msumeno
JF-Expert Member
- Aug 3, 2009
- 2,827
- 1,729
Ukawa nionavyo mimi kwa uelewa wangu finyu...swala la katiba sio turufu inayoweza kuwafikisha ikulu..watanzania si kama wakenya..ingekuwa wakenya hata haya maadamano yalogeuka kama zile ngoma zetu za uswahilini za vigodoro au vile vigoma vya uruguayi yangekua na msisimko mkubwa na for sure watawala wangesalimu amri tu kwa nguvu ya umma. Lakini wengi wetu hata ile katiba tu ya kwanza hatuijui na wengine hata rangi ya cover tu hatulijui wacha kilichomo sasa katika mazingira haya kuwambia watu wakabiliane na police sio rahisi. Ingekua vyema kwanza mkatuelewesha maana ya katiba na athari zake kwa maisha yetu..maana nimewasikia wengine wakisema hata bila ya katiba naishi. Ukiangalia sana unaona kuwa ukawa wangekaa bungeni na kufanya upinzani wa kweli bungeni kwa hoja zenye kashiko wananchi wangewaelewa na popularity ingeogezeka sana kinyume na hivi sasa. Kibaya zaidi wakati wao wakiendelea na maandamano ya vigodoro ccm wao wanalamba vichwa vijijini. Hivi ukawa mmeshindwa kuliona hili?