Ukifika Capetown utashangaa sana

Ukifika Capetown utashangaa sana

Ngoja mimi nikufupishie, Dunia nzima kazi ni connection yako na network yako tu.

Wabongo wanafanyakazi kwenye sekta zote kasoro serikalini tu, hii inadepand who are you na who is ur friends.

Wanasemaga show me ur friends then i will tell u who you are....

Kama company yako ni wa dizaini fulani ukienda nchi walipo kampani yako utafanyakazi wanazofanya wao, formula iko hivyo.

Kitu cha ziada kwenye maisha kuna bahati, hii God given unaweza kukutana na network ambayo hukuitegemea na hata uliowakuta wakakushangaa, maisha yanachange na mambo yananyooka.

Nikupe tofauti kubwa ya Nigerians na Watanzania, tofauti kubwa ni hii

Mtanzania aliyekimbia shule anaweza kujipa matumaini akifika South Africa mambo tambarare bila ya kuwa na network au connection yoyote mwisho wa usiku usishangae kukumkita kaajiliwa na Mnigeria kwenye salon au kuuza matunda.

Tofauti na Wanigeria wengi niliowaona mimi nchi ile siyo Teenegers, ni watu wazima tena hadi wazee wenye exposure kubwa, unakuta mtu amesafa Uk kama 20 years amepiga hesabu zake ameona kwa mkaburu hesabu zake zitalipa unawakuta dizaini hiyo wapo wengi, wana network worldwide.

Ni ngumu kwa Mbongo eti atoke Marekani aende kuhamishia maskani yake South Africa kwakuwa anayo capital na ameiona fursa.

Kwa kifupi tofauti yetu na wao ni hiyo, wao hakuna school boys kule ni watu wazima wanaojitambuwa na wanajuwa wanatafuta nini.

Mnigeria hawezi kuuza matunda, lakini anaweza kumuajiri mtu amuuzie matunda yeye anaendelea na mishe nyingine zenye akili.

Yale mambo ile ela tuma kwenye namba hii wenzetu walifanya miaka ya 90 wakati internet ndio inaingia Africa.

Wala ujapindisha kitu nigeriens ni wapambanaji haswa
 
Hapo ni Table mountain, kuna hotel hapo juu unapanda kwa cable kufika hapo na unaliangalia jiji lote la Cape Town kwa chini na bahari zotebili unaziona Indian ocean east na Antrantic ocean west cost.

Mzee mzima check facts zako vizuri! Hicho kilichopo milimani ni restaurant tu, hamna hotel, na unaweza kufika kwa kuhike pia, si lazma cable car pekee. Milima inayoonekana kwenye hiyo picha, huu wa kwanza unaofanana na "seal" unaitwa Lion's Head japo pia upo ndani ya hifadhi ya table mountains.

Pia upande huu hakuna Indian Ocean hata kidogo.
 
Nilitembelea machinjio ya J/Bug miaka 20 iliyopita ina uwezo wakuchinja ngombe 1200 kwa siku. Nyama ile nzuri hohehahe huwezi kununua. Wametengenezewa kitu kama soseji kubwa itokanayo na vinyamanyama vinapururwa ktk nyama nzuri ili ionekane nzuri inachanganywa na damu. hii hupikwa mithili ya kisusio na kufungwa kama mabomu ya hapa tz. Ndio hiyo wanayosema. Nyama ya maana kama loin au ya kiuno sahau kuila mtu wa kawaida.
Ngoja nikutowe ushamba, hiyo inaitwa Buravozi inatamkwa hivyo, hata Bongo kwenye super market zipo.

Nyama siyo issue south Africa labda uongee jambo lingine.

Wao ndio wanaongoza kwa kula nyama Africa nzima.
 
Ngoja nikutowe ushamba, hiyo inaitwa Buravozi inatamkwa hivyo, hata Bongo kwenye super market zipo.

Nyama siyo issue south Africa labda uongee jambo lingine.

Wao ndio wanaongoza kwa kula nyama Africa nzima.
Nashukuru kunipa jina lake kamili. Wangesema mm nawashika na kamba ya uwongo. Wasiyadharau mabomu ya hapa mmesikia wenzetu wanavyoongoza kwa kula nyama. Nyama ni nyama tu mradi isiwe na ugonjwa.
 
Nashukuru kunipa jina lake kamili. Wangesema mm nawashika na kamba ya uwongo. Wasiyadharau mabomu ya hapa mmesikia wenzetu wanavyoongoza kwa kula nyama. Nyama ni nyama tu mradi isiwe na ugonjwa.
Bado unapotosha, hizo buravozi zipo ni very cheapest price, lakini nyamba nyingine zipo kama kawaida, tena mabucha yao mbele kuna brai mashine,. Unanuwa gram unazotaka unapewa nafuta unachoma mwenyewe nje kwenye brai mashine na ugali unauzwa hapohapo take away maisha yanaendelea

Kimsingi mfumo wa South Africa usipokula nyama labda una matatizo binafsi tu kama uric acid.

Hata Bongo mshikaki unaanzia mia tano mpaka buku mbili ile ya fillet na nundu.
 
Back
Top Bottom