Ukikamatwa na Afisa wa LATRA barabarani, tulia kama unanyolewa. Sheria imewapa nguvu sana

Ukikamatwa na Afisa wa LATRA barabarani, tulia kama unanyolewa. Sheria imewapa nguvu sana

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
26,662
Reaction score
59,100
Tanzania bora ukamatwe na Polisi sio LATRA. Kwanza hawahongeki, hawazoeleki, hawaonei wala hawana huruma.

Hata haya mambo ya Foleni wakiachiwa kazi LATRA, mambo yatanyoka.
logo-sw.png

Afisa huyo wa LATRA akikukamata, atakusalimia kisha atakuomba kukukagua.

Mfano kwa wanaobeba abiria, atakagua utekelezaji wa masharti ya leseni kama vile;

1. Dereva umethibitishwa?
2. Mhudumu umesajiliwa?
3. Dereva umevaa sare?
4. Gari lina leseni hai ya LATRA au kibali?
5. Gari lipo kwenye ruti yake?
6. Gari limefuata ratiba?
7. Kondakta anatoa tiketi za kielektroniki?
8. King'amuzi kimechezewa?
9. Abiria wamepewa tiketi?
10. Abiria wametozwa nauli halali?
11. Kama ni daladala limewekwa mkanda? Na kuonesha linapotoka na linapokwenda?
12. Na masharti mengine mengi kadiri yanavyotolewa na kanuni mbalimbali.

Ambacho Afisa wa LATRA haruhusiwi kukagua tu ni usalama wa gari yaani (Roadworthiness) mara nyingi huitwa "Uwezo wa gari kutembea barabarani" au "Hali ya gari kufaa barabarani") ni hali ya chombo cha moto (gari, basi, lori, n.k.) kuwa katika hali nzuri ya kiufundi na kiusalama inayokubalika kisheria ili kuendeshewa barabarani bila kuhatarisha maisha ya watumiaji wengine. Roadworthiness ni jukumu la Polisi.

Je, ushawahi kukutana Afisa wa LATRA? Ulijinasuaje?
 
Wanakua na bunduki??
LATRA sio Jeshi. Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) ni Mamlaka ya Serikali ambayo imejizatiti kusimamia sekta ya usafiri wa ardhini, hasa usafirishaji wa mizigo na abiria (mabasi ya mjini, mabasi ya njia ndefu, magari ya mizigo, teksi, pikipiki za magurudumu mawili na pikipiki za magurudumu matatu), usafiri wa Reli na usafiri wa Waya.. Mara nyingi wanaongozana na Polisi.. Ila wao sijawahi kuona wakiwa na bunduki.
 
Hakuna kitu hapo, wamejitengenezea kamradi ka kula rushwa na polisi
Kuna mizani wako na polisi, kuna TRA wako na polisi, kuna hifadhi ya misitu wako na polisi, na hao nyongeza
Si muda mrefu kutakuwa na TBS nao wanakamata magari yasio na viwango
 
Ni sahihi,mara nyingi huambatana na POLICE katika utendaji wao wa kazi,nadhani hawana hiyo POWER ya kusimamisha gari( I stand to be corrected)..ila walau kazi yao,huwa inaonekana hasa kipindi cha Sikukuu za mwisho wa Mwaka...

Wito wangu kwao, waongeze tu kasi ya Utendaji hata misimu mingine ya Mwaka na wasibase sana Mjini
 
Achana na LATRA kuna hawa wa parking siku hizi wametufuata majumbani imaging unapack gateni kwako anakuja mtu anascan...
kuna mmoja nusu nimpige na jinsi alivyo kiazi nikamkuta tena mara ya pili anascan, namuuliza anasema boss katuambia hii barabara inatoka hivyo tupite pia huku.

Hii haikubaliki kabisa kuja majumbani najiuiza wanafanya usafi huku hapana aisee
 
Nimeishia hapo!.

Bongo hiyo hiyo ama?
Mkuu, tupe Ushuhuda. LATRA washawahi kukuomba Rushwa? Kuwa muwazi tu sababu tupo hapa kupeana maarifa..

Kama hujawahi ombwa Rushwa, kipi kinafanya uhisi wanspokea Rushwa pale unapoingia 18 zao?
 
Hakuna kitu hapo, wamejitengenezea kamradi ka kula rushwa na polisi
Kuna mizani wako na polisi, kuna TRA wako na polisi, kuna hifadhi ya misitu wako na polisi, na hao nyongeza
Si muda mrefu kutakuwa na TBS nao wanakamata magari yasio na viwango
Nahisi tunaongea vitu Tofauti.. LATRA wanahusikaje na misitu? Nifafanuliie..
Pili kuwepo sio tatizo. Nataka kujenga hoja au challenge. Je, kuna Mtubl wa LATRA kashawahi kukuomba Rushwa.. Acha kusema TRA na Polisi. Jikite kwenye hoja... Tusiwabebeshe mizigo ya watu wengine..

Hili jukwaa ni huru. Tupeni ushuhuda wa jinsi wamepokeea Rushwa.. Mimi sijawahi kusikia
 
LATRA sio Jeshi. Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) ni Mamlaka ya Serikali ambayo imejizatiti kusimamia sekta ya usafiri wa ardhini, hasa usafirishaji wa mizigo na abiria (mabasi ya mjini, mabasi ya njia ndefu, magari ya mizigo, teksi, pikipiki za magurudumu mawili na pikipiki za magurudumu matatu), usafiri wa Reli na usafiri wa Waya.. Mara nyingi wanaongozana na Polisi.. Ila wao sijawahi kuona wakiwa na bunduki.
Kusema imejizatiti ni kuwapa sifa ambazo hawana,swali rahisi tu!

Hapo juu main post hiyo #11 daladala ngapi zimewekwa mikanda?hao nao wanafanya kazi kwa style ya zimamoto tu hawana lolote sema sheria zao zinawapa upana wa kukutana na pesa nje nje maana barabarani Tanzania hii hakuna gari iliyokamilisha vyote hivyo
 
Hakuna kitu hapo, wamejitengenezea kamradi ka kula rushwa na polisi
Kuna mizani wako na polisi, kuna TRA wako na polisi, kuna hifadhi ya misitu wako na polisi, na hao nyongeza
Si muda mrefu kutakuwa na TBS nao wanakamata magari yasio na viwango
Ndiooooooooooo
KAZI ni kipimo cha utu
 
Hapo kwenye hawahongeki ndo nimechoka kabisa.
Rushwa Iko kwenye DNA ya mbongo mkuu na hii sio kulaumu viongozi maana ni tatizo linaanzia kwenye familia zetu.
Kiufupi kuibadilisha hii nchi inahitaji kazi ya ziada vinginevyo labda huijui hii nchi vzr
 
Back
Top Bottom