili hiyo picha? Ahsante
Ngono zimetawala mno vichwani mwa watu wakubwa kwa wadogo wengi wanaangamia kweli UKIMWI umeteketeze dunia. Mapenzi mapenzi jamani, usaliti katika ndoa, ajali, starehe na tamaa za hii dunia zinatumaliza, ukosefu wa maarifa na dhambi ni adhabu kwetu. Mshahara wa dhambi ni mauti, chuki na visasi aaaah ndugu tusameheane yaishe.

Tuwe na kiasi pia turidhike na tulichopewa/tafuta/barikiwa maisha ni kuridhika. Wangapi wamekufa wakaacha mambo ya dunia hii? Vishawishi na vishindwe kwa jina la Mwenyezi-Mungu daima tuvitawale pamoja na hisia. Kwa kujiweka salama tujilinde wenyewe tumkabidhi Mungu wetu maisha yetu kwa kila hatua tunayofanya.

Ushauri wangu kwenu wana MMU.
 
Binafsi namuonea huruma sana anaeambukizwa Ukimwi kwa bahati mbaya au makusudi kupitia vitu vyenye ncha kali au kuongezewa damu, kundi jingine ni lile la wanaoletewa na wenziwao wakiwa wamejituliza kwa uaminifu ktk mausiano au ndoa. Ila hili kundi la wanautafuta kwa tamaa zao za kimwili, wacha wafe maana wanavuna walichopanda.
 
Ni kweli bt dunia ya sasa imeoza hii[emoji134]
Juzi tu hapa kuna wapenz walipima wakafunga ndoa baada one year mke kashika mimba kwenda kupima clinic wanaambiwa unao njoo na mmeo tukushauri jinsi ya kumlinda mtoto hadi azaliwe salama..Huyo sio mlokole huyo alikuwa chui kwnye kundi la kondoo,walokole wenye hofu ya Mungu hawawezi kufanya hayo acha kusingizia watu
akawekwa kikao akakiri alikua na bwana mkoani na akienda anafanya yake Tena walokole atiii...sasa mi nkiolewa na huyu mwenye mambo ya kidunia itakuwaje? naogopa
 
Hata ukosefu wa fedha pia unaangamiza watu wengi sana... Umasikini ndiyo usiseme, kila sekunde unaua mtu...
 
Acheni ngono zembe na mkiweza msubiri,Mi sasa hivi nshaamua sidate na mwanaume hadi tukapime..Maana kuna watu nliwahi kuambiwa wameathirika sikuamini..Sasa ntajuaje kwa mtu wa kukutana nae njiani??
bado sio suluhisho huyo uliemchagua kuwa muneo/mkeo anaweza kukuletea bado hali ni ngumu kikubwa tujikabidhi kwa Mungu kwanzia sasa.
 
Kweli ukimwi ni biashara maana tangu uingie duniani hakuna hata dawa ya kuponyesha. Ila tuwe makini sana na huu ugonjwa upo na unaua.
 
Nadhani Avata yako (Profile Picture) inakinzana na mada nzuri uliyoianzisha. Hivi itakugharimu chochote kubadili hiyo picha? Ahsante
hapana mkuu kikubwa tuweze tu kukubali hali halis na mihemuko yetu najua hapo uko hoi ila sina nia mbaya. accept the challenge you wilk win na sio kukumbia tatizo bali tatua ili siku nyingine ukikumbana nalo lisikusumbue.
 
Kweli ukimwi ni biashara maana tangu uingie duniani hakuna hata dawa ya kuponyesha. Ila tuwe makini sana na huu ugonjwa upo na unaua.
jifanganyeni tuu kwa imani zenu za kipuuzi cancer
nayo ni biashara eeh? wangap huko majuu wana ugua wasanii kama eazy e marehemu, dada yake mariah carey, magic johnson, yule mkali wa pop prince aliekufa juzi. wengine kibao umeshuhudia kwa
macho yako kweli wadhubutu kusema ukimwi haupo
haupo?? ukikupata ndo utaamini poor you shame on you na akina deception kwa kudanganya uma lazima tutoe elimu na onyo anaepita huku ajifunze.
magonjwa mangapi hadi leo hayana tiba it means nayo ni biashara??? by the way pray hard unatatizo kubwa sana wewe na Mungu akuondolee hilo tatizo
ufunguke kichwani.
 
Mhhh. Nafikiri hujaelewa hata wewe Mungu akusaidie. Mwisho nimesema "Tuwe makini sana na huu ugonjwa upo na Unaua" Ila siwezi badili mawazo yako. "Mbuzi na Kuku"
 
Kuna mpwa wangu mmoja kwa kweli nimetafuta thread yake sijawai kuiona tena alijitangaza kuwa ana ngoma, nadhani ilikua ina title ya UKIMWI bila Pesa ni Mateso
 
UKIMWI hauwezi kuisha kwa maneno maneno ya promo mpaka dawa yake ipatikane kwakua umekaa sehemu mbaya nzuri sana ambayo kila mtu anaipenda na vigumu mno kuepuka hiyo sehemu manake ni tamu kuliko vitu vyote duniani.Mimi siamini hata kidogo kua promo zitaumaliza UKIMWI.
 
Jamani tuangalie na maoni yetu kuna watu pia wameathirika sasa ikawa nao wanasoma haya maoni inakuaje
 
Ukimwi hamna siku hizi. Niambie toka umepata akili ulishawahi kumuona mgonjwa wa ukimwi?
 
Back
Top Bottom