Ukifika Capetown utashangaa sana

Ukifika Capetown utashangaa sana

Hapo ni Table mountain, kuna hotel hapo juu unapanda kwa cable kufika hapo na unaliangalia jiji lote la Cape Town kwa chini na bahari zotebili unaziona Indian ocean east na Antrantic ocean west cost.
Sijafika South, Mungu anipe uhai japo siku moja nifike huko hasa Cape Town kwani ni mji unaonivutia sana nikiona makala mbalimbali za mandhari yake.
 
Mkuu kuna kitu hukielewi, Wangoni na wayao wa Tanzania asili yao ni South Africa.

Nitarudi hapa kukupa darasa kuna sehemu nawahi kwanza.
Pia akina Sykes babu zake Dulla ni wa kutoka South,ikumbukwe zamani hakukuwa na viza na muingiliano wa makabila ulikuwa mkubwa sana,ndio kama hao Wangoni,Wamakua,Wayao,Wamakonde na ndio maana hata ukienda India utawakuta watu wanaitwa Sidi(?) wanaongea lugha inayofanana na Kiswahili,inaaminika walitoka ukanda wa pwani wa Afrika Mashariki kwa hiyo uko sawa mkuu labda huyu anayepinga hajui hata historia ya makabila na muingiliano wa watu.
 
Ngoja mimi nikufupishie, Dunia nzima kazi ni connection yako na network yako tu.

Wabongo wanafanyakazi kwenye sekta zote kasoro serikalini tu, hii inadepand who are you na who is ur friends.

Wanasemaga show me ur friends then i will tell u who you are....

Kama company yako ni wa dizaini fulani ukienda nchi walipo kampani yako utafanyakazi wanazofanya wao, formula iko hivyo.

Kitu cha ziada kwenye maisha kuna bahati, hii God given unaweza kukutana na network ambayo hukuitegemea na hata uliowakuta wakakushangaa, maisha yanachange na mambo yananyooka.

Nikupe tofauti kubwa ya Nigerians na Watanzania, tofauti kubwa ni hii

Mtanzania aliyekimbia shule anaweza kujipa matumaini akifika South Africa mambo tambarare bila ya kuwa na network au connection yoyote mwisho wa usiku usishangae kukumkita kaajiliwa na Mnigeria kwenye salon au kuuza matunda.

Tofauti na Wanigeria wengi niliowaona mimi nchi ile siyo Teenegers, ni watu wazima tena hadi wazee wenye exposure kubwa, unakuta mtu amesafa Uk kama 20 years amepiga hesabu zake ameona kwa mkaburu hesabu zake zitalipa unawakuta dizaini hiyo wapo wengi, wana network worldwide.

Ni ngumu kwa Mbongo eti atoke Marekani aende kuhamishia maskani yake South Africa kwakuwa anayo capital na ameiona fursa.

Kwa kifupi tofauti yetu na wao ni hiyo, wao hakuna school boys kule ni watu wazima wanaojitambuwa na wanajuwa wanatafuta nini.

Mnigeria hawezi kuuza matunda, lakini anaweza kumuajiri mtu amuuzie matunda yeye anaendelea na mishe nyingine zenye akili.

Yale mambo ile ela tuma kwenye namba hii wenzetu walifanya miaka ya 90 wakati internet ndio inaingia Africa.
Wazee wa Kitanzania wanaoishi Marekani wengi wao wamekimbilia u pastor,kila mtu ana kanisa lake,hawana ndoto yoyote ya kutafuta pesa ili waweze kuwasiaidia ndugu zao kama wanaijeria,hata wanaijeria wana makanisa yao lakini ni wajanja ndio maana wana makanisa karibu kila pembe ya dunia,hayo makanisa yanawasaidia kupata vibali ,kunetwork na kufanya mambo yao chini ya zuria.Kwa kifupi wazee wa Kitanzania wanaoishi nje ni kama wameshajikatia tamaa,tena baadhi yao ni wasomi wazuri na walikuwa na kazi nzuri sasa wamebaki kuwa mashabiki wa Chadema kutwa wapo mitandaoni,lakini hilo sio tatizo ,tatizo ni kuwa hawapigi hatua zozote za maendeleo si huko ughaibuni au hapa Tanzania na mwishowe hata vijana wao wanafuata tabia hiyo hiyo.
 
Ninashukuru tu nilikaa huo huo mwaka Mmoja tu wa 2004 hapo Chuoni UCT nikarejea 'Bongo' ila kwa 'Mbunye' za huko sasa 'Ngoma' ingeshaniua.
Mtaalam toka nilipo ingiaga cheeky tiger, bree and Simmonds street jozi pale.sijawahi tena kuluka vihunzi vya hizo makitu
 
Waswahili mna maneno ptyuuxx eti ''Beberu''! badala ya'' bana Kuba!"
 
wana iga iga tu, wanalambalamba tu, mpaka zitafunwe na machine weee, ni leo? Mkurya anakupigia kibeberu kizima na miguu yake mbuzi choma jino kwa jino unalinganisha kilo3? na pia hii ina faida nyingi. km unaimarisha meno na taya. na ni mswaki unapiga hutanuka mdomo!, pia una activate enzymes, ni "kichure" siyo kichuri. Kinatokana na mnyama aliye chinjwa kiungo hiki kinaongeza chachu ya ulaji, utamu asilia na kuepusha Blood cholestralaemia -lehemu.Gout, oesteomylitis, HBP,baridi yabisi nk, ndiyo maana jamii zao hazina magonjwa hayo. Wamasai, wakurya, wachaga, wajita, watusi, wamaharic nk wamekula nyama karne nyingi mpaka leo lkn hawana hayo matatizo.ajili ya kiungo cha kichure. Lkn wanao fakamia kichwakichwa km hao ni wateja wa ma-Cardiologists. Nenda umasaini hakuna tabibu wa hivi. na masai wanakula mpaka nundu na supu yake yoteee! Wazee wetu wana akili sana waliwaza mbona mbuzi mwenye mafuta hana gout? Jibu likaja kichure!!
Mkoo acha uongo,nafikiri wachaga wengi watu wazima wanaumwa sana gout.
Pia usiseme umasaini hamna magonjwa kama hayo wakati hawafanyi diagnosis
 
Mkoo acha uongo,nafikiri wachaga wengi watu wazima wanaumwa sana gout.
Pia usiseme umasaini hamna magonjwa kama hayo wakati hawafanyi diagnosis
Siyo uongo Mkuu, ni ukweli nasema, kuhusu wala nyama wenye Gout, Hypertension, IDDM nk, nimeshajibu mkuu, sema tu hujafuatilia uzuri!
 
South ni nchi ya 11 kwa meat consumption Duniani, Nyie Kichuri unawekewa kwenye kibakuli hiyo ni nyama? Mtu anapeleka karibia kilo nzila na hiyo ni kila siku
Nilitembelea machinjio ya J/Bug miaka 20 iliyopita ina uwezo wakuchinja ngombe 1200 kwa siku. Nyama ile nzuri hohehahe huwezi kununua. Wametengenezewa kitu kama soseji kubwa itokanayo na vinyamanyama vinapururwa ktk nyama nzuri ili ionekane nzuri inachanganywa na damu. hii hupikwa mithili ya kisusio na kufungwa kama mabomu ya hapa tz. Ndio hiyo wanayosema. Nyama ya maana kama loin au ya kiuno sahau kuila mtu wa kawaida.
 
Back
Top Bottom