Wewe Kinjikitile unahangaishwa na majimbo 12 wakati bunge lijalo ni wabunge zaidi ya 600, hiyo haiwezi kuwa sababu ya watu kushindwa kuafikiana, hata wakisema ngoja haya majimbo kila mmoja awe kivyake ila huku tulikokubaliana iwe hivyo bado ni turufu ya maana kwao na sidhani kama itawapunguzia nguvu kama wakipenda kubaki na nguvu zao. Wengi tuna mihemko ya kisiasa na agenda za kiitikadi, ila hatima ya Tanzania itakayoleta maendeleo kwa wananchi wake wala si UKAWA au CCM au chama kimoja wapo, ila mifumo inayoweza kulindwa pale mshika usukani anapojisahau na kuona kama ni yeye peke yake anaweza kuwa dereva...lazima wawepo wengine wakumwambia katika hili lazima ubadili gear uweze kupanda mlima. Hivyo upinzani mimara ni maendeleo pia ya nchi yetu, upinzani dhaifu ni liache liende ndani ya yeyeote atakayekuwa amekabidhiwa mamlaka ya kutawala. Ukiangalia mkakati ya reli ya Kenya toka Mombasa hadi Kampala, Kigali, Bujumbura na Kisangani unatuondoa kwenye SOUTHERN CORRIDOH yaani Zambia, DRC maana Musumbiji na Zimbabwe wanapumulia mitaji ya SA, sisi tutakuwa na nguvu tu endapo tutakuwa na uchumi wa kwenda kote kaskazini kwenye East DRC na kusini Zambia na Lubumbashi. Masoko madogo madogo kama Rwanda na Burundi (volume ya watu milioni kama 15 twaweza kugawana wa wakenya halafu Uganda nayo tukagawana na Kenya na tukapata Southern Sudan kabla haijaingiliwa na wengine). Tusipokuwa na upinzani imara hatufiki kokote maana siasa zetu ni za kibinafsi mno na hii inaligharimu taifa kwa masuala ya maendeleo hasa kwa vijaji vijavyo maana kizazi chetu kitakuwa cha kuishia kunywa maji haya haya machafu na umeme usiokuwa na uhakika. Tuimarishe CCM ndiyo, tuimarishe pia na upinzani ili dereva yeyote aweze kushtuliwa anavyotupeleka vibaya na akasikia kwa nguvu ya kura za wabunge wasioweza kufanya maamzi wao pekee yao kama tulivyo kwa sasa hapa Tz.