UKAWA kusambaratika kabla ya Oktoba

UKAWA kusambaratika kabla ya Oktoba

Umoja hakuna itakuwa historia kuwa kulikuwepo na dude lilijulikana kama ukawa kwa maana huwezi kukiita chama, wala ngo, wala shirikisho, ni jitu wala halijasajiliwa popote. Ukawa, ukatoweka,
au ukaisha n kupotea

Genge hilo la ukawa ni la aina yake, kuna watu wanawadanganya sana wenzao juu ya matamanio yao wakihitaji kuungwa mkono ili wafikie wanachotamani. Kumbe wenzao nao wameshajua janja ya nyani kula mahindi mabichi. Mihemko iko njiani maana wameshaanza kukwaruzana kutafuta nani zaidi.
 
siasa za ukawa zinawenyewe ukiwa na akili zimeyumba ukawa ndiyo mahala pake lakini kama wewe uko na utu wako utajitesa tu.
 
siasa za ukawa zinawenyewe ukiwa na akili zimeyumba ukawa ndiyo mahala pake lakini kama wewe uko na utu wako utajitesa tu.

Kweli zinawenyewe mkuu like this of Kiongozi wa KU BUNGENI na mchuma wa Serikali kwenye Peoples Money Use!! image.jpg
 
Kiongozi hiyo ndo shida yenyewe, ukiona malalamiko ujue kuna kansa inatafuna,Kama unabisha check uwiano wa uteuzi wa vyama vya ukawa ZNZ ndo utajua, ina maana nguvu ya vyama vingine iko bara, tena sio kubwa kiivyo sasa kwa mtaji huo hawatafikia lengo ni muungano maslahi.


mkuu wanaolalamika nawajua na tunajua ni nani aliyewatuma
 
Huo ni utafiti wa chini ya mwembe na hizo asilimia ulizoweka sijui umetoa wapi men????UKAWA ni maslahi nani asiyelijua hilo!wako kimkakati kupata mafao na ndo maana CCM muda wako inawamudu ,hizo mbio za kuelekea Ikulu Oktoba wasahau bora wafanye kazi nyingine tu ya kuimarisha chama!CUF zanzibar wameachia jimbo moja tu kwa Salum hilo ni pigo kwa UKAWA yenye chama zaidi ya komoja kuwa dominated ZNZ na huu upande mmoj wa muungano ni muhimu kwa maendeleo ya siasa kwa UKAWA, WENZAO CCM hawana shida kote wana coverage.

Kwa upande wa Serikali itakayoundwa hilo sitaki hata kulisemea maana muda wake utafika Oktoba, ninachojua UKAWA sio chama cha siasa hivyo hakitapewa ridhaa ya kuongoza nchi!Waendelee kujipanga tu mpaka watakaposajiliwa!!!!!!!
Ukawa ni sumu ya kuiondoa madarakani serikali ya wachovu ccm.
 
UKAWA KUVUNJIKA IKIWA CHADEMA WATALAZIMISHA KILA KITU WAPATE WAO.Mjumbe wa Baraza Kuu la UONGOZI Cuf Taifa Mhe Cheif Lutasa Yemba aliwahi kusema kuwa Kamwe yeye kama mjumbe wa Baraza Kuu la UONGOZI Cuf hawezi kukubali Chama Chake kuwa MSHUMAA wa Chadema.
Haiwezekani Chama kimoja kupata 50% ya majimbo kisha kipewe na haki ya kusimamisha mgombea wa URAIS huu ni mgawanyo wa kipumbavu na haukubaliki. haukubaliki haukubaliki kabisa, nitaupinga kwa nguvu zangu zote katika vikao vya chama.
Maamuzi mengine ndani ya UKAWA ni ya kijinga sana huwezi kukataa Chama kama ACT au ADC kujiunga na umoja huu wakati zana nzima ya umoja imeundwa kwa hoja kuwa KURA za wapinzani ukiziunganisha kwa pamoja tungeshinda majimbo mengi sana toka mwaka 2000 na 2010 ndio umuhimu wa kuungana ukapatikana.
Sasa ACT kinauwezo wa kuzuia vyama vyetu vyote sehemu nyingi sana kwa mtindo huo huo wa kugawana KURA na CCM wakaibuka washindi katika chaguzi 2015 huu ni upumbavu na haukubaliki kabisa.
Siasa haina adui wa kudumu wala rafiki wa kudumu ndio maana leo sisi Cuf tunakaa na Chadema na hata KAFULILA (mb) anafanya kazi pamoja na Chadema inashindikana vipi kufanya kazi pamoja na Zitto kwa nia ya kushiriki kuitoa CCM...?
Msimamo wangu kama Cheif Yemba vyama vyote vitakavyo hitaji kujiunga na umoja huu vipewe nafasi ili kuiondoa CCM madarakani 2015 na tuchague mgombea wa URAIS mwenye uwezo wa kuitoa CCM madarakani na uwezo wa kuwasaidia watanzania kwa weledi sio mtu wa hivyo hovyo tu hapana.
Hatuwezi kuwa mbadala waCCM kama ROHO zetu zimejengeka kwa CHUKI CHUKI tu bila kusamehe kuongoza nchi ni jambo linalo hitaji hekima na busara kubwa huwezi kuwa kiongozi wa watu na kuleta maendeleo na haki ukiwa ni mtu wa VISASI na CHUKI ya milele.
Kwanini wenzetu hawataki kuchagua kusimamisha majimbo mengi bila mgombea wa URAIS au kuwa na mgombea wa URAIS na majimbo machache ili kulinda RUZUKU kwa kila chama baada ya uchaguzi,.
KAMA HAYA HAYAWEZEKANI HAKUNA UKAWA NI BORA TUTAFUTE WASHIRIKA WAPYA SIO HAWA WAJANJA WAJANJA.

