Kumbe yale mabasi ambayo mbowe aliwauzia ndiyo ambayo mnayatumia kuwabeba kazaneni sana.
Lipumba hajawahi kushinda uchaguzi wowote toka kuzaliwa kwake
Mkuu Bramo, usitatizwe na like zangu, ni appreciation tuu!, wenzenu tumejaaliwa moyo wa ku appreciate vyote, vizuri, vibaya, vidogo vikubwa, vya maana vya kipuuzi na hata nikitukanwa humu, huwa sirudishi matukano bali hurudisha like nikimaanisha thanks!.Malimu ndo nini sasa?
Hii post ni ya kama mtu aliyeishia Std 6,halafu Pasco unagonga like bila haya
Hata wakalishe mgombea mmoja ni yaleyale hakuna mgombea urais upinzani wote wahuni na wenye kuangalia maslahi binafsi tu wala siyo kitu kingine.VYAMA vya upinzani vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) vimekubaliana kusimamisha mgombea mmoja urais 2015 na vitasaini makubaliano.
Source: NIPASHE Breaking news via sms.
Hata hivyo juzi (17/10/2014) nilihudhuria mkutano wa CHADEMA uliofanyika Mwananyamala Msisiri. Hayo aliyasema Mh. Wenje mbunge wa Mwanza kwamba wapo katika makubaliano ya kusimamisha mgombea mmoja mwenye kukubalika ambaye atatoka katika UKAWA kila jimbo, kata na hadi urais.
Hakuna chama wahuni na washenzi wakubwa duniani kama ccm .UKAWA NI SUMU YA KUUWA CCM NA VIBARAKA WAKE WOTE PAMOJA NA WWHata wakalishe mgombea mmoja ni yaleyale hakuna mgombea urais upinzani wote wahuni na wenye kuangalia maslahi binafsi tu wala siyo kitu kingine.
Ni kweli kabisa muungano wa vyama vitatu vikubwa vya upinzani ndo njia sahihi ya kuiondoa madarakani serikali ya ccmitasaidia sana tu,kumbuka 2010 kuna majimbo ccm walishinda kwa kura chache,sasa pale ukiongeza na za nccr na cuf,lazima wakae!mfano shinyana masele alishinda kwa kura moja!
ndoto za alinacha zinawasumbua...uarafiki huo ni wa mashaka watavurugana muda si mrefu wapeni miezi miwili tu mbele
Jibu swali acha porojo sheria ya vyama vya siasa chama chenye idadi kubwa ya wabunge kinapata ruzuku nyingi, sasa nauliza chama kipi kitachukua ruzuku nyingi.
kwa mujibu wa gazeti la mwananchi, ukawa wana mpango wa kuweka mgombea urais 2015
- aidha, wana mpango wa kusimamisha mgombea ubunge mmoja katika majimbo
- mbowe, mbatia na lipumba wazungumza na kudai ni mapema mno kutoa maelezo juu ya umoja wao!
- vyama vimeshapeleka mapendekezo kwenye sekretarieti za vyama husika kwa ajili ya kufanyiwa uchambuzi wa kufanikisha hili
- mbowe adai kuunganisha nguvu ya vyama vya upinzani ni suala ambalo halikwepeki kwakuwa siasa za sasa ni dynamic (zinabadilika) na fikra za jana ni tofauti na za leo.
- lipumba adai katiba imewaunganisha wapinzani na kuongeza kuwa huu ni mwanzo mzuri unaoweza kutoa mwanga wa nini kitatokea mbeleni.
- mbatia asisitiza kuwa suala la wapinzani kuungana si la kujadili maana ndiyo mahitaji ya wananchi kwa sasa!
Ni jambo jema lakini waende kwa umakini mkubwa.
Tunaelekea mahala pazuri sasa