DONGO HILI LIMEPIGWA KWA CHADEMA NA UVHU WAO WA KUTAKA KILA KITU WAPEWE WAO! Umoja wao kusambaratika soon!
‪Source: Chief Lutasa Yemba.
Una kipaji cha kuimba taarabu mtafute Mzee Yusufu huenda ukatoka kimaisha kazi ya housegirl imekushinda .
 
siasa za ukawa zinawenyewe ukiwa na akili zimeyumba ukawa ndiyo mahala pake lakini kama wewe uko na utu wako utajitesa tu.

Uwezo wako wa kufikiria ndo umeishia hapo.
 
Mkuu usipate shida sana niambie majimbo tata 12 ya UKAWA mmeshapata wagombea?au bado zinapigwa!
Wewe Kinjikitile unahangaishwa na majimbo 12 wakati bunge lijalo ni wabunge zaidi ya 600, hiyo haiwezi kuwa sababu ya watu kushindwa kuafikiana, hata wakisema ngoja haya majimbo kila mmoja awe kivyake ila huku tulikokubaliana iwe hivyo bado ni turufu ya maana kwao na sidhani kama itawapunguzia nguvu kama wakipenda kubaki na nguvu zao. Wengi tuna mihemko ya kisiasa na agenda za kiitikadi, ila hatima ya Tanzania itakayoleta maendeleo kwa wananchi wake wala si UKAWA au CCM au chama kimoja wapo, ila mifumo inayoweza kulindwa pale mshika usukani anapojisahau na kuona kama ni yeye peke yake anaweza kuwa dereva...lazima wawepo wengine wakumwambia katika hili lazima ubadili gear uweze kupanda mlima. Hivyo upinzani mimara ni maendeleo pia ya nchi yetu, upinzani dhaifu ni liache liende ndani ya yeyeote atakayekuwa amekabidhiwa mamlaka ya kutawala. Ukiangalia mkakati ya reli ya Kenya toka Mombasa hadi Kampala, Kigali, Bujumbura na Kisangani unatuondoa kwenye SOUTHERN CORRIDOH yaani Zambia, DRC maana Musumbiji na Zimbabwe wanapumulia mitaji ya SA, sisi tutakuwa na nguvu tu endapo tutakuwa na uchumi wa kwenda kote kaskazini kwenye East DRC na kusini Zambia na Lubumbashi. Masoko madogo madogo kama Rwanda na Burundi (volume ya watu milioni kama 15 twaweza kugawana wa wakenya halafu Uganda nayo tukagawana na Kenya na tukapata Southern Sudan kabla haijaingiliwa na wengine). Tusipokuwa na upinzani imara hatufiki kokote maana siasa zetu ni za kibinafsi mno na hii inaligharimu taifa kwa masuala ya maendeleo hasa kwa vijaji vijavyo maana kizazi chetu kitakuwa cha kuishia kunywa maji haya haya machafu na umeme usiokuwa na uhakika. Tuimarishe CCM ndiyo, tuimarishe pia na upinzani ili dereva yeyote aweze kushtuliwa anavyotupeleka vibaya na akasikia kwa nguvu ya kura za wabunge wasioweza kufanya maamzi wao pekee yao kama tulivyo kwa sasa hapa Tz.
 
Back
Top Bottom